< Mathayo 12 >
1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
At that time Jesus went on the sabbath through the grain-fields; and his disciples were hungry, and began to pluck the ears of grain, and to eat.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
But the Pharisees, seeing it, said to him, Lo! thy disciples are doing that which it is not lawful to do on the sabbath.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
But he said to them, Have ye not read what David did, when he and those who were with him were hungry?
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
how he went into the house of God, and they ate the show-bread, which it was not lawful for him to eat, nor for those who were with him, but for the priests alone?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Or have ye not read in the Law, that on the sabbaths the priests in the temple profane the sabbath, and are blameless?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
But I say to you, that something greater than the temple is here.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
But if ye had known what this meaneth, “I desire mercy and not sacrifice,” ye would not have condemned the guiltless.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
For the Son of man is lord of the sabbath.
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
And departing thence, he went into their synagogue.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
And, lo! there was a man having a withered hand. And they asked him, saying, Is it lawful to heal on the sabbath? that they might accuse him.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
And he said to them, Who of you that owneth one sheep, if it fall into a pit on the sabbath, will not lay hold of it, and lift it out?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
Of how much more worth now is a man than a sheep! So then it is lawful to do well on the sabbath.
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Then saith he to the man, Stretch forth thy hand. And he stretched it forth; and it was restored sound as the other.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
Then the Pharisees went out, and consulted together against him, how they might destroy him.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
But Jesus, knowing it, withdrew from thence; and many followed him; and he healed them all,
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
and strictly charged them not to make him known;
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
that it might be fulfilled which was spoken through Isaiah the prophet, saying,
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
“Behold my servant, whom I chose; my beloved, with whom my soul is well pleased; I will put my Spirit upon him, and he will declare judgment to the nations.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
He will not strive, nor cry aloud, nor will any one hear his voice in the streets.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
A bruised reed he will not break, and smoking flax he will not quench, till he send forth judgment unto victory.
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
And in his name will nations hope.”
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Then was brought to him one possessed by a demon, blind and dumb; and he healed him, so that the dumb man spoke and saw.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
And all the multitudes were amazed, and said, Is this the son of David?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
But the Pharisees, hearing it, said, This man doth not cast out the demons, except through Beelzebul, the prince of the demons.
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
And he, knowing their thoughts, said to them, Every kingdom divided against itself is brought to desolation; and no city or house divided against itself will stand.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
And if Satan cast out Satan, he is divided against himself; how then shall his kingdom stand?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
And if I cast out the demons through Beelzebul, through whom do your sons cast them out? Therefore shall they be judges of you.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
But if I cast out the demons through the Spirit of God, then hath the kingdom of God already come to you.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Or how can one enter into a strong man's house, and seize upon his goods, unless he first bind the strong man, and then plunder his house?
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
He that is not with me is against me; and he that gathereth not with me scattereth abroad.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Therefore I say to you, All manner of sin and evil-speaking will be forgiven to men; but blasphemy against the Spirit will not be forgiven.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn )
And whoever speaketh a word against the Son of man, it will be forgiven him; but whoever speaketh against the Holy Spirit, it will not be forgiven him, either in this world, or in the world to come. (aiōn )
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Either say that the tree is good, and its fruit good; or say that the tree is bad, and its fruit bad; for the tree is known by its fruit. Brood of vipers!
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
How can ye, evil as ye are, speak good things? For out of the abundance of the heart the mouth speaketh.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
The good man, from his good treasure, bringeth out good things; and the evil man, from his evil treasure, bringeth out evil things.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
And I say to you, that for every idle word that men shall speak, they will give account in the day of judgment.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
For by thy words thou wilt be justified, and by thy words thou wilt be condemned.
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then some of the scribes and Pharisees answered him, saying, Teacher, we wish to see a sign from thee.
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
But he answered and said to them, A wicked and adulterous generation is seeking for a sign; and no sign will be given to it, but the sign of Jonah the prophet.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
For as Jonah was three days and three nights in the belly of the great fish, so will the Son of man be three days and three nights in the heart of the earth.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
The men of Nineveh will stand up in the judgment with this generation, and will condemn it; for they repented at the preaching of Jonah; and, lo! something more than Jonah is here.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
The queen of the south will rise up in the judgment with this generation, and will condemn it; for she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon; and lo! something more than Solomon is here.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
But when the unclean spirit is gone out from a man, it goeth through dry places, seeking rest, and findeth it not.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Then it saith, I will return to my house whence I came out. And on coming, it findeth it empty, and swept, and put in order.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Then it goeth and taketh with it seven other spirits more wicked than itself, and they enter in, and dwell there; and the last state of that man becometh worse than the first. So will it be also with this wicked generation.
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
While he was yet speaking to the multitudes, lo! his mother and his brothers were standing without, seeking to speak with him.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
And one said to him, Behold, thy mother and thy brothers are standing without, seeking to speak with thee.
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
But he answered and said to him that told him, Who is my mother, and who are my brothers?
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
And stretching forth his hand toward his disciples, be said, Behold, my mother and my brothers!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
For whoever doeth the will of my Father who is in heaven, he is my brother, and sister, and mother.