< Mathayo 13 >
1 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
Ce même jour, Jésus sortit de la maison et s'assit au bord de la mer
2 Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
et on se rassembla en si grand nombre autour de lui qu'il monta dans une barque et y prit place pour parler de là à toute la multitude restée sur le rivage.
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
Il leur dit beaucoup de choses en paraboles: «Voilà que le semeur est sorti pour semer.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
Il jette sa semence, et des grains sont tombés le long du chemin et les oiseaux sont venus et les ont mangés.»
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
«D'autres sont tombés sur un sol pierreux, où il n'y avait pas beaucoup de terre, et ils ont immédiatement poussé, parce que la terre était sans profondeur.
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
Mais le soleil s'est levé et a brûlé la plante qui, n'ayant point de racine, s'est desséchée.»
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
«D'autres grains sont tombés parmi les épines et les épines ont grandi et les ont étouffés.»
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
«D'autres sont tombés dans la bonne terre et ils ont donné du fruit, tel grain en a produit cent, tel autre soixante, tel autre trente.
9 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Que celui qui a des oreilles entende!»
10 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
Ses disciples s'approchèrent et lui dirent: «Pourquoi leur parles-tu en paraboles?»
11 Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
Il leur répondit: «Parce qu'à vous il est donné de pénétrer les mystères du Royaume des cieux, mais à ceux-là, non point.
12 Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
Car à celui qui a, il sera donné, et il sera dans l’abondance; mais à celui qui n'a pas, même ce qu'il a lui sera ôté.
13 Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
C'est pour cela que je leur parle en paraboles, c'est parce que tout en voyant, ils ne voient point; tout en entendant, ils n'entendent ni ne comprennent.
14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
En eux s'accomplit la prophétie d'Ésaïe, qui dit: «De vos oreilles vous entendrez et vous ne comprendrez point; De vos yeux vous regarderez et vous ne verrez point;
15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
Car le coeur de ce peuple s'est épaissi, Leurs oreilles sont devenues sourdes Et leurs yeux se sont fermés, De peur que leurs yeux ne voient, De peur que leurs oreilles n'entendent, De peur que leur coeur ne comprenne, De peur qu'ils ne se convertissent, De peur que je ne les guérisse.
16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
«Heureux vos yeux, à vous, parce qu’ils voient; heureuses vos oreilles, parce qu'elles entendent!
17 Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
car, je vous le dis en vérité, nombre de prophètes et de justes ont désiré voir ce que vous voyez et ne l'ont pas vu, entendre ce que vous entendez et ne l'ont pas entendu.»
18 “Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
«Pour vous donc, écoutez le sens de la parabole du semeur:
19 Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
«Chaque fois qu'un homme entend la parole du Royaume et ne s'en pénètre pas, survient le Malin et il enlève ce qui a été semé dans son coeur; voilà celui qui a reçu la semence le long du chemin.»
20 Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
«Celui qui l'a reçue sur un sol pierreux, c'est l'homme qui entend la parole et qui tout d'abord l'accueille avec joie.
21 Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
Mais il n'a pas de racine en lui-même; il n'est que pour un temps; une affliction ou une persécution survenant à cause de la parole, il y trouve aussitôt une occasion de chute.»
22 Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn )
«Celui qui a reçu la semence parmi les épines, c'est l'homme qui écoute la parole, mais les sollicitudes de ce monde et la séduction de la richesse étouffent la parole et la rendent stérile. » (aiōn )
23 Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
«Celui qui a reçu la semence dans la bonne terre, c'est l'homme qui écoute la parole et s'en pénètre; celui-là porte des fruits et en donne, tantôt cent, tantôt soixante, tantôt trente.»
24 Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
Il leur proposa une autre parabole. «Voici, dit-il, une similitude du Royaume des cieux: Un homme avait semé du bon grain dans son champ;
25 Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
mais pendant que ses gens dormaient, son ennemi vint semer de l'ivraie au milieu du froment et s'en alla.»
26 Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
«Lorsque l'herbe poussa et porta du fruit, on vit paraître l'ivraie.»
27 “Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
«Les serviteurs s'adressèrent au maître de la maison; ils lui dirent: «Seigneur, n'est-ce pas du bon grain que tu as semé dans ton champ? D'où provient donc l’ivraie?»
28 “Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
Il leur répondit: «C'est un ennemi qui a fait cela.» Ils lui dirent alors: «Veux-tu que nous allions l'arracher?» —
29 “Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
«Non, répondit-il, de peur qu'en arrachant l'ivraie, vous ne déraciniez en même temps le froment.
