< Marko 1 >

1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
beginning the/this/who gospel Jesus Christ son (the/this/who *ko*) God
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
(as/just as *N(k)O*) to write in/on/among (the/this/who Isaiah *NO*) (the/this/who *N(k)O*) (prophet *N(K)O*) look! (I/we *KO*) to send the/this/who angel: messenger me before face you which to prepare the/this/who road you (before you *K*)
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
voice/sound: voice to cry out in/on/among the/this/who deserted to make ready the/this/who road lord: God Straight to do/make: do the/this/who path it/s/he
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
to be John (the/this/who *no*) to baptize in/on/among the/this/who deserted and to preach baptism repentance toward forgiveness sin
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
and to depart to/with it/s/he all the/this/who Judea country and the/this/who Jerusalem all and to baptize by/under: by it/s/he in/on/among the/this/who Jordan river to agree the/this/who sin it/s/he
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
(and *no*) to be (then *k*) the/this/who John to put on hair camel and belt/sash/girdle made of leather about the/this/who loins it/s/he and to eat locust and honey wild
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
and to preach to say to come/go the/this/who strong me after me which no to be sufficient to stoop/bend down to loose the/this/who leather strap the/this/who sandal it/s/he
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
I/we (on the other hand *k*) to baptize you (in/on/among *ko*) water it/s/he then to baptize you in/on/among spirit/breath: spirit holy
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
and to be in/on/among that the/this/who day to come/go Jesus away from Nazareth the/this/who Galilee and to baptize toward the/this/who Jordan by/under: by John
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
and immediately to ascend (out from *N(k)O*) the/this/who water to perceive: see to split the/this/who heaven and the/this/who spirit/breath: spirit (as/when *N(k)O*) dove to come/go down (toward *N(k)O*) it/s/he
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
and voice/sound: voice to be out from the/this/who heaven you to be the/this/who son me the/this/who beloved in/on/among (you *N(K)O*) to delight
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
and immediately the/this/who spirit/breath: spirit it/s/he to expel toward the/this/who deserted
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
and to be (there *k*) in/on/among the/this/who deserted forty day to test/tempt: tempt by/under: by the/this/who Satan and to be with/after the/this/who wild animal and the/this/who angel to serve it/s/he
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
(and *o*) with/after then the/this/who to deliver the/this/who John to come/go the/this/who Jesus toward the/this/who Galilee to preach the/this/who gospel (the/this/who kingdom *K*) the/this/who God
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
and to say that/since: that to fulfill the/this/who time/right time and to come near the/this/who kingdom the/this/who God to repent and to trust (in) in/on/among the/this/who gospel
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
(and *no*) (to pass *N(k)O*) (then *k*) from/with/beside the/this/who sea the/this/who (Sea of) Galilee to perceive: see Simon and Andrew the/this/who brother (it/s/he *k*) (the/this/who *o*) (Simon *no*) (to cast *N(k)O*) (net *k*) in/on/among the/this/who sea to be for fisherman
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
and to say it/s/he the/this/who Jesus come after me and to do/make: do you to be fisherman a human
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
and immediately to release: leave the/this/who net (it/s/he *k*) to follow it/s/he
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
and to advance (from there *k*) little/few to perceive: see James the/this/who the/this/who Zebedee and John the/this/who brother it/s/he and it/s/he in/on/among the/this/who boat to complete the/this/who net
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
and immediately to call: call it/s/he and to release: leave the/this/who father it/s/he Zebedee in/on/among the/this/who boat with/after the/this/who hired worker to go away after it/s/he
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
and to enter toward Capernaum and immediately the/this/who Sabbath to enter toward the/this/who synagogue to teach
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
and be astonished upon/to/against the/this/who teaching it/s/he to be for to teach it/s/he as/when authority to have/be and no as/when the/this/who scribe
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
and (immediately *NO*) to be in/on/among the/this/who synagogue it/s/he a human in/on/among spirit/breath: spirit unclean and to yell
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
to say (ha!/aha! *K*) which? me and you Jesus Nazareth to come/go to destroy me to know you which? to be the/this/who holy the/this/who God
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
and to rebuke it/s/he the/this/who Jesus to say to muzzle and to go out out from it/s/he
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
and to convulse it/s/he the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who unclean and (to call *N(k)O*) voice/sound: voice great to go out out from it/s/he
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
and to astonish (all *N(k)O*) so to debate to/with (themself *N(k)O*) to say which? to be this/he/she/it (which? the/this/who *k*) teaching (the/this/who *k*) new (this/he/she/it that/since: that *k*) according to authority and the/this/who spirit/breath: spirit the/this/who unclean to command and to obey it/s/he
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
(and *no*) to go out (then *k*) the/this/who hearing it/s/he immediately (everywhere *NO*) toward all the/this/who region the/this/who Galilee
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
and immediately out from the/this/who synagogue (to go out to come/go *NK(O)*) toward the/this/who home Simon and Andrew with/after James and John
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
the/this/who then mother-in-law Simon to recline be feverish and immediately to say it/s/he about it/s/he
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
and to come near/agree to arise it/s/he to grasp/seize the/this/who hand (it/s/he *ko*) and to release: leave it/s/he the/this/who fever (immediately *K*) and to serve it/s/he
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
evening then to be when (to set *N(k)O*) the/this/who sun to bear/lead to/with it/s/he all the/this/who badly to have/be and the/this/who be demonised
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
and to be all the/this/who city to gather to/with the/this/who door
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
and to serve/heal much badly to have/be various illness and demon much to expel and no to release: permit to speak the/this/who demon that/since: since to perceive: know it/s/he (Christ to exist *O*)
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
and early at night greatly to arise to go out and to go away toward deserted place and there to pray
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
and (to seek *N(k)O*) it/s/he (the/this/who *ko*) Simon and the/this/who with/after it/s/he
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
and (to find/meet *N(k)O*) it/s/he (and *no*) to say it/s/he that/since: that all to seek you
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
and to say it/s/he to bring (from elsewhere *NO*) toward the/this/who to have/be village in order that/to and there to preach toward this/he/she/it for (to go out *N(k)O*)
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
and (to come/go *N(k)O*) to preach (toward the/this/who synagogue *N(k)O*) it/s/he toward all the/this/who Galilee and the/this/who demon to expel
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
and to come/go to/with it/s/he leprous to plead/comfort it/s/he and to kneel (it/s/he *ko*) and to say it/s/he that/since: that if to will/desire be able me to clean
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
(the/this/who *k*) (and *N(k)O*) (Jesus *k*) (to pity *NK(O)*) to stretch out the/this/who hand it/s/he to touch and to say it/s/he to will/desire to clean
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
and (to say it/s/he *K*) immediately to go away away from it/s/he the/this/who leprosy and to clean
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
and be agitated it/s/he immediately to expel it/s/he
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
and to say it/s/he to see: see nothing nothing to say but to go you to show the/this/who priest and to bring to about the/this/who cleansing you which to order Moses toward testimony it/s/he
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
the/this/who then to go out be first to preach much and to publish abroad the/this/who word so never again it/s/he be able plainly toward city to enter but out/outside(r) (upon/to/against *N(k)O*) deserted place to be and to come/go to/with it/s/he (from all sides *N(k)O*)

< Marko 1 >