< Mathayo 12 >
1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
W tym czasie Jezus przechodził w szabat wśród zbóż, a jego uczniowie byli głodni i zaczęli zrywać kłosy, i jeść.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
Kiedy faryzeusze to zobaczyli, powiedzieli mu: Oto twoi uczniowie robią to, czego nie wolno robić w szabat.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
A on im powiedział: Czy nie czytaliście, co zrobił Dawid, gdy był głodny, on i ci, którzy z nim byli?
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
Jak wszedł do domu Bożego i jadł chleby pokładne, których nie wolno było jeść jemu ani tym, którzy z nim byli, tylko samym kapłanom?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Albo czy nie czytaliście w prawie, że w szabat kapłani w świątyni naruszają szabat, a są bez winy?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
Ale mówię wam, że tu jest [ktoś] większy niż świątynia.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
A gdybyście wiedzieli, co to znaczy: Miłosierdzia chcę, a nie ofiary, nie potępialibyście niewinnych.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
Syn Człowieczy bowiem jest też Panem szabatu.
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
I odszedłszy stamtąd, wszedł do ich synagogi.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
A był tam człowiek, który miał uschłą rękę. I chcąc go oskarżyć, zapytali: Czy wolno uzdrawiać w szabat?
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
A on im odpowiedział: Któż z was, mając jedną owcę, która w szabat wpadłaby do dołu, nie chwyci jej i nie wyciągnie?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
A o ileż ważniejszy jest człowiek niż owca! Tak więc wolno w szabat dobrze czynić.
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Wtedy powiedział do tego człowieka: Wyciągnij rękę. On ją wyciągnął i znowu stała się zdrowa jak i druga.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
A faryzeusze, wyszedłszy, naradzali się przeciwko niemu, w jaki sposób go zgładzić.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
Lecz Jezus, poznawszy to, odszedł stamtąd. Poszło za nim mnóstwo ludzi, a on uzdrowił ich wszystkich.
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
I przykazał im, aby go nie ujawniali;
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
Żeby się wypełniło, co zostało powiedziane przez proroka Izajasza, który powiedział:
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
Oto mój sługa, którego wybrałem, mój umiłowany, w którym moja dusza ma upodobanie. Złożę na nim mojego Ducha, a on ogłosi sąd narodom.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
Nie będzie się spierał ani krzyczał i nikt nie usłyszy na ulicach jego głosu.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
Trzciny nadłamanej nie złamie, a knota tlącego się nie zagasi, dopóki nie doprowadzi sądu do zwycięstwa.
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
A w jego imieniu narody będą pokładać nadzieję.
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Wtedy przyprowadzono do niego opętanego, który był ślepy i niemy. I uzdrowił go tak, że ten ślepy i niemy mówił i widział.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
A wszyscy ludzie, zdumieni, mówili: Czyż to nie jest syn Dawida?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
Ale faryzeusze, usłyszawszy to, powiedzieli: On nie wypędza demonów inaczej, jak tylko przez Belzebuba, władcę demonów.
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
Lecz Jezus, znając ich myśli, powiedział im: Każde królestwo podzielone wewnętrznie pustoszeje i żadne miasto albo dom podzielony wewnętrznie nie przetrwa.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
A jeśli szatan wypędza szatana, jest podzielony wewnętrznie. Jakże więc przetrwa jego królestwo?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
Jeśli ja przez Belzebuba wypędzam demony, to przez kogo wypędzają wasi synowie? Dlatego oni będą waszymi sędziami.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
A jeśli ja wypędzam demony Duchem Bożym, to przyszło do was królestwo Boże.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Albo jak może ktoś wejść do domu mocarza i zagrabić jego własność, jeśli najpierw nie zwiąże mocarza? Dopiero wtedy ograbi jego dom.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
Kto nie jest ze mną, jest przeciwko mnie, a kto nie zbiera ze mną, rozprasza.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Dlatego mówię wam: Każdy grzech i bluźnierstwo będzie ludziom przebaczone, ale bluźnierstwo przeciwko Duchowi [Świętemu] nie będzie ludziom przebaczone.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn )
I ktokolwiek powie słowo przeciwko Synowi Człowieczemu, będzie mu przebaczone, ale kto mówi przeciwko Duchowi Świętemu, nie będzie mu przebaczone ani w tym świecie, ani w przyszłym. (aiōn )
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Sprawcie, aby drzewo było dobre i jego owoc dobry, albo sprawcie, aby drzewo było złe i jego owoc zły. Po owocu bowiem poznaje się drzewo.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
Plemię żmijowe! Jakże możecie mówić dobre rzeczy, będąc złymi? Gdyż z obfitości serca mówią usta.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
Dobry człowiek wydobywa z dobrego skarbca serca dobre [rzeczy], a zły człowiek wydobywa ze złego skarbca złe [rzeczy].
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
Ale mówię wam, że z każdego bezużytecznego słowa, które wypowiedzą ludzie, zdadzą sprawę w dzień sądu.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
Bo na podstawie twoich słów będziesz usprawiedliwiony i na podstawie twoich słów będziesz potępiony.
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Wtedy niektórzy z uczonych w Piśmie i z faryzeuszy odpowiedzieli: Nauczycielu, chcemy widzieć znak od ciebie.
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
A on odpowiedział im: Pokolenie złe i cudzołożne żąda znaku, ale żaden znak nie będzie mu dany, oprócz znaku proroka Jonasza.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
Jak bowiem Jonasz był w brzuchu wieloryba trzy dni i trzy noce, tak Syn Człowieczy będzie w sercu ziemi trzy dni i trzy noce.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
Ludzie z Niniwy staną na sądzie z tym pokoleniem i potępią je, ponieważ pokutowali wskutek głoszenia Jonasza, a oto tu [ktoś] więcej niż Jonasz.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
Królowa z Południa stanie na sądzie z tym pokoleniem i potępi je, bo przybyła z krańców ziemi, aby słuchać mądrości Salomona, a oto tu [ktoś] więcej niż Salomon.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
Kiedy nieczysty duch wychodzi z człowieka, przechadza się po miejscach bezwodnych, szukając odpoczynku, ale nie znajduje.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Wtedy mówi: Wrócę do swego domu, z którego wyszedłem. A przyszedłszy, zastaje [go] pustym, zamiecionym i przyozdobionym.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Wówczas idzie i bierze ze sobą siedem innych duchów gorszych niż on sam i wszedłszy, mieszkają tam. I końcowy stan tego człowieka staje się gorszy niż początkowy. Tak będzie i z tym złym pokoleniem.
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
A gdy on jeszcze mówił do ludzi, jego matka i bracia stanęli przed domem, chcąc z nim rozmawiać.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
I powiedział mu ktoś: Oto twoja matka i twoi bracia stoją przed domem, chcąc z tobą mówić.
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
Lecz on odpowiedział temu, który mu to oznajmił: Któż jest moją matką i kto to są moi bracia?
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
A wyciągnąwszy rękę ku swoim uczniom, powiedział: Oto moja matka i moi bracia!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
Kto bowiem wypełnia wolę mojego Ojca, który jest w niebie, ten jest moim bratem i siostrą, i matką.