< Mathayo 12 >

1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
anantaraM yIzu rvizrAmavArE zsyamadhyEna gacchati, tadA tacchiSyA bubhukSitAH santaH zsyamanjjarIzchatvA chitvA khAditumArabhanta|
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
tad vilOkya phirUzinO yIzuM jagaduH, pazya vizrAmavArE yat karmmAkarttavyaM tadEva tava ziSyAH kurvvanti|
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
sa tAn pratyAvadata, dAyUd tatsagginazca bubhukSitAH santO yat karmmAkurvvan tat kiM yuSmAbhi rnApAThi?
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
yE darzanIyAH pUpAH yAjakAn vinA tasya tatsaggimanujAnAnjcAbhOjanIyAsta IzvarAvAsaM praviSTEna tEna bhuktAH|
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
anyacca vizrAmavArE madhyEmandiraM vizrAmavArIyaM niyamaM lagvantOpi yAjakA nirdOSA bhavanti, zAstramadhyE kimidamapi yuSmAbhi rna paThitaM?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
yuSmAnahaM vadAmi, atra sthAnE mandirAdapi garIyAn Eka AstE|
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
kintu dayAyAM mE yathA prIti rna tathA yajnjakarmmaNi| EtadvacanasyArthaM yadi yuyam ajnjAsiSTa tarhi nirdOSAn dOSiNO nAkArSTa|
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
anyacca manujasutO vizrAmavArasyApi patirAstE|
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
anantaraM sa tatsthAnAt prasthAya tESAM bhajanabhavanaM praviSTavAn, tadAnIm EkaH zuSkakarAmayavAn upasthitavAn|
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
tatO yIzum apavadituM mAnuSAH papracchuH, vizrAmavArE nirAmayatvaM karaNIyaM na vA?
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
tEna sa pratyuvAca, vizrAmavArE yadi kasyacid avi rgarttE patati, tarhi yastaM ghRtvA na tOlayati, EtAdRzO manujO yuSmAkaM madhyE ka AstE?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
avE rmAnavaH kiM nahi zrEyAn? atO vizrAmavArE hitakarmma karttavyaM|
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
anantaraM sa taM mAnavaM gaditavAn, karaM prasAraya; tEna karE prasAritE sOnyakaravat svasthO'bhavat|
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
tadA phirUzinO bahirbhUya kathaM taM haniSyAma iti kumantraNAM tatprAtikUlyEna cakruH|
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
tatO yIzustad viditvA sthanAntaraM gatavAn; anyESu bahunarESu tatpazcAd gatESu tAn sa nirAmayAn kRtvA ityAjnjApayat,
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
yUyaM mAM na paricAyayata|
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
tasmAt mama prIyO manOnItO manasastuSTikArakaH| madIyaH sEvakO yastu vidyatE taM samIkSatAM| tasyOpari svakIyAtmA mayA saMsthApayiSyatE| tEnAnyadEzajAtESu vyavasthA saMprakAzyatE|
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
kEnApi na virOdhaM sa vivAdanjca kariSyati| na ca rAjapathE tEna vacanaM zrAvayiSyatE|
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
vyavasthA calitA yAvat nahi tEna kariSyatE| tAvat nalO vidIrNO'pi bhaMkSyatE nahi tEna ca| tathA sadhUmavarttinjca na sa nirvvApayiSyatE|
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
pratyAzAnjca kariSyanti tannAmni bhinnadEzajAH|
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
yAnyEtAni vacanAni yizayiyabhaviSyadvAdinA prOktAnyAsan, tAni saphalAnyabhavan|
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
anantaraM lOkai statsamIpam AnItO bhUtagrastAndhamUkaikamanujastEna svasthIkRtaH, tataH sO'ndhO mUkO draSTuM vaktunjcArabdhavAn|
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
anEna sarvvE vismitAH kathayAnjcakruH, ESaH kiM dAyUdaH santAnO nahi?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
kintu phirUzinastat zrutvA gaditavantaH, bAlsibUbnAmnO bhUtarAjasya sAhAyyaM vinA nAyaM bhUtAn tyAjayati|
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
tadAnIM yIzustESAm iti mAnasaM vijnjAya tAn avadat kinjcana rAjyaM yadi svavipakSAd bhidyatE, tarhi tat ucchidyatE; yacca kinjcana nagaraM vA gRhaM svavipakSAd vibhidyatE, tat sthAtuM na zaknOti|
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
tadvat zayatAnO yadi zayatAnaM bahiH kRtvA svavipakSAt pRthak pRthak bhavati, tarhi tasya rAjyaM kEna prakArENa sthAsyati?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
ahanjca yadi bAlsibUbA bhUtAn tyAjayAmi, tarhi yuSmAkaM santAnAH kEna bhUtAn tyAjayanti? tasmAd yuSmAkam EtadvicArayitArasta Eva bhaviSyanti|
