< Mathayo 12 >

1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
En ce temps-là, Jésus traversait les champs de blé le jour du sabbat. Ses disciples, qui avaient faim, se mirent à arracher des épis et à manger.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
Mais les pharisiens, voyant cela, lui dirent: « Voici que tes disciples font ce qu'il n'est pas permis de faire le jour du sabbat. »
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
Mais il leur dit: « N'avez-vous pas lu ce que fit David quand il eut faim, et ceux qui étaient avec lui:
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
comment il est entré dans la maison de Dieu et a mangé le pain de proposition, qu'il ne lui était pas permis de manger, ni à ceux qui étaient avec lui, mais seulement aux prêtres?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
N'avez-vous pas lu dans la loi que, le jour du sabbat, les prêtres du temple profanent le sabbat et ne sont pas coupables?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
Mais moi, je vous dis que quelqu'un de plus grand que le temple est ici.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
Mais si vous aviez su ce que cela signifie: « Je veux la miséricorde et non les sacrifices", vous n'auriez pas condamné les innocents.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
Car le Fils de l'homme est le maître du sabbat. »
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
Il partit de là et entra dans leur synagogue.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
Et voici, il y avait là un homme qui avait la main desséchée. Ils lui demandèrent: « Est-il permis de guérir le jour du sabbat? », afin de l'accuser.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
Il leur dit: « Quel est parmi vous l'homme qui a une brebis et qui, si celle-ci tombe dans une fosse le jour du sabbat, ne la saisit pas pour la retirer?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
Combien l'homme a-t-il plus de valeur qu'une brebis! Il est donc permis de faire du bien le jour du sabbat. »
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Alors il dit à l'homme: « Étends ta main. » Il l'étendit; et elle fut rendue entière, comme l'autre.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
Mais les pharisiens sortirent et conspirèrent contre lui, afin de le faire périr.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
Jésus, s'en étant aperçu, se retira de là. Une grande foule le suivit; il les guérit tous,
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
et leur ordonna de ne pas le faire connaître,
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
afin que s'accomplît ce qui avait été annoncé par Ésaïe, le prophète, en ces termes,
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
« Voici mon serviteur que j'ai choisi, mon bien-aimé, en qui mon âme se complaît. Je mettrai mon Esprit sur lui. Il proclamera la justice aux nations.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
Il ne luttera pas, il ne criera pas, personne n'entendra sa voix dans les rues.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
Il ne brisera pas un roseau meurtri. Il n'éteindra pas un lin qui fume, jusqu'à ce qu'il mène la justice à la victoire.
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
En son nom, les nations espéreront. »
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Alors on lui amena un démoniaque, aveugle et muet, et il le guérit, de sorte que l'aveugle et le muet parlaient et voyaient.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
Toute la foule était stupéfaite et disait: « Est-ce là le fils de David? »
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
Mais les pharisiens, ayant entendu cela, dirent: « Cet homme ne chasse les démons que par Béelzébul, le prince des démons. »
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
Connaissant leurs pensées, Jésus leur dit: « Tout royaume divisé contre lui-même est dévasté, et toute ville ou maison divisée contre elle-même ne peut subsister.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
Si Satan chasse Satan, il est divisé contre lui-même. Comment donc son royaume subsistera-t-il?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
Si c'est par Béelzébul que je chasse les démons, par qui vos enfants les chassent-ils? C'est pourquoi ils seront vos juges.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
Mais si c'est par l'Esprit de Dieu que je chasse les démons, alors le Royaume de Dieu est venu sur vous.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Ou bien, comment peut-on entrer dans la maison d'un homme fort et piller ses biens, si l'on ne lie d'abord l'homme fort? Alors il pillera sa maison.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
« Celui qui n'est pas avec moi est contre moi, et celui qui n'assemble pas avec moi se disperse.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
C'est pourquoi je vous le dis: tout péché et tout blasphème sera pardonné aux hommes, mais le blasphème contre l'Esprit ne sera pas pardonné aux hommes.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
Quiconque parlera contre le Fils de l'homme, il lui sera pardonné; mais quiconque parlera contre le Saint-Esprit, il ne lui sera pardonné ni dans ce siècle, ni dans celui qui vient. (aiōn g165)
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
« Ou bien faites que l'arbre soit bon et que son fruit soit bon, ou bien faites que l'arbre soit corrompu et que son fruit soit corrompu; car on reconnaît l'arbre à son fruit.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
Races de vipères, comment pouvez-vous, étant méchants, dire de bonnes choses? Car c'est de l'abondance du cœur que la bouche parle.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
L'homme bon, de son bon trésor, tire de bonnes choses, et l'homme mauvais, de son mauvais trésor, tire de mauvaises choses.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
Je vous le dis: toute parole oiseuse que les hommes prononcent, ils en rendront compte au jour du jugement.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
Car c'est par vos paroles que vous serez justifiés, et c'est par vos paroles que vous serez condamnés. »
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Alors quelques-uns des scribes et des pharisiens prirent la parole et dirent: « Maître, nous voulons voir un signe de ta part. »
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
Mais il leur répondit: « Une génération méchante et adultère cherche un signe; mais il ne lui sera donné d'autre signe que celui du prophète Jonas.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
Car, de même que Jonas a passé trois jours et trois nuits dans le ventre d'un énorme poisson, de même le Fils de l'homme passera trois jours et trois nuits au cœur de la terre.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
Les hommes de Ninive se lèveront en jugement avec cette génération et la condamneront, car ils se sont repentis à la prédication de Jonas; et voici que quelqu'un de plus grand que Jonas est là.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
La reine du Midi se lèvera au moment du jugement de cette génération et la condamnera, car elle est venue des extrémités de la terre pour entendre la sagesse de Salomon; et voici qu'il y a ici quelqu'un de plus grand que Salomon.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
« Lorsqu'un esprit impur est sorti d'un homme, il passe par des lieux sans eau, cherchant le repos, et il ne le trouve pas.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Il dit alors: « Je vais retourner dans ma maison d'où je suis sorti »; et quand il est revenu, il la trouve vide, balayée et rangée.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Alors il va et prend avec lui sept autres esprits plus mauvais que lui, et ils y entrent et y demeurent. Le dernier état de cet homme devient pire que le premier. Il en sera de même pour cette génération mauvaise. »
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
Comme il parlait encore à la foule, voici que sa mère et ses frères se tenaient dehors, cherchant à lui parler.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
Quelqu'un lui dit: « Voici ta mère et tes frères qui sont dehors et qui cherchent à te parler. »
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
Mais il répondit à celui qui lui parlait: « Qui est ma mère? Qui sont mes frères? »
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
Il étendit la main vers ses disciples, et dit: « Voici ma mère et mes frères!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
Car quiconque fait la volonté de mon Père qui est dans les cieux, celui-là est mon frère, et ma sœur, et ma mère. »

< Mathayo 12 >