< Mathayo 13 >
1 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
The same day Jesus went out of the house, and sat by the sea side.
2 Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
And great multitudes were gathered together to him, so that he went into a boat, and sat down; and the whole multitude stood on the shore.
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
And he spoke many things to them in parables, saying, Behold, a sower went forth to sow;
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
And when he sowed, some seeds fell by the way side, and the fowls came and devoured them:
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
Some fell upon stony places, where they had not much earth: and immediately they sprung up, because they had no deepness of earth:
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
And when the sun had risen, they were scorched; and because they had no root, they withered away.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
And some fell among thorns; and the thorns sprung up, and choked them:
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
But others fell into good ground, and brought forth fruit, some an hundredfold, some sixtyfold, some thirtyfold.
9 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Who hath ears to hear, let him hear.
10 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
And the disciples came, and said to him, Why speakest thou to them in parables?
11 Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
He answered and said to them, Because it is given to you to know the mysteries of the kingdom of heaven, but to them it is not given.
12 Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
For whoever hath, to him shall be given, and he shall have more abundance: but whoever hath not, from him shall be taken away even that which he hath.
13 Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
Therefore I speak to them in parables: because they seeing see not; and hearing they hear not, neither do they understand.
14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
And in them is fulfilled the prophecy of Isaiah, which saith, By hearing ye shall hear, and shall not understand; and seeing ye shall see, and shall not perceive:
15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
For this people’s heart has become dull, and their ears are hard of hearing, and their eyes they have closed; lest at any time they should see with their eyes, and hear with their ears, and should understand with their heart, and should be converted, and I should heal them.
16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
But blessed are your eyes, for they see: and your ears, for they hear.
17 Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
For verily I say to you, That many prophets and righteous men have desired to see the things which ye see, and have not seen them; and to hear the things which ye hear, and have not heard them.
18 “Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
Hear ye therefore the parable of the sower.
19 Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
When any one heareth the word of the kingdom, and understandeth it not, then cometh the wicked one, and catcheth away that which was sown in his heart. This is he who received seed by the way side.
20 Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
But he that received the seed into stony places, the same is he that heareth the word, and immediately with joy receiveth it;
21 Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
Yet he hath not root in himself, but endureth for a while: for when tribulation or persecution ariseth because of the word, immediately he is offended.
22 Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn )
He also that received seed among the thorns is he that heareth the word; and the care of this world, and the deceitfulness of riches, choke the word, and he becometh unfruitful. (aiōn )
23 Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
But he that received seed into the good ground is he that heareth the word, and understandeth it; who also beareth fruit, and bringeth forth, some an hundredfold, some sixty, some thirty.
24 Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is likened to a man who sowed good seed in his field:
25 Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
But while men slept, his enemy came and sowed tares among the wheat, and went his way.
26 Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
But when the blade had sprung up, and brought forth fruit, then appeared the tares also.
27 “Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
So the servants of the householder came and said to him, Sir, didst thou not sow good seed in thy field? how then hath it tares?
28 “Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
He said to them, An enemy hath done this. The servants said to him, Wilt thou then that we go and gather them up?
29 “Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
But he said, Nay; lest while ye gather up the tares, ye root up also the wheat with them.
30 Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
Let both grow together until the harvest: and in the time of harvest I will say to the reapers, Gather ye together first the tares, and bind them in bundles to burn them: but gather the wheat into my barn.
31 Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is like a grain of mustard seed, which a man took, and sowed in his field:
32 Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
Which indeed is the least of all seeds: but when it is grown, it is the greatest among herbs, and becometh a tree, so that the birds of the air come and lodge on its branches.
33 Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
Another parable he spoke to them; The kingdom of heaven is like leaven, which a woman took, and hid in three measures of meal, till the whole was leavened.
34 Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
All these things Jesus spoke to the multitude in parables; and without a parable he spoke not to them:
35 Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
That it might be fulfilled which was spoken by the prophet, saying, I will open my mouth in parables; I will utter things which have been kept secret from the foundation of the world.
36 Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
Then Jesus sent the multitude away, and went into the house: and his disciples came to him, saying, Make known to us the meaning of the parable of the tares of the field.
37 Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
He answered and said to them, He that soweth the good seed is the Son of man;
38 Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
The field is the world; the good seed are the children of the kingdom; but the tares are the children of the wicked one;
39 Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn )
The enemy that sowed them is the devil; the harvest is the end of the world; and the reapers are the angels. (aiōn )
40 “Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn )
As therefore the tares are gathered and burned in the fire; so shall it be in the end of this world. (aiōn )
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
The Son of man shall send forth his angels, and they shall gather out of his kingdom all things that offend, and them who do iniquity;
42 Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
And shall cast them into a furnace of fire: there shall be wailing and gnashing of teeth.
43 Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
Then shall the righteous shine forth as the sun in the kingdom of their Father. Who hath ears to hear, let him hear.
44 “Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
Again, the kingdom of heaven is like treasure hid in a field; which when a man hath found, he hideth, and from joy over it goeth and selleth all that he hath, and buyeth that field.
45 “Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
Again, the kingdom of heaven is like a merchant man, seeking fine pearls:
46 Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
Who, when he had found one pearl of great price, went and sold all that he had, and bought it.
47 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
Again, the kingdom of heaven is like a net, that was cast into the sea, and gathered of every kind:
48 Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
Which, when it was full, they drew to the shore, and sat down, and gathered the good into vessels, but cast away the bad.
49 Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn )
So shall it be at the end of the world: the angels shall come forth, and separate the wicked from among the righteous, (aiōn )
50 Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
And shall cast them into the furnace of fire: there shall be wailing and gnashing of teeth.
51 Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
Jesus saith to them, Have ye understood all these things? They say to him, Yea, Lord.
52 Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
Then said he to them, Therefore every scribe who is instructed concerning the kingdom of heaven is like a man that is an householder, who bringeth forth out of his treasure things new and old.
53 Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
And it came to pass, that when Jesus had finished these parables, he departed from there.
54 Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
And when he had come into his own country, he taught them in their synagogue, so that they were astonished, and said, How hath this man this wisdom, and these mighty works?
55 “Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
Is not this the carpenter’s son? is not his mother called Mary? and his brethren, James, and Joses, and Simon, and Judas?
56 Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
And his sisters, are they not all with us? How then hath this man all these things?
57 Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
And they were offended in him. But Jesus said to them, A prophet is not without honour, except in his own country, and in his own house.
58 Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
And he did not many mighty works there because of their unbelief.