< Mathayo 18 >

1 Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
At the same time came the disciples to Jesus, saying, Who is the greatest in the kingdom of heaven?
2 Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
And Jesus called a little child to him, and set him in the midst of them,
3 Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
And said, Verily I say to you, Except ye be converted, and become as little children, ye shall not enter into the kingdom of heaven.
4 Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
Whoever therefore shall humble himself as this little child, the same is greatest in the kingdom of heaven.
5 “Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
And whoever shall receive one such little child in my name, receiveth me.
6 Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
But whoever shall cause one of these little ones who believe in me, to sin, it were better for him that a millstone were hanged about his neck, and [that] he were drowned in the depth of the sea.
7 “Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
Woe to the world because of offenses! for it must needs be that offenses come; but woe to that man by whom the offense cometh!
8 Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
Wherefore, if thy hand or thy foot causeth thee to sin, cut them off, and cast [them] from thee: it is better for thee to enter into life halt or maimed, rather than having two hands or two feet, to be cast into everlasting fire. (aiōnios g166)
9 Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
And if thy eye causeth thee to sin, pluck it out, and cast [it] from thee: it is better for thee to enter into life with one eye, rather than having two eyes, to be cast into hell-fire. (Geenna g1067)
10 “Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
Take heed that ye despise not one of these little ones: for I say to you, that in heaven their angels do always behold the face of my Father who is in heaven.
11 Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
For the Son of man is come to save that which was lost.
12 “Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
How think ye? if a man hath a hundred sheep, and one of them is gone astray, doth he not leave the ninety and nine, and go to the mountains, and seek that which is gone astray?
13 Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
And if he findeth it, verily I say to you, he rejoiceth more over that [sheep], than over the ninety and nine which went not astray.
14 Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
Even so it is not the will of your Father who is in heaven, that one of these little ones should perish.
15 “Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
Moreover, if thy brother shall trespass against thee, go and tell him his fault between thee and him alone: if he shall hear thee, thou hast gained thy brother.
16 Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
But if he will not hear [thee], [then] take with thee one or two more, that in the mouth of two or three witnesses every word may be established.
17 Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
And if he shall neglect to hear them, tell [it] to the church: but if he shall neglect to hear the church, let him be to thee as a heathen and a publican.
18 “Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
Verily I say to you, Whatever ye shall bind on earth, shall be bound in heaven: and whatever ye shall loose on earth, shall be loosed in heaven.
19 “Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
Again I say to you, That if two of you shall agree on earth, concerning any thing that they shall ask, it shall be done for them by my Father who is in heaven.
20 Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
For where two or three are assembled in my name, there am I in the midst of them.
21 Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
Then came Peter to him, and said, Lord, how often shall my brother sin against me, and I forgive him? till seven times?
22 Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
Jesus saith to him, I say not to thee, Until seven times: but, Until seventy times seven.
23 “Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
Therefore is the kingdom of heaven likened to a certain king who would take account of his servants.
24 Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
And when he had begun to reckon, one was brought to him who owed him ten thousand talents.
25 Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
But as he had not ability to pay, his lord commanded him to be sold, and his wife and children, and all that he had, and payment to be made.
26 “Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
The servant therefore fell down, and worshiped him, saying, Lord, have patience with me, and I will pay thee all.
27 Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
Then the lord of that servant was moved with compassion, and loosed him, and forgave him the debt.
28 “Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
But the same servant went out, and found one of his fellow-servants, who owed him a hundred pence: and he laid hands on him, and took [him] by the throat, saying, Pay me what thou owest.
29 “Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
And his fellow-servant fell down at his feet, and besought him, saying, Have patience with me, and I will pay thee all.
30 “Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
And he would not: but went and cast him into prison, till he should pay the debt.
31 Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
So when his fellow-servants saw what was done, they were very sorry, and came and told to their lord all that was done.
32 “Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
Then his lord, having called him, said to him, O thou wicked servant, I forgave thee all that debt, because thou desiredst me:
33 Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
Shouldst thou not also have had compassion on thy fellow-servant, even as I had pity on thee?
34 Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
And his lord was wroth, and delivered him to the tormentors, till he should pay all that was due to him.
35 “Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”
So likewise shall my heavenly Father do to you, if ye from your hearts forgive not every one his brother their trespasses.

< Mathayo 18 >