< Mathayo 2 >

1 Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
Jezus urodził się w miasteczku Betlejem, w Judei, za panowania króla Heroda. Właśnie w tym czasie przybyli do Jerozolimy mędrcy ze Wschodu.
2 wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
—Gdzie znajduje się nowo narodzony Król Żydów?—pytali. —Ujrzeliśmy u nas, na Wschodzie, Jego gwiazdę i przybyliśmy złożyć Mu hołd.
3 Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
Wiadomość o tym bardzo zaniepokoiła Heroda i całą Jerozolimę.
4 Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
Zwołał więc wszystkich najwyższych kapłanów oraz przywódców religijnych i pytał, gdzie ma się narodzić Mesjasz.
5 Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
—W Betlejem w Judei—odpowiedzieli mu. —Bo tak napisał prorok
6 “‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
„A ty, Betlejem w Judzie, wcale nie jesteś najgorsze wśród miast Judy, gdyż z ciebie pochodzić będzie Władca, który będzie pasterzem mojego ludu—Izraela”.
7 Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
Wtedy Herod potajemnie wezwał do siebie mędrców i dowiedział się, kiedy ujrzeli gwiazdę.
8 Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
Następnie skierował ich do Betlejem mówiąc: —Idźcie i dokładnie wypytujcie o dziecko. Gdy je znajdziecie, powiadomcie mnie, abym i ja mógł złożyć mu hołd.
9 Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
Po rozmowie z królem mędrcy wyruszyli w drogę. Znowu ukazała się im gwiazda, którą zobaczyli na Wschodzie, i prowadziła ich. W końcu zatrzymała się nad miejscem, gdzie znajdowało się Dziecko.
10 Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
Widok gwiazdy napełnił ich ogromną radością.
11 Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
Gdy weszli do domu, zobaczyli Dziecko i Jego matkę, Marię. Pokłonili Mu się nisko, otworzyli szkatułki z kosztownościami i ofiarowali Mu w darze złoto, kadzidło oraz mirrę.
12 Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
Później we śnie otrzymali nakaz, by nie wracać do Heroda. Dlatego inną drogą udali się do swojego kraju.
13 Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
Gdy oddalili się, również Józefowi we śnie ukazał się anioł Pana: —Wstawaj, Józefie!—powiedział. —Weź Dziecko oraz Jego matkę i uciekaj do Egiptu. Czekaj tam, aż dam ci znać. Herod bowiem szuka Jezusa i chce Go zabić.
14 Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
Jeszcze tej nocy Józef wstał i wyruszył razem z Marią i Dzieckiem do Egiptu.
15 ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
Pozostał tam aż do śmierci króla Heroda—w ten sposób miały się spełnić słowa Pana wypowiedziane przez proroka: „Z Egiptu wezwałem mojego Syna”.
16 Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
Herod zorientował się, że mędrcy go zawiedli, i wpadł w gniew. Wysłał żołnierzy, którzy w Betlejem i całej okolicy pozabijali wszystkich chłopców do drugiego roku życia—od mędrców bowiem wiedział, w jakim wieku jest dziecko.
17 Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
Tak spełniło się proroctwo Jeremiasza:
18 “Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
„Krzyk rozlega się w Rama, słychać tam płacz i rozpacz. To Rachel opłakuje swoje dzieci i nie daje się pocieszyć, bo już ich nie ma”.
19 Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
Po śmierci Heroda anioł Pana ponownie ukazał się we śnie Józefowi, przebywającemu w Egipcie.
20 na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
—Wstawaj, Józefie!—powiedział. —Weź Dziecko i Jego matkę i ruszajcie do Izraela, bo umarli już ci, którzy chcieli Je zabić.
21 Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
Józef wstał, wziął Dziecko oraz Jego matkę i wyruszył do ziemi izraelskiej.
22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
W drodze dowiedział się, że w Judei panuje Archelaos, syn Heroda. Bał się więc tam wracać. Otrzymał jednak we śnie kolejne polecenie i udał się do Galilei.
23 akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”
Tam osiedlił się w Nazarecie. I znowu spełniła się zapowiedź proroków, mówiąca, że Mesjasz będzie nazwany Nazarejczykiem.

< Mathayo 2 >