< Mathayo 12 >

1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
At that time Jesus went on the Sabbaths through the grainfields, and His disciples were hungry, and they began to pluck ears, and to eat,
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
and the Pharisees having seen, said to Him, “Behold, Your disciples do that which it is not lawful to do on a Sabbath.”
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
And He said to them, “Did you not read what David did when he was hungry, himself and those with him—
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
how he went into the house of God, and ate the Bread of the Presentation, which it is not lawful to him to eat, nor to those with him, except to the priests alone?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Or did you not read in the Law that on the Sabbaths the priests in the temple profane the Sabbath and are blameless?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
And I say to you that [One] greater than the temple is here;
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
and if you had known what [this] is: Kindness I will, and not sacrifice—you had not condemned the blameless,
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
for the Son of Man is Lord even of the Sabbath.”
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
And having departed from there, He went to their synagogue,
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
and behold, there was a man having the hand withered, and they questioned Him, saying, “Is it lawful to heal on the Sabbaths?” That they might accuse Him.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
And He said to them, “What man will be of you who will have one sheep, and if this may fall on the Sabbaths into a ditch, will not lay hold on it and raise [it]?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
How much better, therefore, is a man than a sheep? So that it is lawful on the Sabbaths to do good.”
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Then He says to the man, “Stretch forth your hand,” and he stretched [it] forth, and it was restored whole as the other.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
And the Pharisees having gone forth, held a consultation against Him, how they might destroy Him,
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
and Jesus having known, withdrew from there, and there followed Him great multitudes, and He healed them all,
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
and charged them that they might not make Him apparent,
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
that it might be fulfilled that was spoken through Isaiah the prophet, saying,
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
“Behold, My Servant, whom I chose, My Beloved, in whom My soul delighted, I will put My Spirit on Him, And He will declare judgment to the nations;
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
He will not strive nor cry, Nor will any hear His voice in the broad places;
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
A bruised reed He will not break, And smoking flax He will not quench, Until He may put forth judgment to victory,
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
And in His Name will nations hope.”
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Then was brought to Him a demoniac, blind and mute, and He healed him, so that the blind and mute both spoke and saw.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
And all the multitudes were amazed and said, “Is this the Son of David?”
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
But the Pharisees having heard, said, “This One does not cast out demons, except by Beelzebul, ruler of the demons.”
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
And Jesus, knowing their thoughts, said to them, “Every kingdom having been divided against itself is desolated, and no city or house having been divided against itself stands,
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
and if Satan casts out Satan, against himself he was divided, how then does his kingdom stand?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
And if I, by Beelzebul, cast out the demons, your sons—by whom do they cast out? Because of this they will be your judges.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
But if I, by the Spirit of God, cast out the demons, then the Kingdom of God has already come to you.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Or how is one able to go into the house of the strong man, and to snatch his goods, if first he may not bind the strong man? And then his house he will plunder.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
He who is not with Me is against Me, and he who is not gathering with Me, scatters.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Because of this I say to you, all sin and slander will be forgiven to men, but the slander of the Spirit will not be forgiven to men.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
And whoever may speak a word against the Son of Man it will be forgiven to him, but whoever may speak against the Holy Spirit, it will not be forgiven him, neither in this age, nor in that which is coming. (aiōn g165)
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Either make the tree good, and its fruit good, or make the tree bad, and its fruit bad, for from the fruit is the tree known.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
Brood of vipers! How are you able to speak good things—being evil? For out of the abundance of the heart the mouth speaks.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
The good man out of the good treasure of the heart puts forth the good things, and the evil man out of the evil treasure puts forth evil things.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
And I say to you that every idle word that men may speak, they will give for it a reckoning in [the] day of judgment;
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
for from your words you will be declared righteous, and from your words you will be declared unrighteous.”
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then certain of the scribes and Pharisees answered, saying, “Teacher, we will to see a sign from You.”
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
And He answering said to them, “A generation, evil and adulterous, seeks a sign, and a sign will not be given to it, except the sign of Jonah the prophet;
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
for as Jonah was in the belly of the fish three days and three nights, so will the Son of Man be in the heart of the earth three days and three nights.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
Men of Nineveh will stand up in the judgment with this generation, and will condemn it, for they converted at the proclamation of Jonah, and behold, [One] greater than Jonah [is] here!
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
A queen of the south will rise up in the judgment with this generation, and will condemn it, for she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon, and behold, [One] greater than Solomon [is] here!
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
And when the unclean spirit may go forth from the man, it walks through dry places seeking rest and does not find;
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
then it says, I will return to my house from where I came forth; and having come, it finds [it] unoccupied, swept, and adorned:
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
then it goes, and takes with itself seven other spirits more evil than itself, and having gone in they dwell there, and the last of that man becomes worse than the first; so will it also be to this evil generation.”
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
And while He was yet speaking to the multitudes, behold, His mother and brothers had stood outside, seeking to speak to Him,
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
and one said to Him, “Behold, Your mother and Your brothers stand outside, seeking to speak to You.”
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
And He answering said to him who spoke to Him, “Who is My mother? And who are My brothers?”
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
And having stretched forth His hand toward His disciples, He said, “Behold, My mother and My brothers!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
For whoever may do the will of My Father who is in the heavens, He is My brother, and sister, and mother.”

< Mathayo 12 >