< Mathayo 11 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo kwa wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.
耶稣吩咐完十二门徒后就离开了,到附近各城教导传道。
2 Yohana aliposikia akiwa gerezani mambo ambayo Kristo alikuwa akiyafanya, aliwatuma wanafunzi wake
约翰被关在监牢中时,听到基督所做之事,便派他的门徒
3 ili wakamuulize, “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee mwingine?”
以他的名义去询问耶稣:“你是我们期盼到来之人吗?还是我们必须继续寻找其他人?”
4 Yesu akajibu, “Rudini mkamwambie Yohana yale mnayosikia na kuyaona:
耶稣回答:“你们回去吧,把听见和看见的都告诉约翰,
5 Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
盲者可见,瘸者可行,麻风患者治愈,聋者可以听见,亡者复活,贫苦者听到福音。
6 Amebarikiwa mtu yule asiyechukizwa na mimi.”
不拒绝我者,必被祝福。”
7 Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa wanaondoka, Yesu akaanza kusema na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji. Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani, mlikwenda kuona nini? Je, ni unyasi ukipeperushwa na upepo?
他们继续前行,耶稣对众人讲起约翰。他说:“在荒野中时,你会期待什么?被风吹动的芦苇吗?
8 Kama sivyo, mlikwenda kuona nini basi? Mtu aliyevaa mavazi ya kifahari? La hasha, watu wanaovaa mavazi ya kifahari wako katika majumba ya wafalme.
你们到底想要看什么?身穿华服之人吗?衣着就像王宫中居住的人一样吗?
9 Basi mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii.
那么,你们到那里想要看什么?先知吗?是的,但我要告诉你,他不只是一名先知。
10 Huyu ndiye ambaye habari zake zimeandikwa: “‘Tazama nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako.’
他便是经文中所写那人:‘我差遣使者到你前面,为你备好你的道路。’
11 Amin, nawaambia, miongoni mwa wale waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni ni mkuu kuliko Yohana.
告诉你们实话,在人类世界中,任何人都不如施洗者约翰伟大,但在天国中,他却是最微不足道的那一个。
12 Tangu siku za Yohana Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wanauteka.
从施洗约翰之时到现在,天国不断遭受猛烈攻击,暴徒企图以武力将其占为己有。
13 Kwa maana manabii wote na Sheria walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
因为在约翰到来之前,所有的先知和律法都在讲述上帝之道。
14 Ikiwa mko tayari kukubali hilo, yeye ndiye yule Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema angekuja.
如果你们准备好相信,那么约翰就是你们应该期待的以利亚。
15 Yeye aliye na masikio, na asikie.
如果你有耳朵,就要去听。
16 “Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini? Kinafanana na watoto waliokaa sokoni wakiwaita wenzao na kuwaambia,
我该把这代人比作什么?它就像小孩子坐在市场中,喊着彼此的名字说:
17 “‘Tuliwapigia filimbi, lakini hamkucheza; tuliwaimbia nyimbo za maombolezo, lakini hamkuomboleza.’
‘我们给你们吹笛子,你们却不跳舞,我们唱哀歌,你们也不哭泣。’
18 Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja, alikuwa hali wala hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo mchafu.’
约翰前来,禁食禁水,人们说‘他是鬼附体!’
19 Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, nao wanasema, ‘Tazameni huyu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na “wenye dhambi.”’ Lakini hekima huthibitishwa kuwa kweli kwa matendo yake.”
然后人子来了,禁食禁水,人们却说:‘你看,这人贪食好酒,与税吏和罪人为友。’但通过他的行为,显示出智慧即为正道。”
20 Ndipo Yesu akaanza kushutumu miji ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu.
随后,耶稣开始批判他曾行过大多数上帝神迹的城,因为那里的人不肯悔改。
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingefanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa imetubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.
“哥拉逊啊,你应感到羞愧!伯赛大啊,你应感到羞愧!在你们那里所行上帝神迹,如果出现在推罗和西顿,城中之人早已披麻蒙灰,想要悔改。
22 Lakini nawaambia, itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili katika siku ya hukumu, kuliko ninyi.
但告诉你吧,在审判日那天,推罗和西顿的情况会比你们更好。
23 Nawe Kapernaumu, je, utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, utashushwa mpaka kuzimu. Miujiza iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma, mji huo ungalikuwepo hadi leo. (Hadēs )
至于迦百农,你们会升入天堂吗?不,你们必会跌入冥府。在你们那里行过的上帝神迹,如果行在索多玛,那座城还会存留到今天。 (Hadēs )
24 Lakini nakuambia kwamba, itakuwa rahisi zaidi kwa Sodoma kustahimili katika siku ya hukumu kuliko wewe.”
但我告诉你们,在审判日那天,索多那城所受的惩罚可比你们轻。”
25 Wakati huo Yesu alisema, “Nakuhimidi Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto wadogo.
然后耶稣祈祷:“天父啊,天地之主,我赞美你,因你向智慧和聪明之人隐藏了这一切,却向普罗大众显明。
26 Naam, Baba, kwa kuwa hivyo ndivyo ilivyokupendeza.
天父啊,是的,这样做让你欢喜。
27 “Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: Hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.
天父已将这一切交给我,只有天父理解其子,只有天父之子及其选择进行启示之人,才理解天父。
28 “Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
所有挣扎负重之人,到我这里来。我必让你们休息。
29 Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu.
接受我的轭,向我学习,我内心善良谦卑,从我这里你将获得需要的休息。
30 Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
我的轭很轻柔,我的负重很轻。”