< Mathayo 11 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
And it came to pass, when Jesus had made an end of commanding his twelve disciples, he departed there to teach and to preach in their cities.
2 Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
Now when John had heard in the prison the works of Christ, he sent two of his disciples,
3 ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
And said to him, Are you he that should come, or do we look for another?
4 Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
Jesus answered and said to them, Go and show John again those things which you do hear and see:
5 Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
The blind receive their sight, and the lame walk, the lepers are cleansed, and the deaf hear, the dead are raised up, and the poor have the gospel preached to them.
6 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
And blessed is he, whoever shall not be offended in me.
7 Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
And as they departed, Jesus began to say to the multitudes concerning John, What went you out into the wilderness to see? A reed shaken with the wind?
8 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
But what went you out for to see? A man clothed in soft raiment? behold, they that wear soft clothing are in kings’ houses.
9 Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
But what went you out for to see? A prophet? yes, I say to you, and more than a prophet.
10 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
For this is he, of whom it is written, Behold, I send my messenger before your face, which shall prepare your way before you.
11 Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
Truly I say to you, Among them that are born of women there has not risen a greater than John the Baptist: notwithstanding he that is least in the kingdom of heaven is greater than he.
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
And from the days of John the Baptist until now the kingdom of heaven suffers violence, and the violent take it by force.
13 Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
For all the prophets and the law prophesied until John.
14 Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
And if you will receive it, this is Elias, which was for to come.
15 Yeye aliye na masikio, na asikie.
He that has ears to hear, let him hear.
16 “Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
But to what shall I liken this generation? It is like to children sitting in the markets, and calling to their fellows,
17 “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
And saying, We have piped to you, and you have not danced; we have mourned to you, and you have not lamented.
18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
For John came neither eating nor drinking, and they say, He has a devil.
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
The Son of man came eating and drinking, and they say, Behold a man gluttonous, and a drunkard, a friend of publicans and sinners. But wisdom is justified of her children.
20 Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
Then began he to upbraid the cities wherein most of his mighty works were done, because they repented not:
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
Woe to you, Chorazin! woe to you, Bethsaida! for if the mighty works, which were done in you, had been done in Tyre and Sidon, they would have repented long ago in sackcloth and ashes.
22 Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
But I say to you, It shall be more tolerable for Tyre and Sidon at the day of judgment, than for you.
23 Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs g86)
And you, Capernaum, which are exalted to heaven, shall be brought down to hell: for if the mighty works, which have been done in you, had been done in Sodom, it would have remained until this day. (Hadēs g86)
24 Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
But I say to you, That it shall be more tolerable for the land of Sodom in the day of judgment, than for you.
25 Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
At that time Jesus answered and said, I thank you, O Father, Lord of heaven and earth, because you have hid these things from the wise and prudent, and have revealed them to babes.
26 Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
Even so, Father: for so it seemed good in your sight.
27 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
All things are delivered to me of my Father: and no man knows the Son, but the Father; neither knows any man the Father, save the Son, and he to whomsoever the Son will reveal him.
28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Come to me, all you that labor and are heavy laden, and I will give you rest.
29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Take my yoke on you, and learn of me; for I am meek and lowly in heart: and you shall find rest to your souls.
30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
For my yoke is easy, and my burden is light.

< Mathayo 11 >