< Marko 1 >

1 Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
The beginning of the gospel of Jesus Christ, the Son of God.
2 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Tazama, nitamtuma mjumbe wangu mbele yako, atakayetengeneza njia mbele yako”:
As has been written in the prophets; Behold, I send my messenger before thy face, who will prepare thy way before thee;
3 “sauti ya mtu aliaye nyikani. ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’”
the voice of one roaring in the wilderness; Prepare ye the way of the Lord; make His paths straight.
4 Yohana alikuja, akibatiza huko nyikani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
John the Baptist came preaching in the wilderness the baptism of repentance unto the remission of sins.
5 Watu kutoka Uyahudi wote na sehemu zote za Yerusalemu walikuwa wakimwendea. Nao wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika Mto Yordani.
And all the Judean country and the Jerusalemites were going out unto him, and were being baptized by him in the river Jordan, confessing their sins.
6 Yohana alivaa mavazi yaliyotengenezwa kwa singa za ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwitu.
And John was clothed with camel's hair and a leathern girdle about his loins, and eating locusts and wild honey;
7 Naye alihubiri akisema, “Baada yangu atakuja yeye aliye na uwezo kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kuinama na kulegeza kamba za viatu vyake.
And he proclaimed, saying, I indeed baptized you with water; but One cometh after me more powerful than I; the latchet of His sandals I am not worthy, having stooped down, to loose,
8 Mimi nawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”
and He shall baptize you with the Holy Ghost.
9 Wakati huo Yesu akaja kutoka Nazareti ya Galilaya, naye akabatizwa na Yohana katika Mto Yordani.
And it came to pass in those days, Jesus came from Nazareth of Galilee, and was baptized by John in the Jordan.
10 Yesu alipokuwa akitoka ndani ya maji, aliona mbingu zikifunguka na Roho akishuka juu yake kama hua.
And coming up straightway from the water, He saw the heavens open and the Spirit like a dove descending on Him.
11 Nayo sauti kutoka mbinguni ikasema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
And there was a voice from the heavens: Thou art my beloved Son, in whom I delight.
12 Wakati huo huo, Roho akamwongoza Yesu kwenda nyikani,
And immediately the Spirit casts Him out into the wilderness.
13 naye akawa huko nyikani kwa muda wa siku arobaini, akijaribiwa na Shetani. Alikaa na wanyama wa mwituni, nao malaika wakamhudumia.
And he was in the wilderness forty days being tempted by Satan, and was with the wild beasts; and the angels continued to minister unto Him.
14 Baada ya Yohana kukamatwa na kutiwa gerezani, Yesu aliingia Galilaya akaanza kuhubiri habari njema ya Mungu,
After that John was cast into prison, Jesus came into Galilee preaching the gospel of the kingdom of God,
15 akisema, “Wakati umewadia, Ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema.”
and saying, That the time is fulfilled: the kingdom of God is at hand: repent, and believe the gospel.
16 Yesu alipokuwa akitembea kando ya Bahari ya Galilaya, aliwaona Simoni na Andrea nduguye wakizitupa nyavu zao baharini, kwa kuwa wao walikuwa wavuvi.
And walking by the sea of Galilee, He saw Simon and Andrew his brother casting their net in the sea: for they were fishers.
17 Yesu akawaambia, “Njooni, nifuateni nami nitawafanya mwe wavuvi wa watu.”
Jesus said to them, Come after me, and I will make you to be fishers of men.
18 Mara wakaacha nyavu zao, wakamfuata.
And immediately, having left their nets, they followed Him.
19 Alipokwenda mbele kidogo, akamwona Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, wakiwa kwenye mashua yao wakizitengeneza nyavu zao.
And going forth thence a little, He saw James, the son of Zebedee, and John his brother, themselves also in a ship mending their nets,
20 Papo hapo akawaita, nao wakamwacha Zebedayo baba yao kwenye mashua pamoja na watumishi wa kuajiriwa, nao wakamfuata Yesu.
and immediately He called them. And having left their father Zebedee in the ship with the hired hands, they departed after Him.
