< Mathayo 18 >

1 Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu na kumuuliza, “Je, nani aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?”
In that hour came, the disciples unto Jesus, saying—Who then is, greatest, in the kingdom of the heavens?
2 Yesu akamwita mtoto mdogo na kumsimamisha katikati yao.
And, calling near a child, he set it in the midst of them,
3 Naye akasema: “Amin, nawaambia, msipookoka na kuwa kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.
and said—Verily, I say unto you, Except ye turn and become as the children, in nowise, shall ye enter into the kingdom of the heavens.
4 Kwa hiyo mtu yeyote anyenyekeaye kama huyu mtoto, ndiye aliye mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni.
Whosoever therefore shall humble himself as this child, the same, is the greatest, in the kingdom of the heavens;
5 “Yeyote amkaribishaye mtoto mdogo kama huyu kwa Jina langu, anikaribisha mimi.
And, whosoever shall give welcome unto one such child as this, upon my name, unto me, giveth welcome.
6 Lakini kama mtu yeyote akimsababisha mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini kutenda dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake, na kutoswa katika kilindi cha bahari.
And, whosoever shall cause to stumble one of these little ones who believe in me, it profiteth him, that there be hung a large mill-stone about his neck, and he be sunk in the wide main of the sea.
7 “Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya yale mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mtu yule ambaye huyasababisha.
Alas for the world! by reason of the causes of stumbling; for it is, necessary, that the causes of stumbling come, —nevertheless, alas for the man through whom the cause of stumbling cometh!
8 Ikiwa mkono wako au mguu wako unakusababisha utende dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili, na kutupwa katika moto wa milele. (aiōnios g166)
But, if, thy hand or thy foot, be causing thee to stumble, cut it off, and cast it from thee: It is, seemly for thee, to enter into life, maimed or lame, rather than, having two hands or two feet, to be cast into the age-abiding fire. (aiōnios g166)
9 Nalo jicho lako likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe, ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
And, if, thine eye, causeth thee to stumble, pluck it out, and cast it from thee: It is, seemly, for thee, one-eyed, into life, to enter, rather than, having two eyes, to be cast into the fiery gehenna. (Geenna g1067)
10 “Angalia ili usimdharau mmojawapo wa hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni. [
Beware! do not despise one of these little ones; For I say unto you—that, their messengers in the heavens, do, continually, behold the face of my Father in the heavens.
11 Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.]
12 “Mwaonaje? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je, hatawaacha wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta huyo mmoja aliyepotea?
How, to you, doth it seem? If a certain man come to have a hundred sheep and one from among them go astray, Will he not leave the ninety-nine upon the mountains, and going, seek the straying one?
13 Naye akishampata, amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa ambao hawakupotea.
And, if it should be that he find it, Verily, I say unto you—He rejoiceth over it, more than over the ninety-nine that have not gone astray.
14 Vivyo hivyo, Baba yenu wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa hawa wadogo apotee.
Thus, there is no desire, in the presence of my Father who is in the heavens, that, one of these little ones, should be lost.
15 “Kama ndugu yako akikukosea, nenda ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa umempata tena ndugu yako.
But, if thy brother sin, withdraw, convince him, betwixt thee and him, alone, —If unto thee he hearken, thou hast gained thy brother;
16 Lakini kama hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja au wawili ili kila neno lithibitishwe kwa ushahidi wa mashahidi wawili au watatu.
But, if he do not hearken, take with thee, yet one or two, that, at the mouth of two witnesses or three, every declaration, maybe established;
17 Kama akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa. Naye kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi awe kwenu kama mtu asiyeamini au mtoza ushuru.
But, if he hear them amiss, tell it to the assembly, —And, if, even the assembly, he hear amiss, Let him be unto thee, just as the man of the nations and the tax-collector.
18 “Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
Verily, I say unto you—Whatsoever things ye shall bind on the earth, shall be bound in heaven; and, whatsoever things ye shall loose on the earth, shall be loosed in heaven.
19 “Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu watakubaliana duniani kuhusu jambo lolote watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.
Again, [verily] I say unto you—If two from among you shall agree upon the earth concerning any matter, whatsoever they shall ask, it shall be brought to pass for them, from my Father who is in the heavens;
20 Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa Jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.”
For, where there are two or three, gathered together into my name, there, am I, in their midst.
21 Ndipo Petro akamjia Yesu na kumuuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
Then, coming near, Peter said [to him]—Lord! how many times, shall my brother sin against me, and I forgive him? Until, seven, times?
22 Yesu akamjibu, “Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
Jesus saith to him—I say not unto thee, unto, seven, times, but, until seventy times seven.
23 “Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya hesabu zake za fedha na watumishi wake.
For this cause, hath the kingdom of the heavens become like unto a man, a king, who wished to settle an account with his servants;
24 Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja aliyekuwa anadaiwa talanta10,000, aliletwa kwake.
And, when he, began, to settle, there was brought unto him a, certain, debtor, of a thousand talents;
25 Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa navyo, ili lile deni lipate kulipwa.
and, he, not having, wherewith to pay, the master ordered him to be sold, and the wife, and the children, and whatsoever he had, —and payment to be made.
26 “Yule mtumishi akampigia magoti, akamsihi yule bwana akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
The servant therefore, falling down, began to do homage unto him, saying—Have patience with me, and, all, will I pay thee.
27 Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha aende zake.
And, moved with compassion, the master of that servant released him, and, the loan, he, forgave, him.
28 “Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka nje, akakutana na mtumishi mwenzake aliyekuwa amemkopesha dinarimia moja. Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai!’
But that servant, going out, found one of his fellow-servants, who owed him, a hundred denaries, and, laying hold of him, he began seizing him by the throat, saying, Pay! if anything thou owest.
29 “Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’
His fellow servant, therefore, falling down, began beseeching him, saying, Have patience with me! And I will pay thee.
30 “Lakini akakataa. Badala yake, alienda akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni.
He, however, would not, but went away and cast him into prison, —until he should pay what was owing.
31 Watumishi wenzake walipoona haya yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa kimetukia.
His fellow-servants, therefore, seeing, the things that were done, were grieved exceedingly, —and went and made quite plain to their master all the things which had been done.
32 “Yule bwana akamwita yule mtumishi akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi nilikusamehe deni lako lote uliponisihi.
Then, calling him near, his master saith unto him—O wicked servant! All that debt, forgave I thee, because thou didst beseech me.
33 Je, haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’
Was it not binding, upon thee also, to have mercy upon thy fellow-servant, as, I also, on thee, had mercy?
34 Kwa hasira, yule bwana wake akamtia yule mtumishi mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
And, provoked to anger, his master delivered him up to the torturers, until he should pay all that was owing.
35 “Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwake.”
Thus, my heavenly Father also, will do unto you, if ye forgive not each one his brother, from your hearts.

< Mathayo 18 >