< Mathayo 13 >

1 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
The same day Jesus went out of the house, and sat by the shore of the lake;
2 Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
and great multitudes were gathered together to him, so that he went into a boat, and sat down; and all the multitude stood on the beach.
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
And he spoke many things to them in parables, saying, Behold, a sower went forth to sow.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
And as he sowed, some seeds fell by the wayside; and the birds came and devoured them.
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
And others fell upon rocky places, where they had not much earth; and they sprung up immediately, because they had no depth of earth.
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
But when the sun was up, they were scorched; and because they had no root, they withered away.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
And others fell among thorns; and the thorns grew up, and choked them.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
And others fell upon good ground; and yielded fruit, some a hundred fold, some Sixty, some thirty fold.
9 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
He that hath ears, let him hear.
10 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
And the disciples came and said to him, Why dost thou speak to them in parables?
11 Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
He answered and said, Because to you it hath been given to know the mysteries of the kingdom of heaven; but to them it hath not been given.
12 Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
For whoever hath, to him will be given, and he will have abundance; but whoever hath not, from him will be taken away even what he hath.
13 Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
Therefore I speak to them in parables, because seeing they see not, and hearing they hear not, nor understand.
14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
And in them is fulfilled the prophecy of Isaiah, which saith, “Ye will hear indeed, and not understand; and ye will see indeed, and not perceive.
15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
For this people's heart hath become gross, and their ears are dull of hearing, and their eyes they have closed, lest they should see with their eyes, and hear with their ears, and understand with their heart, and turn from their ways, and I should heal them.”
16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
But blessed are your eyes, for they see; and your ears, for they hear.
17 Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
Truly do I say to you, that many prophets and righteous men desired to see the things which ye see, and did not see them; and to hear the things which ye hear, and did not hear them.
18 “Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
Hear ye therefore the parable of the sower.
19 Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
When any one heareth the word of the kingdom, and understandeth it not, the Evil One cometh, and snatcheth away that which was sown in his heart; this man is what was sown by the wayside.
20 Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
And what was sown on the rocky places, this is he that heareth the word, and immediately receiveth it with joy,
21 Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
but, having no root within him, endureth only for a time; and when tribulation or persecution ariseth on account of the word, he immediately falleth away.
22 Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn g165)
And what was sown among the thorns, this is he that heareth the word, but the cares of the world and the deceitfulness of riches choke the word, and he becometh unfruitful. (aiōn g165)
23 Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
And what was sown on the good ground, this is he that heareth the word, and understandeth it; who also beareth fruit, and yieldeth, one a hundred fold, another sixty, another thirty fold.
24 Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is like a man who sowed good seed in his field.
25 Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
But while men slept, his enemy came, and sowed tares among the wheat; and went away.
26 Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
But when the blade grew up, and put forth fruit, then appeared the tares also.
27 “Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
So the servants of the householder came and said to him, Sir, didst not thou sow good seed in thy field? Whence then hath it tares?
28 “Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
He said to them, An enemy did this. The servants say to him, Dost thou wish then that we go and gather them up?
29 “Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
But he said, Nay; lest, while ye gather up the tares, ye root up the wheat with them.
30 Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
Let both grow together until the harvest; and in the time of harvest I will say to the reapers, Gather up first the tares, and bind them in bundles, to burn them; but gather the wheat into my barn.
31 Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
Another parable he put forth to them, saying, The kingdom of heaven is like a grain of mustard, which a man took and sowed in his field.
32 Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
Which is the least indeed of all seeds; but when it is grown, it is greater than the herbs, and becometh a tree, so that the birds of the air come and lodge in its branches.
33 Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
Another parable he spoke to them: The kingdom of heaven is like leaven, which a woman took and hid in three measures of meal, till the whole was leavened.
34 Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
All these things Jesus spoke to the multitudes in parables, and without a parable he spoke nothing to them;
35 Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
that it might be fulfilled which was spoken through the prophet Isaiah, saying, “I will open my mouth in parables; I will utter things hidden from the foundation [[of the world]].”
36 Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
Then he sent the multitudes away, and went into the house. And his disciples came to him, saying, Explain to us the parable of the tares of the field.
37 Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
He answered and said, He that soweth the good seed is the Son of man.
38 Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
The field is the world; the good seed is the sons of the kingdom; but the tares are the sons of the Evil One;
39 Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
the enemy that sowed them is the Devil; the harvest is the end of the world; and the reapers are angels. (aiōn g165)
40 “Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn g165)
As therefore the tares are gathered up and burned with fire, so will it be at the end of the world. (aiōn g165)
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
The Son of man will send forth his angels, and they will gather out of his kingdom all the stumbling-blocks, and those who do iniquity,
42 Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
and will cast them into the furnace of fire; there will be wailing and gnashing of teeth.
43 Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
Then will the righteous shine forth as the sun, in the kingdom of their Father. He that hath ears, let him hear.
44 “Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
The kingdom of heaven is like a treasure hid in a field, which a man found and hid; and for joy thereof he goeth and selleth all that he hath, and buyeth that field.
45 “Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
Again, the kingdom of heaven is like a merchant seeking goodly pearls.
46 Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
And having found one pearl of great price, he went and sold all that he had, and bought it.
47 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
Again, the kingdom of heaven is like a net, cast into the sea, and bringing together fish of every kind;
48 Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
which, when it was full, they drew upon the beach, and sat down and gathered the good into vessels, but threw the bad away.
49 Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn g165)
So will it be at the end of the world. The angels will come forth, and separate the wicked from among the righteous, (aiōn g165)
50 Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
and will cast them into the furnace of fire; there will be wailing and gnashing of teeth.
51 Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
Did ye understand all these things? They say to him, Yea.
52 Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
And he said to them, Thus then every scribe, instructed for the kingdom of heaven, is like a householder, who bringeth out from his storehouse things new and old.
53 Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
And it came to pass, when Jesus had ended these parables, that he departed thence.
54 Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
And having come into his own country, he taught them in their synagogue, so that they were astonished, and said, Whence hath this man this wisdom, and the miracles?
55 “Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
Is not this the carpenter's son? Is not his mother called Mary, and his brothers, James, and Joseph, and Simon, and Judas?
56 Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
And his sisters, are they not all with us? Whence then hath this man all these things?
57 Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
And they took offence at him. But Jesus said to them, A prophet is not without honor, except in his own country, and in his own house.
58 Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
And he did not work many miracles there, because of their unbelief.

< Mathayo 13 >