< Mathayo 17 >
1 Siku sita baada ya jambo hili, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana ndugu yake Yakobo, akawapeleka juu ya mlima mrefu peke yao.
Amhnüp khyuk käna Jesuh naw Pita, Jakuk ja a na Johan mcunga hlüngnaka a jah cehpüi.
2 Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura mbele yao. Uso wake ukangʼaa kama jua na nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza macho.
Acunüng Jesuh a hmai khawnghngia mäiha vai lü, a suisak pi akvai mäiha bawk lawki.
3 Ghafula wakawatokea mbele yao Mose na Eliya, wakizungumza na Yesu.
Acunüng axüisaw kthum naw Jesuh cun Mosi ja Elijah naw ngthuheipüi ni se ami jah hmuh.
4 Ndipo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vyema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.”
Acunüng Pita naw Jesuh üng, “Bawipa aw, ahia mi ve vai hin daw ve. Na hlüei üng ta, nanga phäh mat, Mosia phäh mat, Elijaha phäh mat, sam kthum ka pha vai sü,” ti lü a mtheh.
5 Petro alipokuwa angali ananena, ghafula wingu lililongʼaa likawafunika, na sauti ikatoka kwenye hilo wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa naye sana. Msikieni yeye.”
Acukba a pyen k'um üng, khawngmei bawk naw jah msung law lü, “Hin hin ka mhläkphyanak pipia ka Capa ni, ani üng ka jeki, a pyen ngai ua” tia, kthai cun ngmei üngka naw ngjakie.
6 Wanafunzi waliposikia haya, wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu.
Axüisawe naw ami ngjak üng, aktäa kyühei u lü mce da ngmümkie.
7 Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia, “Inukeni na wala msiogope.”
Jesuh naw law lü jah hnetki naw, “Tho law u, käh kyüei ua,” a ti.
8 Walipoinua macho yao, hawakumwona mtu mwingine yeyote isipokuwa Yesu.
Ami jeng mdei üng Jesuh amät däk ve se ami hmuh.
9 Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani, Yesu akawaagiza, “Msimwambie mtu yeyote mambo mliyoyaona hapa, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuliwa kutoka kwa wafu.”
Mcung üngka naw ami kyum law be üng, Jesuh naw axüisaw he üng, “Khyanga Capa thihnak üngka naw am a thawh be hama küt üng nami hmuha mdannak hin u üng pi käh nami mtheh vai,” ti lü, a jah cük.
10 Wale wanafunzi wakamuuliza, “Kwa nini basi walimu wa sheria husema kwamba ni lazima Eliya aje kwanza?”
Axüisawe naw Jesuh üng, “Acunüng ise thumksinge naw Elijah law ma khai ami ti ni? ti u se,
11 Yesu akawajibu, “Ni kweli, Eliya lazima aje kwanza, naye atatengeneza mambo yote.
Jesuh naw, “Akcanga Elijah cun law ma lü ahmäi jah pyang law khai,” a ti.
12 Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao hawakumtambua, bali walimtendea kila kitu walichotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu pia atateswa mikononi mwao.”
Acunüngpi ka ning jah mthehki, Elijah cun law pängki ni. Cunsepi am ksingki he naw ami ngaih ngaiha ami mkhuimkha, acukba bäa Khyanga Capa pi mkhuimkha khaie” a ti.
13 Ndipo wale wanafunzi wakaelewa kuwa alikuwa anazungumza nao habari za Yohana Mbatizaji.
Acunüng, axüisaw he naw Baptican Johana mawng jah mthehkia ami ksing.
14 Walipofika penye umati wa watu, mtu mmoja akamjia Yesu na kupiga magoti mbele yake, akasema,
Khyang hea veia ami nghlat law be üng, khyang mat Jesuha veia law lü ngdängki naw,
15 “Bwana, mhurumie mwanangu. Yeye ana kifafa na anateseka sana. Mara kwa mara huanguka kwenye moto au kwenye maji.
“Bawipa aw, ka capa mpyeneia! Kphyaw se aläa tui üng ngcum lü am ani üng mei üng lut lü khuikha ve.”
