< Mathayo 12 >
1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
At that time Jesus went through the corn on the sabbath: and his disciples being hungry, began to pluck the ears, and to eat.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
And the Pharisees seeing them, said to him: Behold thy disciples do that which is not lawful to do on the sabbath days.
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
But he said to them: Have you not read what David did when he was hungry, and they that were with him:
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
How he entered into the house of God, and did eat the loaves of proposition, which it was not lawful for him to eat, nor for them that were with him, but for the priests only?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Or have ye not read in the law, that on the sabbath days the priests in the temple break the sabbath, and are without blame?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
But I tell you that there is here a greater than the temple.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
And if you knew what this meaneth: I will have mercy, and not sacrifice: you would never have condemned the innocent.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
For the Son of man is Lord even of the sabbath.
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
And when he has passed from thence, he came into their synagogues.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
And behold there was a man who had a withered hand, and they asked him, saying: Is it lawful to heal on the sabbath days? that they might accuse him.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
But he said to them: What man shall there be among you, that hath one sheep: and if the same fall into a pit on the sabbath day, will he not take hold on it and lift it up?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
How much better is a man than a sheep? Therefore it is lawful to do a good deed on the sabbath days.
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Then he saith to the man: Stretch forth thy hand; and he stretched it forth, and it was restored to health even as the other.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
And the Pharisees going out made a consultation against him, how they might destroy him.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
But Jesus knowing it, retired from thence: and many followed him, and he healed them all.
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
And he charged them that they should not make him known.
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
That it might be fulfilled which was spoken by Isaias the prophet, saying:
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
Behold my servant whom I have chosen, my beloved in whom my soul hath been well pleased. I will put my spirit upon him, and he shall shew judgment to the Gentiles.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
He shall not contend, nor cry out, neither shall any man hear his voice in the streets.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
The bruised reed he shall not break: and smoking flax he shall not extinguish: till he send forth judgment unto victory.
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
And in his name the Gentiles shall hope.
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Then was offered to him one possessed with a devil, blind and dumb: and he healed him, so that he spoke and saw.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
And all the multitudes were amazed, and said: Is not this the son of David?
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
But the Pharisees hearing it, said: This man casteth not out the devils but by Beelzebub the prince of the devils.
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
And Jesus knowing their thoughts, said to them: Every kingdom divided against itself shall be made desolate: and every city or house divided against itself shall not stand.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
And if Satan cast out Satan, he is divided against himself: how then shall his kingdom stand?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
And if I by Beelzebub cast out devils, by whom do your children cast them out? Therefore they shall be your judges.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
But if I by the Spirit of God cast out devils, then is the kingdom of God come upon you.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Or how can any one enter into the house of the strong, and rifle his goods, unless he first bind the strong? and then he will rifle his house.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
He that is not with me, is against me: and he that gathereth not with me, scattereth.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Therefore I say to you: Every sin and blasphemy shall be forgiven men, but the blasphemy of the Spirit shall not be forgiven.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn )
And whosoever shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him: but he that shall speak against the Holy Ghost, it shall not be forgiven him, neither in this world, nor in the world to come. (aiōn )
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Either make the tree good and its fruit good: or make the tree evil, and its fruit evil. For by the fruit the tree is known.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
O generation of vipers, how can you speak good things, whereas you are evil? for out of the abundance of the heart the mouth speaketh.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
A good man out of a good treasure bringeth forth good things: and an evil man out of an evil treasure bringeth forth evil things.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
But I say unto you, that every idle word that men shall speak, they shall render an account for it in the day of judgment.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
For by thy words thou shalt be justified, and by thy words thou shalt be condemned.
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then some of the scribes and Pharisees answered him, saying: Master we would see a sign from thee.
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
Who answering said to them: An evil and adulterous generation seeketh a sign: and a sign shall not be given it, but the sign of Jonas the prophet.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
For as Jonas was in the whale’s belly three days and three nights: so shall the Son of man be in the heart of the earth three days and three nights.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
The men of Ninive shall rise in judgment with this generation, and shall condemn it: because they did penance at the preaching of Jonas. And behold a greater than Jonas here.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
The queen of the south shall rise in judgment with this generation, and shall condemn it: because she came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon, and behold a greater than Solomon here.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
And when an unclean spirit is gone out of a man he walketh through dry places seeking rest, and findeth none.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Then he saith: I will return into my house from whence I came out. And coming he findeth it empty, swept, and garnished.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Then he goeth, and taketh with him seven other spirits more wicked than himself, and they enter in and dwell there: and the last state of that man is made worse than the first. So shall it be also to this wicked generation.
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
As he was yet speaking to the multitudes, behold his mother and his brethren stood without, seeking to speak to him.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
And one said unto him: Behold thy mother and thy brethren stand without, seeking thee.
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
But he answering him that told him, said: Who is my mother, and who are my brethren?
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
And stretching forth his hand towards his disciples, he said: Behold my mother and my brethren.
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
For whosoever shall do the will of my Father, that is in heaven, he is my brother, and sister, and mother.