< Mathayo 14 >
1 Wakati huo, Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za Yesu,
V tem času zasliši četrtnik Herod glas o Jezusu,
2 akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji; amefufuka kutoka kwa wafu! Hii ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza zinafanya kazi ndani yake.”
Ter reče hlapcem svojim: Ta je Janez Krstnik; on je vstal od mrtvih, in za to dela čudeže.
3 Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake,
Kajti Herod je bil Janeza vjel in ga vklenil in posadil v ječo, za voljo Herodijade, svojega brata Filipa žene.
4 kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode: “Si halali kwako kuwa na huyo mwanamke.”
Kajti Janez mu je djal: Ni ti dovoljeno nje imeti.
5 Herode alitaka sana kumuua Yohana, lakini akaogopa watu, kwa maana walimtambua kuwa ni nabii.
In hotel ga je umoriti; ali zbal se je ljudstva, ker so ga imeli za preroka.
6 Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza mbele ya watu waliohudhuria, akamfurahisha sana Herode,
Ko je bil pa Herodovega rojstva dan, plesala je po sredi Herodijadina hči, in ugodila je Herodu.
7 kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kumpa huyo binti chochote angeomba.
Za to jej s prisego obreče dati, karkoli bi prosila.
8 Huyo binti, akiwa amechochewa na mama yake, akasema, “Nipe kichwa cha Yohana Mbatizaji kwenye sinia.”
Ona pa, naučena od matere svoje: Daj mi, reče, tu v skledi glavo Janeza Krstnika.
9 Mfalme akasikitika, lakini kwa sababu ya viapo alivyoapa mbele ya wageni, akaamuru kwamba apatiwe ombi lake.
In kralju se užali. Pa za voljo prisege in gostov jej ukaže dati.
10 Hivyo akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle gerezani.
In pošlje, in odseka Janezu v ječi glavo.
11 Kichwa chake kikaletwa kwenye sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea mama yake.
Ter prinesó glavo njegovo v skledi, in dadó jo dekletu; in nese jo materi svojej.
12 Wanafunzi wa Yohana wakaja na kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha wakaenda wakamwambia Yesu.
In prišedši učenci njegovi, vzemó truplo in ga pokopljejo; ter pridejo in sporočé Jezusu.
13 Yesu aliposikia yaliyokuwa yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu kupitia nchi kavu kutoka miji.
In slišavši to Jezus, odrine odtod na ladji posebej na samoten kraj. In ko ljudstvo to sliši, odidejo peš za njim iz mest.
14 Yesu alipofika kando ya bahari, aliona makutano makubwa ya watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa wao.
In Jezus izide in ugleda mnogo ljudstva; in zasmilijo mu se, ter uzdravi njih bolnike.
15 Ilipofika jioni, wanafunzi wake walienda kwake, wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na muda sasa umekwisha. Waage makutano ili waende zao vijijini wakajinunulie chakula.”
Ko se je pa zvečerilo, pristopijo k njemu učenci njegovi, govoreč: Kraj je samoten, in ura uže pozna; razpusti ljudstvo, da odidejo v vasí in si kupijo živeža.
16 Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.”
Jezus jim pa reče: Ni jim treba oditi; dajte jim vi jesti.
17 Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na samaki wawili tu.”
Oni mu pa rekó: Nimamo več tu nego pet hlebov in dve ribi,
18 Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.”
On pa reče: Prinesite jih sem!
19 Yesu akaagiza makutano wakae chini kwenye nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akainua macho yake akatazama mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate. Kisha akawapa wanafunzi, nao wanafunzi wakawagawia makutano.
Ter ukaže ljudstvu, naj sedejo po travi, in vzeme petere hlebe in tisti dve ribi, in pogledavši na nebo, blagoslovi; ter prelomi in dá hlebe učencem, učenci pa ljudstvu.
20 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
In jedli so vsi, in nasitili so se; in pobrali so ostanke koscev, dvanajst košev polnih.
21 Idadi ya watu waliokula walikuwa wanaume wapatao 5,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
Bilo jih je pa, kteri so jedli, kakih pet tisoči móž, brez žen in otrók.
22 Mara Yesu akawaambia wanafunzi wake waingie kwenye mashua watangulie kwenda ngʼambo ya bahari, wakati yeye alikuwa akiwaaga wale makutano.
In precej prisili Jezus učence svoje, naj stopijo v ladjo, in gredó naprej na drugo stran, dokler ne razpustí ljudstva.
23 Baada ya kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke yake.
In razpustivši ljudstvo, odide sam posebej na goro molit. Ko se je pa zvečerilo, bil je sam tu.
24 Wakati huo ile mashua ilikuwa mbali kutoka nchi kavu ikisukwasukwa na mawimbi, kwa sababu upepo ulikuwa wa mbisho.
Ladja je bila pa uže sredi morja, in valovi so jo metali; kajti bil je veter nasproti.
25 Wakati wa zamu ya nne ya usiku, Yesu akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea juu ya maji.
O četrtej straži po noči pa odide Jezus k njim, hodé po morji.
26 Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu, wakasema, “Ni mzimu.” Wakapiga yowe kwa kuogopa.
In ko ga učenci ugledajo, da hodi po morji, ustrašijo se in rekó: Prikazen je! in od strahu zakričé.
27 Lakini mara Yesu akasema nao, akawaambia, “Jipeni moyo! Ni mimi. Msiogope.”
Jezus jih pa precej ogovorí, in reče: Bodite srčni! Jaz sem; ne bojte se.
28 Petro akamjibu, “Bwana, ikiwa ni wewe, niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.”
Peter mu pa odgovorí in reče: Gospod! če si ti, ukaži mi, naj pridem k tebi pò vodi.
29 Yesu akamwambia, “Njoo.” Basi Petro akatoka kwenye chombo, akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
On pa reče: Pridi! In stopivši Peter iz ladje, hodil je po vodi, da pride k Jezusu.
30 Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu, naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele, “Bwana, niokoe!”
Ko pa vidi, da je veter močán, uplaši se; in ko se začne potapljati, zavpije, govoreč; Gospod, otmi me!
31 Mara Yesu akaunyoosha mkono wake na kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani haba, kwa nini uliona shaka?”
Jezus pa precej stegne roko in ga prime, ter mu reče: Maloverni! po kaj si dvomil?
32 Nao walipoingia ndani ya mashua, upepo ukakoma.
In ko stopita v ladjo, veter utihne.
33 Ndipo wote waliokuwa ndani ya ile mashua wakamwabudu Yesu, wakisema, “Hakika, wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
Tisti pa, ki so bili v ladji, pristopijo, ter mu se poklonijo, govoreč: Resnično si sin Božji!
34 Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya Genesareti.
In prepeljavši se, pridejo v zemljo Genezaretsko.
35 Watu wa eneo lile walipomtambua Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. Watu wakamletea wagonjwa wao wote,
In ko ga tega kraja možjé spoznajo, pošljejo po vsej tistej okolici; in prinesó mu vse bolnike.
36 wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu pindo la vazi lake, nao wote waliomgusa, wakaponywa.
In prosili so ga, da bi se le robú obleke njegove dotaknili. In kterikoli so se dotaknili, ozdraveli so.