< Mathayo 2 >

1 Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
Pärast Jeesuse sündimist Petlemmas Juudamaal, kuningas Heroodese valitsusajal, saabusid hommikumaalt pärit tähetargad Jeruusalemma.
2 wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
„Kus on see laps, kes sündis juutide kuningaks?“küsisid nad. „Me nägime ta tähte tõusmas ja tulime teda kummardama.“
3 Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
Seda kuuldes läks kuningas Heroodes ärevile ja kogu Jeruusalemm koos temaga.
4 Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
Ta kutsus kokku kõik juutide ülempreestrid ja kirjatundjad ning päris nende käest, kus Messias pidi sündima.
5 Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
Need vastasid talle: „Juudamaa linnas Petlemmas, sest nõnda on prohvet kirjutanud:
6 “‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
„Sina, Petlemm Juudamaal, ei ole vähim Juuda valitsejate seas, sest sinust võrsub Valitseja, kes mu rahvast Iisraeli karjatseb.““
7 Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
Siis kutsus Heroodes tähetargad salaja enda juurde ja uuris neilt välja aja, millal täht oli paistma hakanud.
8 Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
Seejärel läkitas ta nad Petlemma, öeldes: „Minge ja otsige last. Kui te ta leiate, siis teatage mulle, et minagi võiksin minna teda kummardama!“
9 Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
Tähetargad kuulasid kuninga ära ja asusid teele. Ja ennäe, täht, mille tõusu nad olid jälginud, juhatas neid, kuni jäi seisma selle paiga kohal, kus asus laps.
10 Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
Seda nähes rõõmustasid tähetargad väga.
11 Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
Nad astusid majja ja nägid last koos tema ema Maarjaga ning kummardusid ta ette maha. Siis avasid nad oma varalaekad ja andsid talle kinke: kulda, viirukit ja mürri.
12 Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
Ja saanud unenäos Jumalalt hoiatuse, et nad ei läheks enam Heroodese juurde, pöördusid nad teist teed pidi tagasi oma maale.
13 Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
Kui tähetargad olid lahkunud, ilmus Issanda ingel unenäos Joosepile ja ütles: „Tõuse üles, võta kaasa laps ja tema ema! Põgene Egiptusesse ja ole seal, kuni ma sulle ütlen; sest Heroodes hakkab otsima last, et teda hukata.“
14 Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
Joosep tõusis, võttis kaasa lapse ja tema ema ning põgenes öösel Egiptusesse.
15 ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
Seal viibis ta Heroodese surmani, et läheks täide, mida Issand oli öelnud prohveti kaudu: „Ma kutsusin oma poja Egiptusest.“
16 Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
Kui Heroodes nägi, et tähetargad olid teda petnud, sattus ta suurde raevu. Ta andis käsu hukata kõik poisslapsed Petlemmas ja kogu selle ümbruses: kaheaastased ja alla selle, vastavalt ajale, mille ta oli tähetarkadelt välja uurinud.
17 Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
Nii läks täide, mis oli öeldud prohvet Jeremija suu läbi:
18 “Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
„Raamas on kuulda häält, rohket nuttu ja hala. Raahel nutab taga lapsi ega lase end lohutada, sest neid ei ole enam.“
19 Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
Ent pärast Heroodese surma ilmus Issanda ingel Egiptuses viibivale Joosepile unenäos
20 na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
ja ütles: „Tõuse üles, võta kaasa laps ja tema ema ning mine Iisraelimaale! Need, kes lapse elu kallale kippusid, on nüüd surnud!“
21 Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
Joosep võttis lapse ja tema ema ning läks Iisraelimaale.
22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
Aga kui ta kuulis, et Arhelaos valitseb Juudamaad kuningana oma isa Heroodese asemel, kartis ta sinna minna. Ja saanud Jumalalt unenäos hoiatuse, suundus ta Galilea aladele
23 akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”
ning asus elama Naatsareti linna. Nii läks täide, mis oli öeldud prohvetite suu läbi: „Teda hüütakse Naatsaretlaseks.“

< Mathayo 2 >