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
kintavahaM yadIzvarAtmanA bhUtAn tyAjayAmi, tarhIzvarasya rAjyaM yuSmAkaM sannidhimAgatavat|
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
anyanjca kOpi balavanta janaM prathamatO na badvvA kEna prakArENa tasya gRhaM pravizya taddravyAdi lOThayituM zaknOti? kintu tat kRtvA tadIyagRsya dravyAdi lOThayituM zaknOti|
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
yaH kazcit mama svapakSIyO nahi sa vipakSIya AstE, yazca mayA sAkaM na saMgRhlAti, sa vikirati|
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
ataEva yuSmAnahaM vadAmi, manujAnAM sarvvaprakArapApAnAM nindAyAzca marSaNaM bhavituM zaknOti, kintu pavitrasyAtmanO viruddhanindAyA marSaNaM bhavituM na zaknOti|
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
yO manujasutasya viruddhAM kathAM kathayati, tasyAparAdhasya kSamA bhavituM zaknOti, kintu yaH kazcit pavitrasyAtmanO viruddhAM kathAM kathayati nEhalOkE na prEtya tasyAparAdhasya kSamA bhavituM zaknOti| (aiōn g165)
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
pAdapaM yadi bhadraM vadatha, tarhi tasya phalamapi sAdhu vaktavyaM, yadi ca pAdapaM asAdhuM vadatha, tarhi tasya phalamapyasAdhu vaktavyaM; yataH svIyasvIyaphalEna pAdapaH paricIyatE|
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
rE bhujagavaMzA yUyamasAdhavaH santaH kathaM sAdhu vAkyaM vaktuM zakSyatha? yasmAd antaHkaraNasya pUrNabhAvAnusArAd vadanAd vacO nirgacchati|
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
tEna sAdhurmAnavO'ntaHkaraNarUpAt sAdhubhANPAgArAt sAdhu dravyaM nirgamayati, asAdhurmAnuSastvasAdhubhANPAgArAd asAdhuvastUni nirgamayati|
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
kintvahaM yuSmAn vadAmi, manujA yAvantyAlasyavacAMsi vadanti, vicAradinE taduttaramavazyaM dAtavyaM,
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
yatastvaM svIyavacObhi rniraparAdhaH svIyavacObhizca sAparAdhO gaNiSyasE|
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
tadAnIM katipayA upAdhyAyAH phirUzinazca jagaduH, hE gurO vayaM bhavattaH kinjcana lakSma didRkSAmaH|
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
tadA sa pratyuktavAn, duSTO vyabhicArI ca vaMzO lakSma mRgayatE, kintu bhaviSyadvAdinO yUnasO lakSma vihAyAnyat kimapi lakSma tE na pradarzayiSyantE|
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
yatO yUnam yathA tryahOrAtraM bRhanmInasya kukSAvAsIt, tathA manujaputrOpi tryahOrAtraM mEdinyA madhyE sthAsyati|
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
aparaM nInivIyA mAnavA vicAradina EtadvaMzIyAnAM pratikUlam utthAya tAn dOSiNaH kariSyanti, yasmAttE yUnasa upadEzAt manAMsi parAvarttayAnjcakrirE, kintvatra yUnasOpi gurutara Eka AstE|
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
punazca dakSiNadEzIyA rAjnjI vicAradina EtadvaMzIyAnAM pratikUlamutthAya tAn dOSiNaH kariSyati yataH sA rAjnjI sulEmanO vidyAyAH kathAM zrOtuM mEdinyAH sImna Agacchat, kintu sulEmanOpi gurutara EkO janO'tra AstE|
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
aparaM manujAd bahirgatO 'pavitrabhUtaH zuSkasthAnEna gatvA vizrAmaM gavESayati, kintu tadalabhamAnaH sa vakti, yasmA; nikEtanAd AgamaM, tadEva vEzma pakAvRtya yAmi|
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
pazcAt sa tat sthAnam upasthAya tat zUnyaM mArjjitaM zObhitanjca vilOkya vrajan svatOpi duSTatarAn anyasaptabhUtAn sagginaH karOti|
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
tatastE tat sthAnaM pravizya nivasanti, tEna tasya manujasya zESadazA pUrvvadazAtOtIvAzubhA bhavati, EtESAM duSTavaMzyAnAmapi tathaiva ghaTiSyatE|
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
mAnavEbhya EtAsAM kathanAM kathanakAlE tasya mAtA sahajAzca tEna sAkaM kAnjcit kathAM kathayituM vAnjchantO bahirEva sthitavantaH|
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
tataH kazcit tasmai kathitavAn, pazya tava jananI sahajAzca tvayA sAkaM kAnjcana kathAM kathayituM kAmayamAnA bahistiSThanti|
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
kintu sa taM pratyavadat, mama kA jananI? kE vA mama sahajAH?
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
pazcAt ziSyAn prati karaM prasAryya kathitavAn, pazya mama jananI mama sahajAzcaitE;
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
yaH kazcit mama svargasthasya pituriSTaM karmma kurutE, saEva mama bhrAtA bhaginI jananI ca|

< Mathayo 12 >