< Mathayo 13 >

1 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
On the same day Jesus went out of the house and sat by the sea.
2 Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
And large crowds were gathered together to Him, so He got into a boat to sit down; and the whole crowd stood on the shore.
3 Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
Then He spoke many things to them in parables saying: “Listen, a sower went out to sow.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
And as he sowed, some seeds fell alongside the road, and the birds came and devoured them.
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
Others fell on stony places, where they did not have much earth; so they sprouted quickly because they had no depth of earth.
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
But when the sun came up they were scorched, and because they had no root they withered away.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
And others fell among the thorns, and the thorns grew up and smothered them.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
But others fell on the good ground and yielded a crop: some a hundredfold, some sixty, some thirty.
9 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
He who has ears to hear, let him hear!”
10 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
And the disciples approached and said to Him, “Why do you speak to them in parables?”
11 Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
So in answer He said to them: “To you it has been given to know the mysteries of the kingdom of the heavens, but to them it has not been given.
12 Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
For whoever has, to him more will be given and he will have abundance; but whoever does not have, even what he has will be taken away from him.
13 Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
Therefore I speak to them in parables, that seeing they not see and hearing they not hear nor understand.
14 Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
And in them the prophecy of Isaiah is fulfilled, which says: ‘By hearing you (ye) will hear and not understand, and seeing you will see and not perceive.
15 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
Because the A hearts of this people have grown dull, and their B ears hard of hearing, and their C eyes they have closed; lest they should see with their C eyes and hear with their B ears and understand with their A hearts, and turn around; and I would heal them.’
16 Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
But blessed are your eyes because they see, and your ears because they hear;
17 Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
for assuredly I say to you that many prophets and righteous ones desired to see what you see and did not see it, and to hear what you hear and did not hear it.
18 “Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
“Therefore hear the parable of the sower:
19 Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
When anyone hears the word of the kingdom and does not understand, the malignant one comes and snatches away what was sown in his heart—this is the seed sown alongside the road.
20 Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
But the seed sown on stony places—this is he who hears the word and directly receives it with joy,
21 Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
but he has no root in himself and is short-lived; for when trial or persecution comes because of the word, directly he is offended.
22 Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn g165)
But the seed sown among the thorns—this is he who hears the word, but the care of this age and the deceitfulness of riches choke out the word, and it becomes fruitless. (aiōn g165)
23 Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
Now the seed sown on the good ground—this is he who hears the word and understands, who indeed bears fruit and produces: some a hundredfold, some sixty, some thirty.”
24 Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
He put another parable to them, saying: “The kingdom of the heavens is like a man who sowed good seed in his field;
25 Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
but while the people were sleeping his enemy came and sowed tares among the wheat and went away.
26 Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
But when the stalk sprouted and produced fruit, then the tares also appeared.
27 “Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
So the servants of the owner came and said to him, ‘Sir, was it not good seed that you sowed in your field? How then does it have tares?’
28 “Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
He said to them, ‘An enemy did it.’ The servants said to him, ‘So do you want us to go and gather them up?’
29 “Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
But he said: ‘No, lest gathering up the tares you also uproot the wheat with them.
30 Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
Let both grow together until the harvest, and at the time of the harvest I will say to the reapers, “First gather up the tares and bind them into bundles to burn them, but gather the wheat into my barn.”’”
31 Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
He put another parable to them, saying: “The kingdom of the heavens is like a mustard seed which a man took and sowed in his field;
32 Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
which indeed is smaller than all the seeds, but when it is grown it is greater than all the vegetables and becomes a tree, so that the birds of the air come and rest in its branches.”
33 Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
He spoke another parable to them: “The kingdom of the heavens is like yeast, which a woman took and hid in three measures of meal until it was all leavened.”
34 Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
All these things Jesus spoke to the crowds in parables, and without a parable He did not speak to them,
35 Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
so that what was spoken through the prophet should be fulfilled, namely: “I will open my mouth in parables; I will utter things kept secret from the foundation of the world.”
36 Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
Then Jesus dismissed the crowds and went into the house. And His disciples approached Him saying, “Explain to us the parable of the tares of the field.”
37 Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
So He answered and said to them: “He who sows the good seed is the Son of the Man.
38 Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
The field is the world; as for the good seed, these are the sons of the kingdom, while the tares are the sons of the malignant one.
39 Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
The enemy who sowed them is the devil; the harvest is the end of the age, and the reapers are angels. (aiōn g165)
40 “Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn g165)
Therefore just as the tares are gathered and burned with fire, so it will be at the end of this age. (aiōn g165)
41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
The Son of the Man will send out His angels, and they will collect out of His kingdom everything that is offensive, and those who perpetrate lawlessness;
42 Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
and they will throw them into the furnace of fire. There there will be weeping and gnashing of teeth.
43 Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
Then the righteous will shine forth as the sun in the kingdom of their Father. He who has ears to hear, let him hear.
44 “Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
“Again, the kingdom of the heavens is like a treasure hidden in a field, which a man found and re-hid, and in his joy he goes and sells everything he has and buys that field.
45 “Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
“Again, the kingdom of the heavens is like a man, a merchant, seeking beautiful pearls,
46 Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
who upon finding one very valuable pearl went and sold everything he had and bought it.
47 “Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
“Again, the kingdom of the heavens is like a seine that was cast into the sea and gathered of every kind,
48 Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
which, when it was full, they pulled upon the shore; and sitting down they collected the good into vessels, but threw out the bad.
49 Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn g165)
So it will be at the end of the age. The angels will come forth and will separate the malignant out from among the righteous, (aiōn g165)
50 Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
and they will throw them into the furnace of fire. There there will be weeping and gnashing of teeth.”
51 Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
Jesus says to them, “Did you understand all these things?” They say to Him, “Yes, Lord.”
52 Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
So He said to them, “Therefore every scribe who has been discipled into the kingdom of the heavens is like a man, a householder, who brings out of his reservoir things new and old.”
53 Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
Now it happened, when Jesus had finished these parables, that He departed from there.
54 Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
And coming into His hometown He began to teach them in their synagogue, so that they were astonished and said: “Where did this man get this wisdom, and the mighty works?
55 “Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
Is this not the carpenter's son? Is not his mother called Mary, and his brothers James and Joses and Simon and Jude?
56 Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
And his sisters, are they not all with us? Where then did this man get all these things?”
57 Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
So they were offended at him. But Jesus said to them, “A prophet is not without honor except in his hometown and in his own house.”
58 Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.
And He did not do many mighty works there because of their unbelief.

< Mathayo 13 >