< Mathayo 16 >

1 Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
法利赛人和撒都该人前来试探耶稣,要求他显化上天的上帝神迹。
2 Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’
耶稣回答:“黄昏时你们会说:‘天色通红,明天一定是晴天。’
3 Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati.
清晨时你们会说:‘天色阴沉暗红,今天一定有风雨。’你们知道如何分辨天色预测天气,却不能分辨时代的征兆吗!
4 Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake.
不信上帝的邪恶之人如寻奇迹之兆,除了约拿的上帝神迹之外,不会有任何上帝神迹显化。”说罢,耶稣就离开了。
5 Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
门徒到了对岸时,才发现忘记了带饼。
6 Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
耶稣对他们说:“你们要小心,提防法利赛人和撒都该人的酵母。”
7 Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”
门徒们彼此争论:“他这样说是因为我们没有带饼吧。”
8 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate?
耶稣知道他们在说什么:“你们对我的信任太少了,为什么你们要议论没有饼这件事呢?
9 Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
你们难道还不明白吗?还记得用五块饼分给五千人,又装满了多少个篮子呢?
10 Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya?
还记得用七块饼分给四千人,又装满了多少篮子?
11 Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”
我说的并非关于饼,你们不明白吗?你们要提防法利赛人和撒都该人的酵母。”
12 Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
这时门徒才领会,耶稣不是叫他们防备做饼用的酵母,而是提防法利赛人和撒都该人的教义。
13 Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?”
耶稣来到该撒利亚,这里属于腓立比的地区。他问自己的门徒:“民众认为人子是谁?”
14 Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.”
他们回答:“有人说是施洗约翰,有人说是以利亚,也有人说是耶利米,或是某位先知。”
15 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?”
耶稣继续问门徒:“你们认为我是谁?”
16 Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.”
西门(彼得)回答:“你是弥赛亚,是永生上帝之子。”
17 Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni.
耶稣对他说:“约拿的儿子西门,你是真正有福之人,因为这启示并非源自凡人肉体,而是我的天父从天上赐予你。
18 Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. (Hadēs g86)
我还要告诉你:你是彼得,我要在这块岩石上创建我的教会,即使死亡的力量也不能胜过它。 (Hadēs g86)
19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.”
我要把天国的钥匙交给你,你在人间所禁止之事,也会在天国禁止,你在人间允许之事,也会在天国允许。”
20 Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo.
于是耶稣吩咐门徒,不可对人说他就是基督。
21 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa.
此后,耶稣开始向门徒解释:他必须去耶路撒冷,然后会受到长老、祭司长和宗教老师的折磨迫害,被杀,在死后第三天复活。
22 Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!”
彼得于是把耶稣拉到一边,责怪他说:“上帝不容,主啊,千万不可如此,这事怎能发生在你身上。”
23 Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
耶稣转身对彼得说:“走开吧,撒旦!你是绊倒我的陷阱,因为你所思并非上帝之意,不过人类思想而已。”
24 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
随后耶稣对门徒说:“如果有人愿意跟从我,就当舍弃自己,背起你的十字架追随我。
25 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata.
若你想拯救自己生命,必丧掉生命,但为我牺牲生命,必得生命。
26 Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
纵使抓住全世界,却赔上自己的生命,有何益处?人能用什么换回自己的生命呢?
27 Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
人子将在天父的荣耀中与众天使共同降临,届时他给每个人的,都是每个人行动应得的。
28 Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”
和你们说实话,站在这里的人,有的人必会在有生之年看见人子携其国度降临人间。”

< Mathayo 16 >