< Mathayo 19 >
1 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani.
And it came to pass, when Jesus ended these words, he removed from Galilee and came into the bounds of Judaea beyond the Jordan.
2 Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.
And there followed him large multitudes, and he cured them there.
3 Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
And there came unto him Pharisees, testing him, and saying, —Whether is it allowed a man to divorce his wife, for every cause?
4 Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke,
And, he, answering, said—Did ye never read—He who created at the beginning, Male and female, made them, —
5 naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?
and said—For this cause, will a man leave his father and his mother, and be united to his wife, —and, the two, will become, one flesh;
6 Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
So that, the longer, are they, two, but, one flesh, What, therefore, God, hath yoked together, Let not, a man, put asunder.
7 Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”
They say unto him—Why then did, Moses, command, to give a writing of repudiation and to divorce?
8 Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
He saith unto them—Moses, in view of your hardness of heart, permitted you to divorce your wives; From the beginning however, hath it not been done, thus.
9 Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”
And I say unto you—Whosoever shall divorce his wife, saving for unfaithfulness, and shall marry another, committeth adultery.
10 Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”
The disciples say unto him—If, so, is the cause of the husband with the wife, it is not expedient to marry.
11 Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu.
But, he, said unto them—Not all, find room for he word, save they to whom it hath been given;
12 Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”
For there, are, eunuchs, who, from their mother’s womb, were born so, and there, are, eunuchs, who were made eunuchs, by men, —and there, are, eunuchs, who have made, themselves, eunuchs, for the sake the kingdom of the heavens: He that is able to find room, let him find room.
13 Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.
Then, were brought unto him children, —that he might lay his hands upon them, and pray. And, the disciples, rebuked them.
14 Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.”
But, Jesus, said—Suffer the children—and do not hinder them—to come unto me, —for, of such, is the kingdom of the heavens.
15 Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.
And, laying his hands upon them, he went his way from thence.
16 Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios )
And lo! one coming near unto him, said, Teacher! what good thing shall I do, that I may have life age-abiding? (aiōnios )
17 Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”
And, he, said unto him—Why dost thou question me concerning that which is good? There is, One, that is good! But, if thou desirest, into life, to enter, be keeping the commandments.
18 Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
He saith unto him, Which? Jesus, said—These: Thou shalt not commit murder, Thou shalt not commit adultery, Thou shalt not steal, —Thou shalt not bear false witness;
19 waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”
Honour thy father and thy mother, —and—Thou shalt love thy neighbour as, thyself.
20 Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”
The young man saith unto him—These all, have I kept, —What, further, do I lack?
21 Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
Jesus said unto him—If thou desirest to be perfect, Withdraw! sell thy substance, and give to the destitute, —and thou shalt have treasure in the heavens; and come! be following me.
22 Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
And the young man, hearing, this word, went away sorrowing, —for he was holding large possessions.
23 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni.
And, Jesus, said unto his disciples—Verily, I say unto you, A rich man, with difficulty, shall enter into the kingdom of the heavens.
24 Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Again I say unto you—Easier, is it for, a camel, through the eye of a needle, to enter, than a rich man—into the kingdom of God.
25 Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
And, hearing it, the disciples were being struck with the greatest astonishment, saying—Who then can be saved?
26 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
And, looking intently, Jesus said unto them—With men, this is, impossible, but, with God, all things are possible.
27 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”
Then, making answer, Peter said unto him—Lo! we, have left all, and followed thee, —What then shall there be, for us?
28 Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
And, Jesus, said unto them—Verily, I say unto you, As for you who followed me in the regeneration, When the Son of Man shall take his seat on his throne of glory, ye also, shall be seated upon twelve thrones, judging the twelve tribes of Israel.
29 Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios )
And, whosoever left houses, or brethren, or sisters, or father, or mother, or children, or lands, for sake of my name, manifold, shall receive, and life, age-abiding, shall inherit. (aiōnios )
30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
But many shall be—first-last, and last-first.