< Mathayo 16 >
1 Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
And the Pharisees and Sadducees came to try him, and asked him to show them a sign from heaven.
2 Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
And he answering said to them, When it is evening, ye say, Fair weather! for the sky is red.
3 Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
And in the morning, A storm today! for the sky is red and lowering. Ye know how to judge of the face of the sky, and can ye not discern the signs of the times?
4 Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
A wicked and adulterous generation seeketh after a sign; and no sign will be given to it, but the sign of Jonah. And he left them and went away.
5 Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
And the disciples having come to the other side, had forgotten to take bread.
6 Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
And Jesus said to them, Take heed, and beware of the leaven of the Pharisees and Sadducees.
7 Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
And they reasoned among themselves, saying, It is because we took no bread.
8 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
And Jesus knowing it, said, Why are ye reasoning among yourselves, ye of little faith, because ye took no bread?
9 Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
Do ye not yet understand, nor remember the five loaves of the five thousand, and how many baskets ye took up?
10 Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
Nor the seven loaves of the four thousand, and how many baskets ye took up?
11 Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
How is it that ye do not understand, that I spoke not to you of loaves? But [[I said]] Beware of the leaven of the Pharisees and Sadducees.
12 Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
Then they understood, that he did not bid them beware of the leaven of the Pharisees and Sadducees, but of the teaching of the Pharisees and Sadducees.
13 Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
And Jesus, having come into the region of Caesarea Philippi, asked his disciples, saying, Who do men say that the Son of man is?
14 Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
And they said, Some, John the Baptist; but some, Elijah; and others, Jeremiah, or one of the prophets.
15 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
He saith to them, But who do ye say that I am?
16 Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
And Simon Peter answering said, Thou art the Christ, the Son of the living God.
17 Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
And Jesus answering said to him, Blessed art thou, Simon, son of Jonah; for flesh and blood did not reveal it to thee, but my Father who is in heaven.
18 Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs )
And I on my part say to thee, that thou art Peter, a rock, and on this rock will I build my church, and the gates of the underworld shall not prevail against it. (Hadēs )
19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
I will give thee the keys of the kingdom of heaven; and whatever thou shalt bind on earth will be bound in heaven; and whatever thou shalt loose on earth will be loosed in heaven.
20 Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
Then he charged the disciples to tell no one that he was the Christ.
21 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
From that time Jesus began to show to his disciples, that he must go to Jerusalem, and suffer many things from the elders and chief priests and scribes, and be put to death, and rise again on the third day.
22 Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
Then Peter, taking him aside, began to rebuke him, saying, Be it far from thee, Lord! This shall not be to thee.
23 Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
But he turned and said to Peter, Get thee behind me, Satan! thou art my stumbling-block; for thy thoughts are not on the things of God, but on those of men.
24 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
Then Jesus said to his disciples, If any one chooseth to come after me, let him deny himself, and take up his cross, and follow me.
25 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
For whoever chooseth to save his life will lose it; and whoever shall lose his life for my sake will find it.
26 Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
For what will a man be profited, if be gain the whole world, and forfeit his life? or what shall a man give as an exchange for his life?
27 Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
For the Son of man is to come in the glory of his Father, with his angels; and then will he render to every one according to his works.
28 Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”
Truly do I say to you, There are some of those standing here who will not taste of death, till they have seen the Son of man coming in his kingdom.