< Mathayo 15 >

1 Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
Then some Scribes and Pharisees of Jerusalem addressed him, saying,
2 “Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
Why do your disciples transgress the tradition of the elders; for they was not their hands before meals.
3 Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
Jesus answering, saud to them, Why do you yourselves by your tradition, transgress the commandment of God?
4 Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
For God has commanded, saying, "Honor father and mother"; and "Whosoever reviles father or mother, let him be punished with death."
5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
But you affirm, If a man say to father or mother, I devote whatever of mine shall profit you,
6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
he shall not afterward honor by his assistance, his father or his mother. Thus, by your tradition, you annul the commandment of God.
7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
Hypocrites, well do you suit the character which Isaiah gave of you, saying,
8 “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
"This people honor me with their lips. though their heart is estranged from me.
9 Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
But in vain they worship me, while they teach institutions merely human."
10 Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
Then, having called the multitude, he said to them, Hear, and be instructed.
11 kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
It is not what goes into the mouth pollutes the man; but it is what proceeds out of the mouth, that pollutes the man.
12 Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
On which his disciples accosting him, said, Did you observe how the Pharisees, when they heard that saying were offended?
13 Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
He answered, Every plant, which my heavenly Father has not planted, shall be extirpated.
14 Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
Let them alone. They are blind leaders of the blind; and if the blind lead the blind, both will fall into the ditch.
15 Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
Then Peter addressing him, said, Explain to us that parable.
16 Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
Jesus answered, Are you also void of understanding?
17 Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
Do you not apprehend, that whatever enters the mouth passes into the stomach, and is thrown out into the sink.
18 Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
But that which proceeds out of the mouth, issues from the heart, and so pollutes the man.
19 Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
For out of the heart proceed malicious contrivances, murders, adulteries, fornications, thefts, false testimonies, calumnies.
20 Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
These are the things which pollute the man; but to eat with unwashed hands pollutes not the man.
21 Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
Then Jesus withdrew into the confines of Tyre and Sidon;
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
and behold! a Canaanitish woman of these territories came to him, crying, Master, Son of David, have pity on me; my daughter is grievously afflicted by a demon.
23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
But he gave her no answer. Then his disciples interposed, and entreated him, saying, Dismiss her, for she clamors after us.
24 Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
He answering said, My mission is only to the lost sheep of the stock of Israel.
25 Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
She, nevertheless, advanced, and prostrating herself before him, said, O Lord, help me.
26 Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
He replied, It is not seemly to take the children's bread, and throw it to the dogs.
27 Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
True, Sir, returned she. Yet even the dogs are allowed the crumbs which fall from their master's table.
28 Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
Then Jesus, answering, said to her, O woman! great is your faith. Be it to you as you desire. And that instant her daughter was healed.
29 Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
Jesus having left that place, came nigh to the sea of Galilee, and repaired to a mountain, where he sat down;
30 Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
and great multitudes flocked to him, bringing with them the lame, the blind, the dumb, the cripple, and several others, whom they laid at his feet; and he healed them:
31 Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
insomuch that the people beheld, with admiration, the dumb speaking, the cripple sound, the lame walking, and the blind seeing; and they glorified the God of Israel.
32 Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
Then Jesus called to him his disciples, and said, I have compassion on the multitude because they have now attended me three days, and have nothing to eat; I will not dismiss them fasting, lest they faint by the way.
33 Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
His disciples answered, Whence can we get bread enough, in the solitude, to satisfy such a crowd?
34 Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
He asked them, How many loaves have you? They said, Seven, and a few small fishes.
35 Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
Then commanding the people to recline upon the ground,
36 Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
he took the seven loaves and the fishes, which, having given thanks, he divided and gave to his disciples, who distributed them among the people.
37 Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
When all had eat, and were satisfied, they carried off seven hand-baskets full of the fragments that remained.
38 Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
Now they that had eat were four thousand men, besides women and children.
39 Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.
Then having dismissed the multitude, he embarked, and sailed to the coast of Magdala.

< Mathayo 15 >