< Mathayo 15 >

1 Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamjia Yesu kutoka Yerusalemu na kumuuliza,
Then Pharisees and scribes came to Jesus from Jerusalem, saying,
2 “Mbona wanafunzi wako wanakiuka mapokeo ya wazee? Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla ya kula!”
“Why do your disciples disobey the tradition of the elders? For they do not wash their hands when they eat bread.”
3 Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
He answered them, “Why do you also disobey the commandment of God because of your tradition?
4 Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
For God commanded, ‘Honor your father and your mother,’ and, ‘He who speaks evil of father or mother, let him be put to death.’
5 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa Mungu,’
But you say, ‘Whoever may tell his father or his mother, “Whatever help you might otherwise have gotten from me is a gift devoted to God,”
6 basi hana tena sababu ya kumheshimu baba yake nacho. Basi kwa ajili ya mafundisho yenu mnavunja amri ya Mungu.
he shall not honor his father or mother.’ You have made the commandment of God void because of your tradition.
7 Ninyi wanafiki! Isaya alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba:
You hypocrites! Well did Isaiah prophesy of you, saying,
8 “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
‘These people draw near to me with their mouth, and honor me with their lips; but their heart is far from me.
9 Huniabudu bure; nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’”
And they worship me in vain, teaching as doctrine rules made by men.’”
10 Yesu akaita ule umati wa watu, akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe:
He summoned the multitude, and said to them, “Hear, and understand.
11 kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
That which enters into the mouth does not defile the man; but that which proceeds out of the mouth, this defiles the man.”
12 Kisha wanafunzi wake wakamjia na kumuuliza, “Je, unajua kwamba Mafarisayo walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?”
Then the disciples came and said to him, “Do you know that the Pharisees were offended when they heard this saying?”
13 Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba yangu wa mbinguni hakulipanda, litangʼolewa.
But he answered, “Every plant which my heavenly Father did not plant will be uprooted.
14 Waacheni; wao ni viongozi vipofu, wanaoongoza vipofu. Kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili watatumbukia shimoni.”
Leave them alone. They are blind guides of the blind. If the blind guide the blind, both will fall into a pit.”
15 Petro akasema, “Tueleze maana ya huu mfano.”
Peter answered him, “Explain the parable to us.”
16 Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi hamfahamu?
So Jesus said, “Do you also still not understand?
17 Je, hamwelewi kwamba chochote kiingiacho kinywani huenda tumboni, na hatimaye hutolewa nje kikiwa uchafu?
Do not you understand that whatever goes into the mouth passes into the belly and then out of the body?
18 Lakini kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki ndicho kimtiacho mtu unajisi.
But the things which proceed out of the mouth come out of the heart, and they defile the man.
19 Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.
For out of the heart come evil thoughts, murders, adulteries, sexual sins, thefts, false testimony, and blasphemies.
20 Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu unajisi.”
These are the things which defile the man; but to eat with unwashed hands does not defile the man.”
21 Yesu aliondoka mahali pale, akaenda sehemu za Tiro na Sidoni.
Jesus went out from there and withdrew into the region of Tyre and Sidon.
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu jirani na hizo akaja kwake akilia, akasema, “Nihurumie, Ee Bwana, Mwana wa Daudi! Binti yangu amepagawa na pepo mchafu, na anateseka sana.”
Behold, a Canaanite woman came out from those borders and cried, saying, “Have mercy on me, Lord, you son of David! My daughter is severely possessed by a demon!”
23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele.”
But he answered her not a word. His disciples came and begged him, saying, “Send her away; for she cries after us.”
24 Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”
But he answered, “I was not sent to anyone but the lost sheep of the house of Israel.”
25 Lakini yule mwanamke akaja, akapiga magoti mbele ya Yesu, akasema, “Bwana, nisaidie!”
But she came and worshiped him, saying, “Lord, help me.”
26 Yesu akajibu, “Si haki kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
But he answered, “It is not appropriate to take the children’s bread and throw it to the dogs.”
27 Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka kutoka kwenye meza za bwana zao.”
But she said, “Yes, Lord, but even the dogs eat the crumbs which fall from their masters’ table.”
28 Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke, imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama unavyotaka.” Naye binti yake akapona tangu saa ile.
Then Jesus answered her, “Woman, great is your faith! Be it done to you even as you desire.” And her daughter was healed from that hour.
29 Yesu akaondoka na kwenda kando ya Bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani, akaketi huko.
Jesus departed from there and came near to the sea of Galilee; and he went up on the mountain and sat there.
30 Umati mkubwa wa watu ukamjia, wakiwaleta vilema, vipofu, viwete, bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; naye akawaponya.
Great multitudes came to him, having with them the lame, blind, mute, maimed, and many others, and they put them down at his feet. He healed them,
31 Hao watu wakashangaa walipoona bubu wakisema, vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli.
so that the multitude wondered when they saw the mute speaking, the injured healed, the lame walking, and the blind seeing—and they glorified the God of Israel.
32 Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake, akawaambia, “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa muda wa siku tatu, na hawana chakula chochote. Nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa, wasije wakazimia njiani.”
Jesus summoned his disciples and said, “I have compassion on the multitude, because they have continued with me now three days and have nothing to eat. I do not want to send them away fasting, or they might faint on the way.”
33 Wanafunzi wake wakasema, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?”
The disciples said to him, “Where could we get so many loaves in a deserted place as to satisfy so great a multitude?”
34 Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
Jesus said to them, “How many loaves do you have?” They said, “Seven, and a few small fish.”
35 Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
He commanded the multitude to sit down on the ground;
36 Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
and he took the seven loaves and the fish. He gave thanks and broke them, and gave to the disciples, and the disciples to the multitudes.
37 Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
They all ate and were filled. They took up seven baskets full of the broken pieces that were left over.
38 Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
Those who ate were four thousand men, in addition to women and children.
39 Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu aliingia katika mashua, akaenda sehemu za Magadani.
Then he sent away the multitudes, got into the boat, and came into the borders of Magdala.

< Mathayo 15 >