< Mathayo 19 >
1 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ngʼambo ya Mto Yordani.
At the conclusion of this teaching, Jesus withdrew from Galilee, and went into that district of Judea which is on the other side of the Jordan.
2 Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.
Great crowds followed him, and he cured them there.
3 Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”
Presently some Pharisees came up to him, and, to test him, said, “Has a man the right to divorce his wife for every cause?”
4 Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke,
“Haven’t you read,” replied Jesus, “that at the beginning the Creator ‘made them male and female,’
5 naye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’?
and said – ‘For this reason a man will leave his father and mother, and be united to his wife, and the man and his wife will become one’?
6 Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
So that they are no longer two, but one. What God himself, then, has yoked together people must not separate.”
7 Wakamuuliza, “Kwa nini basi Mose aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na kumwacha?”
“Why, then,” they said, “did Moses direct that a man should serve his wife with a notice of separation and divorce her?”
8 Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.
“Moses, owing to the hardness of your hearts,” answered Jesus, “permitted you to divorce your wives, but that was not so at the beginning.
9 Mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati naye akaoa mke mwingine, anazini. Naye amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia anazini.”
But I tell you that anyone who divorces his wife, except on the ground of some serious sexual sin, and marries another woman, is guilty of adultery.”
10 Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali mtu asioe!”
“If that,” said the disciples, “is the position of a man with regard to his wife, it is better not to marry.”
11 Yesu akawaambia, “Si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu.
“It is not everyone,” replied Jesus, “who can accept this teaching, but only those who have been enabled to do so.
12 Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo; wengine wamefanywa matowashi na wanadamu; na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”
Some men are incapable of marriage because they were born that way, or have been made so by other people, while there are others who stay single for the sake of the kingdom of Heaven. Accept this if you can.”
13 Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na awaombee. Lakini wanafunzi wake wakawakemea wale waliowaleta.
Then some little children were brought to Jesus, for him to place his hands on them, and pray; but the disciples found fault with those who had brought them.
14 Yesu akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio kama hawa.”
Jesus, however, said, “Let the little children come to me, and do not hinder them, for it is to the childlike that the kingdom of heaven belongs.”
15 Naye akaweka mikono yake juu yao, na akaondoka huko.
So he placed his hands on them, and then went on his way.
16 Mtu mmoja akamjia Yesu na kumuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios )
A man came up to Jesus, and said, “Teacher, what good thing must I do to obtain eternal life?” (aiōnios )
17 Yesu akamjibu, “Mbona unaniuliza habari ya mema? Aliye mwema ni Mmoja tu. Lakini ukitaka kuingia uzimani, zitii amri.”
“Why ask me about goodness?” answered Jesus. “There is but One who is good. If you want to enter the life, keep the commandments.”
18 Yule mtu akamuuliza, “Amri zipi?” Yesu akamjibu, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,
“What commandments?” asked the man. “These,” answered Jesus, – “‘You must not kill. You must not commit adultery. You must not steal. You must not say what is false about others.
19 waheshimu baba yako na mama yako, na umpende jirani yako kama nafsi yako.”
Honor your father and your mother.’ And ‘You must love your neighbor as you love yourself.’”
20 Yule kijana akasema, “Hizi zote nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?”
“I have observed all these,” said the young man. “What is still wanting in me?”
21 Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze vitu vyote ulivyo navyo, na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
“If you wish to be perfect,” answered Jesus, “go and sell your property, and give to the poor, and you will have wealth in heaven; then come and follow me.”
22 Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
On hearing these words, the young man went away distressed, for he had great possessions.
23 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Amin, nawaambia, itakuwa vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni.
At this, Jesus said to his disciples, “I tell you that a rich person will find it hard to enter the kingdom of heaven!
24 Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
I say again, it is easier for a camel to get through a needle’s eye than for a rich person to enter the kingdom of heaven!”
25 Wanafunzi wake waliposikia haya, walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
On hearing this, the disciples exclaimed in great astonishment, “Who then can possibly be saved?”
26 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
But Jesus looked at them, and said, “With people this is impossible, but with God everything is possible.” Then Peter turned and said to Jesus,
27 Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata! Tutapata nini basi?”
“But we – we left everything, and followed you; what, then, will we have?”
28 Yesu akawaambia, “Amin, nawaambia, wakati wa kufanywa upya vitu vyote, Mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake kitukufu cha enzi, ninyi mlionifuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
“I tell you,” answered Jesus, “that at the new creation, when the Son of Man takes his seat on his throne of glory, you who followed me will be seated on twelve thrones, as judges of the twelve tribes of Israel.
29 Kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu zake wa kiume au wa kike, baba au mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo, na ataurithi uzima wa milele. (aiōnios )
Everyone who has left houses, or brothers, or sisters, or father, or mother, or children, or land, for my sake, will receive many times as much, and will gain eternal life. (aiōnios )
30 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
But many who are first now will then be last, and those who are last will be first.