< Mathayo 13 >
1 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
Tisti dan je pa izšel Jezus iz hiše, in sedel je pri morji.
2 Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
In zbere se pri njem mnogo naroda, toliko, da stopi v ladjo in sede; in vse ljudstvo je stalo na bregu.
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
In pripoveda jim v prilikah mnogo, govoreč: Glej, izšel je sejalec sejat.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
In ko je sejal, padlo je nekaj zrnja poleg ceste; in priletele so tice in so ga pozobale.
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
Drugo je pa padlo na skalnata tla, kjer ni imelo mnogo zemlje; in precej je pognalo, ker ni imelo globoke zemlje.
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
Ko je pa vzšlo solnce, ovenelo je; in ker ni imelo korenine, usahnilo je.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
Drugo je pa padlo v trnje; in trnje je zraslo in ga udušilo.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
Drugo je pa padlo na dobro zemljo, in dajalo je sad, nekaj po sto, nekaj pa po šestdeset, a nekaj po trideset.
9 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Kdor ima ušesa, da sliši, naj sliši!
10 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
Pa pristopijo učenci in mu rekó: Za kaj jim v prilikah govoriš?
11 Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
On pa odgovorí in jim reče: Vam je dano, da spoznate skrivnosti nebeškega kraljestva, njim pa ni dano.
12 Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
Kajti kdor ima, dalo mu se bo, in preveč mu bo; kdor pa nima, odvzelo mu se bo tudi to, kar ima.
13 Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
Za to vam govorim v prilikah, ker tisti, kteri vidijo, ne vidijo, in tisti, kteri slišijo, ne slišijo, in ne umejo.
14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
In na njih se izpolnjuje prerokovanje Izaija, ktero pravi: "S sluhom boste slišali, in ne boste umeli; in z očmi boste gledali, in ne boste videli.
15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
Kajti temu ljudstvu je srce okamenelo, in z ušesi težko slišijo, in očí svoje so zatisnili: da ne bi kedaj z očmi videli, in z ušesi slišali, in s srcem umeli in se spreobrnili, in bi jih ozdravil."
16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
Blagor pa vašim očém, da vidijo, in vašim ušesom, da slišijo.
17 Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
Kajti resnično vam pravim, da so mnogi preroki in pravični želeli videti, kar vi vidite, in niso videli; in slišati, kar vi slišite, in niso slišali.
18 “Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
Čujte torej vi priliko o sejalcu!
19 Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
Vsakemu, kdor besedo o kraljestvu sliši, pa je ne ume, pride hudoba, in ukrade, kar je posejano v srcu njegovem; ta je, ki je posejan poleg ceste.
20 Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
Ki je pa posejan na skalnatih tléh, ta je, kdor besedo sliši in jo precej z veseljem sprejema;
21 Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
Ali nima korenine v sebi, nego je nestanoviten. Ko pa nastane stiska ali preganjanje za voljo besede, pohujšuje se precej.
22 Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn )
Ki je pa posejan v trnji, ta je, kdor besedo sliši; ali skrb tega svetá in ničemurnost bogastva uduší besedo, in brez sadú ostane. (aiōn )
23 Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
Ki je pa posejan na dobro zemljo, ta je, kdor besedo sliši in umé; kdor torej rodí sad, in donaša nekteri po sto, nekteri pa po šestdeset, a nekteri po trideset.
24 Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
Predloží jim drugo priliko, govoreč: Nebeško kraljestvo je podobno človeku, kteri je posejal dobro seme na njivi svojej.
25 Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
Ko so pa ljudjé spali, prišel je njegov sovražnik, in posejal je kukolj po pšenici, in odšel.
26 Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
Ko je pa zrastla trava in je donesla sad, pokaže se tudi kukolj.
27 “Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
Pa pridejo hišnega gospodarja hlapci in mu rekó: Gospod! nisi li dobrega semena posejal na svojej njivi? Odkod se je pa vzel kukolj?
28 “Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
On jim pa reče: Sovražnik človek je to storil. Hlapci mu pa rekó: Hočeš li, da gremo in ga izplevemo?
29 “Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
On pa reče: Ne! da ne bi kedaj, trgaje kukolj, izrovali ž njim vred pšenice.
