< Mathayo 15 >
1 Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
THEN came to Jesus scribes and Pharisees from Jerusalem, saying,
2 “Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
Why do thy disciples transgress the tradition of the elders? for they wash not their hands when they eat bread?
3 Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
And he answering said to them, And why do you transgress the command of God, by your tradition?
4 Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
For God commanded, saying “Honour thy father and thy mother:” and, He that curseth father or mother, let him surely die.
5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
But ye say, If any man declare to his father or mother, This is a devoted gift, which else might have been employed by me for thy advantage;
6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
then he shall not with it honour his father and mother: so have ye vacated the command of God by your tradition.
7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
Ye hypocrites, well hath Isaiah prophesied concerning you, saying,
8 “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
This people draweth nigh to me with their mouths, and honoureth me with the lips, but their heart is far distant from me.
9 Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
But in vain do they worship me, teaching doctrines the commandments of men.
10 Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
And he called to him the multitude, and said unto them, Hear, and understand:
11 kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
not that which goeth into the mouth defileth a man; but what cometh out of the mouth, that defileth the man.
12 Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
Then his disciples approaching, said to him, Knowest thou how offended the Pharisees were at hearing that speech?
13 Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
Then he answered and said, Every plant which my heavenly Father hath not planted shall be rooted up.
14 Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
Leave them to themselves: they are blind leaders of the blind. But if the blind lead the blind, they will both fall into the pit.
15 Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
Then Peter answering said unto him, Explain to us this parable.
16 Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
And Jesus said, Are ye also to this time destitute of intelligence?
17 Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
Do ye not observe, that every thing which entereth into the mouth passeth into the belly, and is ejected into the vault?
18 Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
But the things which go forth out of the mouth, come out of the heart, and they are the things which defile a man:
19 Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
for out of the heart proceed wicked reasonings, murders, adulteries, whoredoms, thefts, false testimonies, blasphemies:
20 Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
these are the things which defile a man: but to eat with unwashed hands doth not defile a man.
21 Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
And going forth thence, Jesus retired into the coasts of Tyre and Sidon.
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
And lo! a woman of Canaan coming out of these coasts, cried aloud, saying to him, Have mercy on me, Lord, Son of David: my daughter is a grievous demoniac.
23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
But he replied not a word to her. Then his disciples came and intreated him, saying, Send her away; for she is crying aloud after us.
24 Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
But he said in reply, I am not sent, save only to the lost sheep of the house of Israel.
25 Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
Then she came, and worshiped him, saying, Lord, help me!
26 Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
But he answering said, It is not proper to take the children’s bread and throw it to the dogs.
27 Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
And she said, True, Lord: yet even the dogs eat of the crumbs which fall from their master’s table.
28 Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
Then Jesus answering said unto her, O woman, great is thy faith! be it unto thee even as thou desirest. And her daughter was cured from that hour.
29 Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
And departing thence, Jesus went to the sea-side of Galilee; and ascending a mountain, he sat down there.
30 Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
And great multitudes came to him, bringing with them the lame, blind, dumb, cripples, and many others, and cast them down at the feet of Jesus; and he cured them all:
31 Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
insomuch that the multitude marvelled when they saw the dumb speaking, the cripples sound, the lame walking, and the blind restored to sight: and they glorified the God of Israel.
32 Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
Then Jesus calling his disciples, said, I have compassion on the multitude, for they have now continued with me three days, and have not any thing to eat: and send them away fasting I will not, lest they faint on the road.
33 Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
And his disciples said unto him, Whence can we in the wilderness have loaves enough to satisfy the cravings of so great a multitude?
34 Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
And Jesus said unto them, How many loaves have ye? And they said, Seven, and a few small fishes.
35 Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
And he commanded the multitude to sit down on the ground.
36 Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
And taking the seven loaves and the fishes, he gave thanks, and brake, and gave to his disciples, and the disciples to the multitude.
37 Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
And they did all eat, and were filled: and took up a superabundance of fragments seven baskets full.
38 Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
And they that had eaten were four thousand men, besides women and children.
39 Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.
And dismissing the multitudes he went on board a vessel, and came into the coasts of Magdala.