< Mathayo 15 >
1 Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
Then, there come unto Jesus from Jerusalem Pharisees and Scribes, saying—
2 “Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
Wherefore do thy disciples transgress the tradition of the elders? for they wash not their hands, when they eat bread!
3 Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
But, he, answering, said unto them—Wherefore do, ye also, transgress the commandment of God for the sake of your tradition?
4 Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
For, God, said—Honour thy father and thy mother, and—He that revileth father or mother, let him, surely die!
5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
But, ye, say—Whosoever shall say to his father or his mother—A gift! Whatsoever, out of me, thou mightest be profited,
6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
in nowise, shall honour his father or his mother—and so ye have cancelled, the word of God, for the sake of your, tradition.
7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
Hypocrites! well prophesied concerning you, Isaiah, saying—
8 “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
This people, with the lips, do, honour, me, while, their heart, far off, holdeth from me;
9 Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
But, in vain, do they pay devotions unto me, teaching, for teachings, the commandments of men.
10 Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
And, calling near the multitude, he said to them—Hear and understand!
11 kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
Not that which entereth into the mouth, defileth the man, but, that which proceedeth out of the mouth, the same, defileth the man,
12 Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
Then, coming near, his disciples say unto him—Knowest thou, that the Pharisees, hearing the word, were caused to stumble?
13 Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
And, he, answering, said—Every plant which my heavenly Father hath not planted, will be uprooted:
14 Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
Let them alone! they are, blind leaders; and, if the, blind, lead the, blind, both, into a ditch, will fall.
15 Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
And Peter, answering, said unto him, Declare to us the parable.
16 Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
And, he, said, To this moment, are, ye also, without discernment?
17 Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
Perceive ye not that, every thing which entereth into the mouth, into the stomach, findeth way, and, into the draught, is passed;
18 Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
while, the things which proceed out of the mouth, out of the heart, come forth, and, they, defile the man.
19 Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
For, out of the heart, come forth wicked designs, —murders, adulteries, fornications, thefts, false testimonies, profane speakings:
20 Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
these, are the things which defile the man, but, the eating with unwashed hands, doth not defile the man.
21 Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
And, going forth from thence, Jesus retired into the parts of Tyre and Zidon.
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
And lo! a Canaanite woman, from those bounds, coming forth, began crying out, saying, Have mercy on me, Lord, Son of David! My daughter, is miserably demonized.
23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
But, he, answered her no a word. And his disciples, coming forward began requesting him, saying—Dismiss her, because she is crying out after us.
24 Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
But, he, answering, said, I was not sent forth, save unto the lost sheep of the house of Israel.
25 Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
And, she, coming, began bowing down to him, saying, Lord! help me.
26 Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
But, he, answering, said, It is, not seemly, to take the loaf of, the children, and cast, to the little dogs.
27 Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
And, she, said, True, Lord! [for], even the little dogs, eat of the crumbs which are falling from the table of, their masters.
28 Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
Then, answering, Jesus said to her—O woman! great, is, thy faith! Be it, done, for thee, as thou desirest. And her daughter was healed, from that hour.
29 Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
And, passing on from thence, Jesus came near the sea of Galilee, and, going up into the mountain, was sitting there.
30 Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
And there came unto him large multitudes, having with themselves the lame, the maimed, the blind, the dumb, and many others, —and they cast them near his feet, and he cured them;
31 Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
so that the multitude marvelled, seeing the dumb speaking, the lame walking, and the blind seeing, —and they glorified the God of Israel.
32 Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
But, Jesus, calling near his disciples, said—My compassions are moved towards the multitude, because [even now], three days, abide they with me, and they have nothing to eat, —and, to dismiss them fasting, I am not willing, lest by any means they faint in the way.
33 Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
And his disciples say unto him—Whence, to us, in a wilderness, loaves in such numbers as to fill a multitude, so great?
34 Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
And Jesus saith unto them—How many, loaves have ye? And, they, said, —Seven, and a few small fishes.
35 Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
And, sending word to the multitude to recline upon the ground,
36 Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
he took the seven loaves, and the fishes, and, giving thanks, brake, —and began giving to his disciples, and, the disciples, to the multitudes.
37 Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
And they all did eat and were filled, —and, the remainder of the broken pieces, took they up, seven hampers, full.
38 Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
And, they who did eat, were four thousand men, besides women and children.
39 Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.
And, dismissing the multitudes, he went up into the boat, —and came into the bounds of Magadan.