< Mathayo 19 >

1 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani.
Or il arriva, quand Jésus eut achevé ces discours, qu'il partit de la Galilée et vint sur le territoire de la Judée, au delà du Jourdain.
2 Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.
De grandes foules l'y suivirent, et il guérit leurs malades.
3 Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
Alors les pharisiens s'approchèrent pour le mettre à l'épreuve, et ils lui dirent: Est-il permis de répudier sa femme, pour quelque sujet que ce soit?
4 Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke,
Il leur répondit: N'avez-vous pas lu que le Créateur, au commencement, fit un homme et une femme,
5 naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?
et qu'il dit: «C'est pourquoi, l'homme quittera son père et sa mère, et s'attachera à sa femme; et les deux ne feront plus qu'une seule chair»?
6 Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
Ainsi ils ne sont plus deux, mais une seule chair. Que l'homme ne sépare donc pas ce que Dieu a uni!
7 Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”
Ils lui dirent: Pourquoi donc Moïse a-t-il commandé de donner à la femme une lettre de divorce pour la répudier?
8 Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
Il leur répondit: C'est à cause de la dureté de votre coeur que Moïse vous a permis de répudier vos femmes; mais, au commencement, il n'en était pas ainsi.
9 Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”
Or, je vous le déclare, quiconque répudie sa femme, si ce n'est pour inconduite, et en épouse une autre, commet un adultère.
10 Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”
Ses disciples lui dirent: Si telle est la condition de l'homme à l'égard de la femme, il vaut mieux ne pas se marier!
11 Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu.
Il leur répondit: Tous ne sont pas capables d'accepter cette parole, mais seulement ceux à qui cela est donné.
12 Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”
Car il y a des eunuques qui le sont dès le sein de leur mère; il y en a qui ont été faits eunuques par les hommes, et il y en a qui se sont faits eunuques eux-mêmes pour le royaume des cieux. Que celui qui peut recevoir cette parole, la reçoive!
13 Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.
A ce moment, on lui présenta des petits enfants, afin qu'il leur imposât les mains et qu'il priât pour eux; et les disciples reprenaient ceux qui les présentaient.
14 Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.”
Mais Jésus leur dit: Laissez venir à moi les petits enfants, et ne les en empêchez point; car le royaume des cieux est pour ceux qui leur ressemblent.
15 Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.
Et, leur ayant imposé les mains, il partit de là.
16 Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
Alors un homme s'approcha et lui dit: Maître, que dois-je faire de bon pour avoir la vie éternelle? (aiōnios g166)
17 Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”
Jésus lui dit: Pourquoi m'interroges-tu sur ce qui est bon? Un seul est bon. Si tu veux entrer dans la vie, observe les commandements.
18 Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
— Lesquels? dit-il. — Jésus lui répondit: Ceux-ci: «Tu ne tueras point; tu ne commettras point d'adultère; tu ne déroberas point; tu ne diras point de faux témoignage;
19 waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”
honore ton père et ta mère»; et aussi: «Tu aimeras ton prochain comme toi-même.»
20 Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”
Le jeune homme lui dit: J'ai observé toutes ces choses; que me manque-t-il encore?
21 Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Jésus lui dit: Si tu veux être parfait, va, vends ce que tu as, donne-le aux pauvres, et tu auras un trésor dans le ciel; puis, viens et suis-moi.
22 Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Mais quand le jeune homme eut entendu cette parole, il s'en alla tout triste; car il avait de grands biens.
23 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni.
Alors Jésus dit à ses disciples: En vérité, je vous le déclare, un riche entrera difficilement dans le royaume des cieux.
24 Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Je vous le répète: Il est plus aisé qu'un chameau passe par le trou de l'aiguille, qu'il ne l'est à un riche d'entrer dans le royaume de Dieu.
25 Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
En entendant ces paroles, ses disciples furent extrêmement étonnés, et ils disaient: Qui donc peut être sauvé?
26 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
Jésus, les regardant, leur dit: Cela est impossible aux hommes; mais tout est possible à Dieu.
27 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”
Alors Pierre, prenant la parole, lui dit: Et nous, nous avons tout quitté, et nous t'avons suivi; qu'avons-nous donc à attendre?
28 Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
Jésus leur répondit: En vérité, je vous le déclare, au renouvellement de toutes choses, lorsque le Fils de l'homme sera assis sur le trône de sa gloire, vous qui m'avez suivi, vous serez de même assis sur douze trônes, jugeant les douze tribus d'Israël.
29 Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios g166)
Et quiconque aura quitté frères ou soeurs, ou père, ou mère, ou enfants, ou champs, ou maisons, à cause de mon nom, recevra beaucoup plus, et il héritera de la vie éternelle. (aiōnios g166)
30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Mais plusieurs des premiers seront les derniers, et plusieurs des derniers seront les premiers.

< Mathayo 19 >