30 Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
Laissez-les croître l'un et l'autre jusqu'à la moisson; au temps de la moisson, je dirai aux moissonneurs: arrachez d'abord l'ivraie et liez-la en gerbes pour la brûler; quant au froment, vous le recueillerez dans mon grenier.»
31 Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
Il leur proposa une autre parabole: «Le Royaume des cieux est semblable à un grain de sénevé qu'un homme prend et sème dans son champ.
32 Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
C'est bien la plus petite de toutes les semences, et quand il a pris sa croissance, il est plus grand que les plantes potagères; il devient un arbre, tellement que les oiseaux du ciel viennent faire leurs nids dans ses branches.»
33 Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
Il leur raconta une autre parabole: «Le Royaume des cieux est semblable à du levain qu'une femme prend et qu'elle cache dans trois mesures de farine jusqu'à ce que le levain ait partout pénétré.»
34 Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
Toutes ces choses, Jésus les dit en paraboles aux multitudes; il ne leur parlait qu'en paraboles
35 Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
(afin que fût accomplie la parole du prophète: «J'ouvrirai ma bouche pour parler en paraboles; Je révélerai des choses restées cachées depuis la création.»)
36 Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
Lorsqu'il eut congédié la foule et fut rentré dans la maison, ses disciples vinrent le trouver et lui dirent: «Explique-nous la parabole de l'ivraie dans le champ.»
37 Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
Il leur répondit: «Celui qui sème le bon grain, c'est le Fils de l'homme.»
38 Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
«Le champ, c'est le monde.» «Le bon grain, ce sont les enfants du Royaume. L'ivraie, ce sont les enfants du Malin.»
39 Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn )
«L'ennemi qui l'a semée, c'est le diable.» «La moisson, c'est la fin du monde; les moissonneurs, ce sont les anges.» (aiōn )
40 “Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn )
«De même donc qu'on arrache l'ivraie et qu'on la brûle dans le feu, de même, à la fin du monde, (aiōn )
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
le Fils de l'homme enverra ses anges et ils arracheront de son Royaume tous les scandales et tous ceux qui opèrent l'iniquité
42 Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
et ils les précipiteront dans l'ardente fournaise. Là seront les pleurs et le grincement des dents.
43 Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
C'est alors que les justes, dans le Royaume de leur Père, resplendiront comme le soleil. — Que celui qui a des oreilles entende»
44 “Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
«Le Royaume des cieux est semblable à un trésor enfoui dans un champ. L'homme qui le trouve le tient caché et puis, débordant de joie, il s'en va vendre tout ce qu'il a et il achète ce champ.»
45 “Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
«Le Royaume des cieux est encore semblable à un marchand en quête de belles perles
46 Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
et qui, en ayant trouvé une d'un grand prix, est allé vendre tout ce qu'il avait et a acheté cette perle.»
47 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
«Le Royaume des cieux est encore semblable à un filet que l'on a jeté en mer et qui a ramassé des poissons de toutes sortes.
48 Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
Quand il a été plein, les pêcheurs l'ont tiré à eux; puis, s'asseyant sur le rivage, ils ont mis tous ceux qui étaient bons dans des jarres et ils ont jeté les mauvaise.
49 Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn )
Il en sera de même à la fin du monde: les anges viendront séparer les méchants du milieu des justes (aiōn )
50 Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
et ils précipiteront ces méchants dans l'ardente fournaise. Là seront les pleurs et le grincement des dents.»
51 Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
«Avez-vous compris tout cela?» — «Oui, répondirent-ils.»
52 Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
Alors il leur dit: «Ainsi donc tout scribe instruit sur le Royaume des cieux est semblable à un homme, chef de maison, qui tire de son trésor des choses nouvelles et des choses anciennes.»
53 Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
Quand Jésus eut achevé de raconter ces paraboles, il partit de là
54 Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
et revint chez ses compatriotes. Il se mit à enseigner dans leur synagogue, ce dont ils furent extrêmement surpris; ils disaient: «D'où lui viennent cette sagesse et ces miracles?
55 “Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
N'est-ce pas là le fils du charpentier? Sa mère ne s'appelle-t-elle pas Marie? Et Jacques, et Joseph, et Simon et Jude ne sont-ils pas ses frères?
56 Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
Ses soeurs ne demeurent-elles pas toutes avec nous? D'où lui vient donc tout cela?»
57 Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
Pour eux il était une occasion de chute. Alors Jésus leur dit: «Un prophète n'est sans honneur que dans sa patrie et dans sa maison.»
58 Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
Aussi ne fit-il là que peu de miracles, à cause de leur incrédulité.