30 Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
Pustite, naj raste oboje skupaj do žetve; in v čas žetve porečem koscem: Poberite najprej kukolj, in povežite ga v snope, da ga sežgem; pšenico pa spravite v žitnico mojo.
31 Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
Predloží jim drugo priliko, govoreč: Nebeško kraljestvo je podobno gorušičnemu zrnu, ktero je človek vzel, in posejal na njivi svojej,
32 Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
Ktero je res najdrobneje od vseh semen: kedar pa zraste, veče je od zelišč, in postane drevo, da prileté tice nebeške in se nastanjujejo po vejah njegovih.
33 Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
Pové jim drugo priliko: Nebeško kraljestvo je podobno kvasu, kterega je žena vzela in primesila trem mericam moke, dokler se vse ne skvasi.
34 Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
Vse to je govoril Jezus ljudém v prilikah, in brez prilike jim ni govoril;
35 Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
Da se izpolni, kar je rečeno po preroku, kteri pravi: "V prilikah bom odprl usta svoja; pripovedal bom skrivnosti od začetka sveta."
36 Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
Tedaj razpustí Jezus ljudstvo, in pride domú. Pa pristopijo k njemu učenci njegovi, govoreč: Razloži nam priliko o kukolji na njivi.
37 Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
On pa odgovorí in jim reče: Sejalec dobrega semena je sin človečji.
38 Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
Njiva je pa svet; a dobro seme, ti so sinovi kraljestva; kukolj so pa sinovi hudobije.
39 Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn )
Sovražnik, kteri ga je posejal, je hudič; žetev je pa konec svetá; a kosci so angelji. (aiōn )
40 “Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn )
Kakor se torej kukolj pobira, in v ognji sežiga, tako bo na koncu tega sveta. (aiōn )
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
Sin človečji bo poslal angelje svoje, in pobrali bodo vsa puhujšanja iz kraljestva njegovega in tiste, kteri delajo krivico,
42 Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
In vrgli jih bodo v ognjeno peč: tam bo jok in škripanje z zobmí.
43 Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
Tedaj se bodo zasvetili pravični kakor solnce v svojega očeta kraljestvu. Kdor ima ušesa, da sliši, naj sliši!
44 “Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
Zopet je nebeško kraljestvo podobno skritemu zakladu na polji, kterega je človek našel in skril; in od veselja svojega je šel in je prodal vse, kar je imel, in kupil je tisto polje.
45 “Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
Zopet je nebeško kraljestvo podobno človeku kupcu, kteri je iskal lepih biserjev.
46 Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
In ko je našel en dragocen biser, šel je, prodal vse, kar je imel, in ga je kupil.
47 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
Zopet je nebeško kraljestvo podobno saku, kteri se je vrgel v morje, in je zajel od vsakega rodú.
48 Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
In ko se je napolnil, izvlekli so ga na kraj in so sedli, in kar je bilo dobro, pobrali so v posode, a kar je bilo slabo, vrgli so proč.
49 Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn )
Tako bo na koncu sveta. Angelji pojdejo, in odločili bodo hudobne izsred pravičnih. (aiōn )
50 Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
In vrgli jih bodo v ognjeno peč; tam bo jok in škripanje z zobmí.
51 Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
Jezus jim reče: Ste li vse to umeli? Rekó mu: Dà, Gospod!
52 Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
On jim pa reče: Za to je vsak pismar, kteri se je naučil kraljestva nebeškega, podoben človeku gospodarju, kteri prinaša iz zaklada svojega novo in staro.
53 Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
In zgodí se, ko Jezus te prilike končá, odide odtod.
54 Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
In prišedši v domovino svojo, učil je v njih shajališči, da so se zavzemali in so govorili: Odkod temu ta modrost in močí?
55 “Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
Ali ni ta tesarjev sin? ali se ne imenuje mati njegova Marija, in bratje njegovi Jakob in Judej in Simon in Juda?
56 Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
In niso li vse sestre njegove pri nas? Odkod torej temu vse to?
57 Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
In pohujševali so se nad njim. Jezus jim pa reče: Prerok ni brez častí, razen v domovini svojej, in na domu svojem.
58 Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
In ni storil ondej mnogo čudežev, za voljo njih nevere.