16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”
“Acunakyase, na xüisawea veia ka lawpüi kyaw amimi naw pi am mdaw be khawh ve u,” a ti.
17 Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi mpaka lini? Nitawavumilia mpaka lini? Mleteni mvulana hapa kwangu.”
Jesuh naw, “Jumeinak am takia khyang ksee aw, ivei nami veia ka ve khai ni? Ivei ka ning jah msawkei vai ni? Kpamica ka veia lawpüi ua,” a ti.
18 Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akamtoka yule kijana, naye akapona saa ile ile.
Jesuh naw khawyai jüi se kpamica üngka naw lut law beki. Acunja kpamica cun daw beki.
19 Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu wakiwa peke yao, wakamuuliza, “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
Acunüng axüisaw he Jesuha veia ampyua law u lü, “Ise keimi naw am kami ksät khawh ni,” ti lü ami kthäh.
20 Akawajibu, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Ninawaambia kweli, mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mtauambia mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale,’ nao utaondoka. Wala hakutakuwa na jambo lisilowezekana kwenu. [
Jesuh naw, “Nami jumeinak a ngceka phäh ni, akcanga ka ning jah mthehki, anca ui teh jumnak nami tak üng, hina mcung üng ‘Caia ngpyawta’ nami ti üng ngpyawt khai. Ai pi, am nami pawh khawh käh ve khai,” ti lü, a jah mtheh.
21 Lakini hali kama hii haitoki ila kwa kuomba na kufunga.]”
Ahina ngkhaw cun ei jeihnak ja ktaiyünak am ni mkhüt khawh” a ti.
22 Siku moja walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.
Kalilea ami ve üng Jesuh naw, “Khyanga Capa, khyang hea kut üng petnak vaia kcün pha lawki ni,”
23 Nao watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa.” Wanafunzi wakahuzunika sana.
hnim u se, amhnüp kthum üng tho law be khai,” ti lü jah mtheh se, axüisaw he aktäa vedamkie.
24 Baada ya Yesu na wanafunzi wake kufika Kapernaumu, wakusanya kodi ya Hekalu wakamjia Petro na kumuuliza, “Je, Mwalimu wenu halipi kodi ya Hekalu?”
Kapenawm mlüh Jesuh ja axüisaw he ami law üng, temple khawn kawkie cun Pita veia law u lü, “Nami saja naw temple khawn am pe hlüki mä? ti lü ami kthäh.
25 Petro akajibu, “Ndiyo, yeye hulipa.” Petro aliporudi nyumbani, Yesu akawa wa kwanza kulizungumzia, akamuuliza, “Unaonaje Simoni? Wafalme wa dunia hupokea ushuru na kodi kutoka kwa nani? Je, ni kutoka kwa watoto wao au kutoka kwa watu wengine?”
Pita naw, “Ä, peki ni,” a ti. Pita im k'uma a luh üng, ‘Jesuh naw, “Sihmon Pita, ihawkba na ngaiki ni” Khawmdek Sangpuxange naw akhawn ami mkhäm üng, ua veia ni ami tä khawi? Khaw mahea veia mä, pekce khyang hea veia mä ami tä khawi? a ti,
26 Petro akamjibu, “Kutoka kwa watu wengine.” Yesu akamwambia, “Kwa hiyo watoto wao wamesamehewa.
Pita naw, “Pekce khyang hea veia,” a ti. Jesuh naw Pita üng, “Acukba ani üng, khaw mahe naw akhawn pet vai am hlü.”
27 Lakini ili tusije tukawaudhi, nenda baharini ukatupe ndoana. Mchukue samaki wa kwanza utakayemvua. Fungua kinywa chake nawe utakuta humo fedha, ichukue ukalipe kodi yako na yangu.”
Acunüngpi, akhawn am mi peta phäh ami mlung käh se khaia, tuia va cit lü nga va mkaiha. Akcüka na phaa nga lo lü a mka na phyen vai. Acunüng tangka mat na hmuh khai. Acun lo lü ka phäh ja na phäha temple khawn va pea,” a ti.