< Mathayo 11 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
And it came to pass, when Jesus finished teaching His twelve disciples, He departed thence to teach and to preach in their cities.
2 Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
And John hearing in the prison the works of Christ, sending two of his disciples,
3 ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
said to Him, Art thou He who is coming, or must we expect another?
4 Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
Jesus responding said to them, Having gone, proclaim unto John the things which you hear and see.
5 Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
The blind are looking up, and the lame are walking about, the lepers are being cleansed, and the deaf are hearing, the dead are being raised, and the poor are having the gospel preached unto them:
6 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
and blessed is he, whosoever may not be offended in me.
7 Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
And they departing, Jesus began to speak to the multitudes concerning John, What went you out in the wilderness to see? a reed shaken by the wind?
8 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
But what went you out to see? a man clothed in soft raiment? Behold those wearing soft raiment are in the houses of the kings.
9 Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
But what went you out to see? a prophet? Yea, I say unto you, and more than a prophet:
10 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
for this is he, concerning whom it has been written, Behold, I send my messenger before my face, who will prepare thy way before thee.
11 Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
Truly I say unto you, Among those having been born of women there has not risen a greater than John the Baptist: nevertheless the least in the kingdom of the heavens is greater than he.
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
From the days of John the Baptist until now the kingdom of the heavens suffers violence, and the violent are taking it by force.
13 Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
For all the prophets and the law prophesied till John.
14 Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
And if you wish to receive it, he is Elijah, who is to come.
15 Yeye aliye na masikio, na asikie.
Let the one having ears to hear, hear.
16 “Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
But to whom shall I liken this generation? It is like little children sitting in the market-place, and calling to their comrades, and saying,
17 “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
We piped unto you, and you did not dance; we mourned unto you, and you did not lament.
18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
For John came neither eating nor drinking, and they say, He has a demon.
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
The Son of man came eating and drinking, and they say, Behold, a gluttonous and wine-drinking man, a friend of publicans and sinners. Wisdom is truly justified by her children.
20 Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
Then He began to upbraid the cities in which the most mighty works of His were performed, because they did not repent.
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
Woe unto thee, Chorazin! Woe unto thee, Bethsaida! because if the mighty works which were wrought in you had been in Tyre and Sidon, they would have repented long ago in sackcloth and ashes.
22 Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
Moreover I say unto you, it will be more tolerable for Tyre and Sidon in the day of judgment than for you.
23 Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs )
And thou, Capernaum, art thou not exalted up to heaven? thou shall be cast down to Hades: because if the mighty works which were wrought in thee had been performed in Sodom, it would have remained until this day. (Hadēs )
24 Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
Moreover I say unto you, that it shall be more tolerable for the land of Sodom in the day of judgment, than for thee.
25 Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
At that time Jesus responding said, I praise thee, O Father, Lord of heaven and of earth, because thou hast hidden these things from the wise and the prudent, and reveal them unto babes.
26 Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
Yea, Father, because it was so well pleasing in thy sight.
27 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
All things were delivered unto me by my Father: and no one perfectly knows the Son, except the Father; neither does any one perfectly know the Father, except the Son; and he to whom the Son may wish to reveal Him.
28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Come unto me, all ye who labor and are heavy laden, and I will give you rest.
29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
Take my yoke upon you, and learn of me; because I am meek and lowly in heart: and you shall find rest unto your souls.
30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
For my yoke is easy and my burden is light.