< Mathayo 12 >

1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
Paa den Tid vandrede Jesus paa Sabbaten igennem en Sædemark; men hans Disciple bleve hungrige og begyndte at plukke Aks og at spise.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
Men da Farisæerne saa det, sagde de til ham: „Se, dine Disciple gøre, hvad det ikke er tilladt at gøre paa en Sabbat.”
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
Men han sagde til dem: „Have I ikke læst, hvad David gjorde, da han blev hungrig og de, som vare med ham?
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
hvorledes han gik ind i Guds Hus og spiste Skuebrødene, som det ikke var ham tilladt at spise, ej heller dem, som vare med ham, men alene Præsterne?
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Eller have I ikke læst i Loven, at paa Sabbaterne vanhellige Præsterne Sabbaten i Helligdommen og ere dog uden Skyld?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
Men jeg siger eder, at her er det, som er større end Helligdommen.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
Men dersom I havde vidst, hvad det Ord betyder: Jeg har Lyst til Barmhjertighed og ikke til Offer, da havde I ikke fordømt dem, som ere uden Skyld.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
Thi Menneskesønnen er Herre over Sabbaten.”
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
Og han gik videre derfra og kom ind i deres Synagoge.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
Og se, der var en Mand, som havde en vissen Haand; og de spurgte ham ad og sagde: „Er det tilladt at helbrede paa Sabbaten?” for at de kunde anklage ham.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
Men han sagde til dem: „Hvilket Menneske er der iblandt eder, som har kun eet Faar, og ikke tager fat paa det og drager det op, dersom det paa Sabbaten falder i en Grav?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
Hvor meget er nu ikke et Menneske mere end et Faar? Altsaa er det tilladt at gøre vel paa Sabbaten.”
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Da siger han til Manden: „Ræk din Haand ud!” og han rakte den ud, og den blev igen sund som den anden.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
Men Farisæerne gik ud og lagde Raad op imod ham, hvorledes de kunde slaa ham ihjel.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
Men da Jesus mærkede det, drog han bort derfra; og mange fulgte ham, og han helbredte dem alle.
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
Og han bød dem strengt, at de ikke maatte gøre ham kendt;
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
for at det skulde opfyldes, som er talt ved Profeten Esajas, som siger:
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
„Se, min Tjener, som jeg har udvalgt, min elskede, i hvem min Sjæl har Velbehag; jeg vil give min Aand over ham, og han skal forkynde Hedningerne Ret.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
Han skal ikke kives og ikke raabe, og ingen skal høre hans Røst paa Gaderne.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
Han skal ikke sønderbryde det knækkede Rør og ikke udslukke den rygende Tande, indtil han faar ført Retten frem til Sejr.
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
Og paa hans Navn skulle Hedninger haabe.”
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Da blev en besat, som var blind og stum, ført til ham; og han helbredte ham, saa at den stumme talte og saa.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
Og alle Skarerne forfærdedes og sagde: „Mon denne skulde være Davids Søn?”
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
Men da Farisæerne hørte det, sagde de: „Denne uddriver ikke de onde Aander uden ved Beelzebul, de onde Aanders Fyrste.”
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
Men saasom han kendte deres Tanker, sagde han til dem: „Hvert Rige, som er kommet i Splid med sig selv, lægges øde; og hver By eller Hus, som er kommet i Splid med sig selv, kan ikke bestaa.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
Og hvis Satan uddriver Satan, saa er han kommen i Splid med sig selv; hvorledes skal da hans Rige bestaa?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
Og dersom jeg uddriver de onde Aander ved Beelzebul, ved hvem uddrive da eders Sønner dem? Derfor skulle de være eders Dommere.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
Men dersom jeg uddriver de onde Aander ved Guds Aand, da er jo Guds Rige kommet til eder.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
Eller hvorledes kan nogen gaa ind i den stærkes Hus og røve hans Ejendele, uden han først binder den stærke? Da kan han plyndre hans Hus.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
Den, som ikke er med mig, er imod mig; og den, som ikke samler med mig, adspreder.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Derfor siger jeg eder: Al Synd og Bespottelse skal forlades Menneskene, men Bespottelsen imod Aanden skal ikke forlades.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
Og den, som taler et Ord imod Menneskesønnen, ham skal det forlades; men den, som taler imod den Helligaand, ham skal det ikke forlades, hverken i denne Verden eller i den kommende. (aiōn g165)
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Lader enten Træet være godt og dets Frugt god; eller lader Træet være raaddent, og dets Frugt raadden; thi Træet kendes paa Frugten.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
I Øgleunger! hvorledes kunne I tale godt, naar I ere onde? Thi af Hjertets Overflødighed taler Munden.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
Et godt Menneske fremtager gode Ting af sit gode Forraad; og et ondt Menneske fremtager onde Ting af sit onde Forraad.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
Men jeg siger eder, at Menneskene skulle gøre Regnskab paa Dommens Dag for hvert utilbørligt Ord, som de tale.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
Thi af dine Ord skal du retfærdiggøres, og af dine Ord skal du fordømmes.”
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Da svarede nogle af de skriftkloge og Farisæerne ham og sagde: „Mester! vi ønske at se et Tegn af dig.”
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
Men han svarede og sagde til dem: „En ond og utro Slægt forlanger Tegn, men der skal intet Tegn gives den uden Profeten Jonas's Tegn.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
Thi ligesom Jonas var tre Dage og tre Nætter i Havdyrets Bug, saaledes skal Menneskesønnen være tre Dage og tre Nætter i Jordens Skød.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
Mænd fra Ninive skulle opstaa ved Dommen sammen med denne Slægt og fordømme den; thi de omvendte sig ved Jonas's Prædiken; og se, her er mere end Jonas.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
Sydens Dronning skal oprejses ved Dommen sammen med denne Slægt og fordømme den; thi hun kom fra Jordens Grænser for at høre Salomons Visdom; og se, her er mere end Salomon.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
Men naar den urene Aand er faren ud af Mennesket, vandrer den igennem vandløse Steder, søger Hvile og finder den ikke.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Da siger den: Jeg vil vende om til mit Hus, som jeg gik ud af; og naar den kommer, finder den det ledigt, fejet og prydet.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Saa gaar den hen og tager syv andre Aander med sig, som ere værre end den selv, og naar de ere komne derind, bo de der; og det sidste bliver værre med dette Menneske end det første. Saaledes skal det ogsaa gaa denne onde Slægt.”
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
Medens han endnu talte til Skarerne, se, da stode hans Moder og hans Brødre udenfor og begærede at tale med ham.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
Da sagde en til ham: „Se, din Moder og dine Brødre staa udenfor og begære at tale med dig.”
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
Men han svarede og sagde til den, som sagde ham det: „Hvem er min Moder? og hvem ere mine Brødre?”
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
Og han rakte sin Haand ud over sine Disciple og sagde: „Se, her er min Moder og mine Brødre!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
Thi enhver, der gør min Faders Villie, som er i Himlene, han er min Broder og Søster og Moder.”

< Mathayo 12 >