< Mathayo 11 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
Kiedy Jezus skończył rozkazywać swoim dwunastu uczniom, odszedł stamtąd, aby nauczać i głosić w ich miastach.
2 Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
A gdy Jan usłyszał w więzieniu o czynach Chrystusa, posłał dwóch ze swoich uczniów;
3 ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
Z pytaniem: Czy ty jesteś tym, który ma przyjść, czy mamy oczekiwać innego?
4 Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
A Jezus odpowiedział im: Idźcie i oznajmijcie Janowi, co słyszycie i widzicie.
5 Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
Ślepi widzą, chromi chodzą, trędowaci zostają oczyszczeni, głusi słyszą, umarli zmartwychwstają, a ubogim opowiadana jest ewangelia.
6 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
A błogosławiony jest ten, kto się nie zgorszy z mojego powodu.
7 Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
A gdy odeszli, Jezus zaczął mówić do tłumów o Janie: Co wyszliście oglądać na pustyni? Trzcinę kołyszącą się na wietrze?
8 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
Ale co wyszliście zobaczyć? Człowieka ubranego w miękkie szaty? Oto ci, którzy noszą miękkie szaty, są w domach królewskich.
9 Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
Ale co wyszliście zobaczyć? Proroka? Owszem, mówię wam, nawet więcej niż proroka.
10 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
Bo on jest tym, o którym jest napisane: Oto ja posyłam mego posłańca przed twoim obliczem, który przygotuje twoją drogę przed tobą.
11 Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
Zaprawdę powiadam wam: Nie powstał z tych, którzy rodzą się z kobiet, większy od Jana Chrzciciela. Ale ten, kto jest najmniejszy w królestwie niebieskim, jest większy niż on.
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
A od dni Jana Chrzciciela aż dotąd królestwo niebieskie doznaje gwałtu i gwałtownicy je zdobywają.
13 Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
Bo wszyscy Prorocy i Prawo prorokowali aż do Jana.
14 Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
A jeśli chcecie [to] przyjąć, on jest Eliaszem, który miał przyjść.
15 Yeye aliye na masikio, na asikie.
Kto ma uszy do słuchania, niech słucha.
16 “Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
Ale do kogo przyrównam to pokolenie? Podobne jest do dzieci, które siedzą na rynku i wołają na swoich towarzyszy:
17 “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
Graliśmy wam na flecie, a nie tańczyliście; śpiewaliśmy pieśni żałobne, a nie płakaliście.
18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
Przyszedł bowiem Jan, nie jadł i nie pił, a mówią: Ma demona.
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
Przyszedł Syn Człowieczy, jedząc i pijąc, a mówią: Oto żarłok i pijak, przyjaciel celników i grzeszników. Lecz usprawiedliwiona jest mądrość przez swoje dzieci.
20 Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
Wtedy zaczął ganić miasta, w których działo się najwięcej jego cudów, że nie pokutowały, [mówiąc]:
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
Biada tobie, Korozain! Biada tobie, Betsaido! Bo gdyby w Tyrze i Sydonie działy się te cuda, które się w was dokonały, dawno by w worze i popiele pokutowały.
22 Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
Ale mówię wam: Lżej będzie Tyrowi i Sydonowi w dniu sądu niż wam.
23 Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs )
A ty, Kafarnaum, które jesteś wywyższone aż do nieba, aż do piekła będziesz strącone. Bo gdyby w Sodomie działy się cuda, które się w tobie dokonały, przetrwałaby aż do dziś. (Hadēs )
24 Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
Ale mówię wam: Lżej będzie ziemi Sodomy w dzień sądu niż tobie.
25 Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
W tym czasie Jezus powiedział: Wysławiam cię, Ojcze, Panie nieba i ziemi, że zakryłeś te sprawy przed mądrymi i roztropnymi, a objawiłeś je niemowlętom.
26 Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
Tak, Ojcze, gdyż tak się tobie upodobało.
27 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
Wszystko zostało mi dane od mego Ojca i nikt nie zna Syna, tylko Ojciec, ani nikt nie zna Ojca, tylko Syn i ten, komu Syn zechce objawić.
28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Przyjdźcie do mnie wszyscy, którzy jesteście spracowani i obciążeni, a ja wam dam odpoczynek.
29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Weźcie na siebie moje jarzmo i uczcie się ode mnie, że jestem cichy i pokornego serca, a znajdziecie odpoczynek dla waszych dusz.
30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
Moje jarzmo bowiem jest przyjemne, a moje brzemię lekkie.