< Mathayo 17 >
1 Siku sita baada ya jambo hili, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake Yakobo, akawapeleka juu ya mlima mrefu peke yao.
天以後,耶穌帶著伯多祿,雅各伯和他的兄弟若望,單獨帶領他們上了一座高山,
2 Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura mbele yao. Uso wake ukangʼaa kama jua na nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza macho.
在他們面前變了容貌發光有如太陽,他的衣服潔白如光。
3 Ghafula wakawatokea mbele yao Mose na Eliya, wakizungumza na Yesu.
忽然,梅瑟和厄里亞也顯現給他們,正在同耶穌談論。
4 Ndipo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vyema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
伯多祿就開口對耶穌說:「主啊! 我們在這裏真好!你若願意,我就在這裏搭三個帳棚:一個為你,一個為梅瑟,一個為厄里亞。」
5 Petro alipokuwa angali ananena, ghafula wingu lililongʼaa likawafunika, na sauti ikatoka kwenye hilo wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana. Msikieni yeye.”
他還在說話的時候,忽然有一片光耀的雲彩遮敝了他們,並且雲中有聲因說:「這是我的愛子,我所喜悅的,你們要聽從他!」
6 Wanafunzi waliposikia haya, wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu.
門徒聽了就俯服在地,非常害怕。
7 Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia, “Inukeni na wala msiogope.”
耶穌遂前來,撫摩他們說:「起來不要害怕!」
8 Walipoinua macho yao, hawakumwona mtu mwingine yeyote isipokuwa Yesu.
他們舉目一看,任誰都不見了,只有耶穌獨自一人。
9 Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawaagiza, “Msimwambie mtu yeyote mambo mliyoyaona hapa, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuliwa kutoka kwa wafu.”
他們從山上下來的時候,耶穌囑咐他們說:「非等人子由死者中復活,你們不要將所見告的告訴任何人」
10 Wale wanafunzi wakamuuliza, “Kwa nini basi walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
門徒便問耶穌說:「那麼,為什麼經師說:厄里亞應該先來呢?」
11 Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya lazima aje kwanza, naye atatengeneza mambo yote.
耶穌回答說:「厄里亞的確要來,且要重整一切;
12 Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao hawakumtambua, bali walimtendea kila kitu walichotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu pia atateswa mikononi mwao.”
但我告訴你們:厄里亞已經來了,人們卻不認識他,反兒任意待了他;照樣,人子也要受他們的磨難。」
13 Ndipo wale wanafunzi wakaelewa kuwa alikuwa anazungumza nao habari za Yohana Mbatizaji.
門徒這纔明白耶穌給他們所說的,是指的洗者若翰。
14 Walipofika penye umati wa watu, mtu mmoja akamjia Yesu na kupiga magoti mbele yake, akasema,
當他們來到群眾那裏時,有一個人來到耶穌跟前,跪下說:
15 “Bwana, mhurumie mwanangu. Yeye ana kifafa na anateseka sana. Mara kwa mara huanguka kwenye moto au kwenye maji.
「主啊,可憐我的兒子罷!他患癲癇病很苦,屢次跌在火中,又屢次跌在水裏。
16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”
我把他帶到你的們徒跟前,他們卻不能治好他。」
17 Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana hapa kwangu.”
耶穌回答說:「哎!無信敗壞的世代,我同你們在一起要到幾時呢? 我容忍你們要到幾時呢?把他給我帶到這裏來!」
18 Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akamtoka yule kijana, naye akapona saa ile ile.
耶穌遂叱責魔鬼,魔鬼就從還子身上出去了;從那時刻,孩子就好了。
19 Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu wakiwa peke yao, wakamuuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
以後,門徒前來私下對耶穌說:「為什麼我們不能逐出這魔鬼呢?」
20 Akawajibu, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Ninawaambia kweli, mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka. Wala hakutakuwa na jambo lisilowezekana kwenu. [
耶穌對他們說:「由於你們缺少信德;我實在告訴你們:假如你們有像芥子那麼大的信德,你們向這座山說:從這邊移到那邊去!它必會移過去的;為你們沒有不可能的事。
21 Lakini hali kama hii haitoki ila kwa kuomba na kufunga.]”
『但這類魔鬼非用祈禱和禁食,是不能趕出去的。』
22 Siku moja walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.
當耶穌同門徒在加里肋亞周遊時,耶穌對他們說:「人子將被交於人們手中。
23 Nao watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa.” Wanafunzi wakahuzunika sana.
他們要殺害他,第三天他必要復活。門徒就非常憂鬱。
24 Baada ya Yesu na wanafunzi wake kufika Kapernaumu, wakusanya kodi ya Hekalu wakamjia Petro na kumuuliza, “Je, Mwalimu wenu halipi kodi ya Hekalu?”
他們來到葛法翁時,收殿稅的人來到伯多祿跟前說:「你們的師傅不納殿稅嗎?」
25 Petro akajibu, “Ndiyo, yeye hulipa.” Petro aliporudi nyumbani, Yesu akawa wa kwanza kulizungumzia, akamuuliza, “Unaonaje Simoni? Wafalme wa dunia hupokea ushuru na kodi kutoka kwa nani? Je, ni kutoka kwa watoto wao au kutoka kwa watu wengine?”
伯多碌說:「自然納的。」他一進到屋裏,耶穌就先對他說:「西滿!你以為怎樣?地上的君王向誰征收關稅或丁稅呢?向自己的兒子,或是向外人?
26 Petro akamjibu, “Kutoka kwa watu wengine.” Yesu akamwambia, “Kwa hiyo watoto wao wamesamehewa.
伯多碌說:「向外人。」耶穌對他說:「所以兒子是免稅的了。
27 Lakini ili tusije tukawaudhi, nenda baharini ukatupe ndoana. Mchukue samaki wa kwanza utakayemvua. Fungua kinywa chake nawe utakuta humo fedha, ichukue ukalipe kodi yako na yangu.”
但是,為避免使他們疑怪,你往海邊去垂釣,拿釣上來的第一條魚,開了它的口,就會找到一塊「斯塔特。」拿去交給他們,當作我和你的殿稅。」