< Mathayo 2 >
1 Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa utawala wa Mfalme Herode, wataalamu wa mambo ya nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu
Now when Jesus had been born in Bethlehem of Judaea, in the days of Herod the king, lo! there came magians from the East to Jerusalem,
2 wakiuliza, “Yuko wapi huyo aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi tumekuja kumwabudu.”
saying, Where is the king of the Jews that hath been born? for we saw his star in the East, and came to do him homage.
3 Mfalme Herode aliposikia jambo hili aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa Yerusalemu.
But when Herod the king heard of these things, he was troubled, and all Jerusalem with him;
4 Herode akawaita pamoja viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo angezaliwa.
and assembling all the chief priests and scribes of the people, he inquired of them where the Christ was to be born.
5 Nao wakamwambia, “Katika Bethlehemu ya Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa na nabii:
And they said to him, In Bethlehem of Judaea; for thus it is written by the prophet:
6 “‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, wewe si mdogo miongoni mwa watawala wa Yuda; kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala atakayekuwa mchungaji wa watu wangu Israeli.’”
“And thou Bethlehem, land of Judah, art by no means least among the princes of Judah; for out of thee shall come a ruler, who shall feed my people Israel.”
7 Ndipo Herode akawaita wale wataalamu wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao uhakika kamili wa wakati ile nyota ilionekana.
Then Herod, having privately called the magians ascertained from them exactly the time when the star appeared.
8 Kisha akawatuma waende Bethlehemu akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii huyo mtoto. Nanyi mara mtakapomwona, mniletee habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.”
And he sent them to Bethlehem, and said, Go and search carefully for the child; and when ye have found him, bring me word, that I also may go and do him homage.
9 Baada ya kumsikia mfalme, wale wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale alipokuwa mtoto.
When they had heard the king, they departed. And lo! the star, which they had seen in the East, went before them, till it came and stood over where the child was.
10 Walipoiona ile nyota wakajawa na furaha kubwa mno.
When they saw the star, they rejoiced with exceeding great joy;
11 Walipoingia ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja na Maria mama yake, wakamsujudu na kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za dhahabu, uvumba na manemane.
and when they had come into the house, they saw the child with Mary his mother, and fell down, and did homage to him; and opening their treasures, they presented him gifts, gold and frankincense and myrrh.
12 Nao wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa njia nyingine.
And having been warned by God in a dream not to return to Herod, they went back to their own country another way.
13 Walipokwisha kwenda zao, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kumtafuta huyu mtoto ili amuue.”
And when they had gone, lo! an angel of the Lord appeareth to Joseph in a dream, saying, Arise, and take the child and his mother, and flee into Egypt, and remain there until I speak to thee; for Herod will seek the child, to destroy him.
14 Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake wakati wa usiku, nao wakaenda Misri
And he arose, and took the child and his mother by night, and went to Egypt;
15 ambako walikaa mpaka Herode alipofariki. Hili lilifanyika ili litimie lile lililonenwa na Bwana kwa kinywa cha nabii kusema: “Nilimwita mwanangu kutoka Misri.”
and was there until the death of Herod; that it might be fulfilled which was spoken by the Lord through the prophet, saying, “I called my son out of Egypt.”
16 Herode alipongʼamua kwamba wale wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili, alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
Then Herod, when he saw that he had been deceived by the magians, was greatly enraged; and sent forth, and slew all the male children that were in Bethlehem, and in all its borders, from two years old and under, according to the time which he had ascertained from the magians.
17 Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia.
Then was fulfilled that which was spoken through Jeremiah the prophet, saying,
18 “Sauti ilisikika huko Rama, maombolezo na kilio kikubwa, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe, akikataa kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”
“A voice was heard in Ramah, weeping, and great mourning; Rachel weeping for her children, and refusing to be comforted, because they were no more.”
19 Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri
But when Herod was dead, lo! an angel of the Lord appeareth in a dream to Joseph in Egypt,
20 na kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama yake mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa mtoto wamekufa.”
saying, Arise, and take the child and his mother, and go to the land of Israel; for they who sought the child's life are dead.
21 Basi Yosefu, akaondoka akamchukua mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya Israeli.
And he arose, and took the child and his mother, and came into the land of Israel.
22 Lakini aliposikia kwamba Arkelao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa Herode baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda zake sehemu za Galilaya,
But when he heard that Archelaus was reigning in Judaea in the place of his father Herod, he was afraid to go thither; and being warned by God in a dream, he withdrew into the parts of Galilee,
23 akaenda akaishi katika mji ulioitwa Nazareti. Hivyo likawa limetimia neno lililonenwa na manabii, “Ataitwa Mnazarayo.”
and came and took up his abode in a city called Nazareth; that it might be fulfilled which was spoken through the prophets, “He will be called a Nazarene,”