21 Wakaenda mpaka Kapernaumu. Ilipofika siku ya Sabato, mara Yesu akaingia sinagogi, akaanza kufundisha.
And they come into Capernaum; and immediately on the Sabbath, He was teaching in the synagogue.
22 Watu wakashangaa sana kwa mafundisho yake, kwa maana aliwafundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wa sheria.
And they were astonished at His teaching; for Ile was teaching them as one having authority, and not as the scribes.
23 Wakati huo huo katika sinagogi lao palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu,
And there was a man in their synagogue with an unclean spirit; and he cried out,
24 naye akapiga kelele akisema, “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”
saying, Let me alone; what is there to us and thee, thou Jesus, the Nazarene? You have come to destroy us; I know thee who thou art, the Holy One of God.
25 Lakini Yesu akamkemea, akamwambia, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!”
And Jesus rebuked him, saying, Be silent, and come out from him.
26 Yule pepo mchafu akamtikisatikisa huyo mtu kwa nguvu, kisha akamtoka akipiga kelele kwa sauti kubwa.
And the unclean spirit, convulsing him and crying with a great voice, came out from him.
27 Watu wote wakashangaa, hata wakaulizana wao kwa wao, “Haya ni mambo gani? Ni mafundisho mapya, tena yenye mamlaka! Anaamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”
And they were all astonished, so that they were inquiring one to another, saying, What is this? what new teaching is this? Because according to authority He commands the unclean spirits, and they obey Him;
28 Sifa zake zikaanza kuenea haraka katika eneo lote la karibu na Galilaya.
and His fame went out immediately into all the surrounding country of Galilee.
29 Mara walipotoka katika sinagogi, walikwenda pamoja na Yakobo na Yohana hadi nyumbani kwa Simoni na Andrea.
And immediately, having come out from the synagogue, they came into the house of Simon and Andrew, with James and John.
30 Mama mkwe wa Simoni alikuwa kitandani, ana homa, nao wakamweleza Yesu habari zake.
And the mother-in-law of Simon was lying down burning with fever; and immediately they speak to Him concerning her:
31 Hivyo Yesu akamwendea, akamshika mkono na kumwinua. Kisha homa ikamwacha, naye akaanza kuwahudumia.
And having come to her, taking her by the hand, He raised her up; and immediately the fever left her, and she continued to minister unto them.
32 Jioni ile baada ya jua kutua, watu wakamletea Yesu wagonjwa wote na waliopagawa na pepo wachafu.
And it being evening, when the sun went down, they were carrying to Him all the sick and demonized;
33 Mji wote ukakusanyika mbele ya nyumba hiyo.
and the whole city was gathered to the door.
34 Yesu akawaponya watu wengi waliokuwa na magonjwa ya aina mbalimbali. Akawatoa pepo wachafu wengi, lakini hakuwaacha hao pepo wachafu waseme, kwa sababu walimjua yeye ni nani.
And He healed many who were afflicted with various diseases, and He cast out many demons; and did not suffer the demons to speak, because they knew Him.
35 Alfajiri na mapema sana kulipokuwa bado kuna giza, Yesu akaamka, akaondoka, akaenda mahali pa faragha ili kuomba.
And in the morning, exceedingly early, while it was yet night, having arisen up He came out, and went away into a desert place, and was praying there.
36 Simoni na wenzake wakaenda kumtafuta,
And Simon and those who were with him followed Him.
37 nao walipomwona, wakamwambia, “Kila mtu anakutafuta!”
And they found Him, and say to Him, All are seeking after thee.
38 Yesu akawajibu, “Twendeni mahali pengine kwenye vijiji jirani, ili niweze kuhubiri huko pia, kwa sababu hicho ndicho nilichokuja kukifanya.”
And He says to them, Let us go into the surrounding villages and cities, that I may preach there; for unto this I have come out.
39 Kwa hiyo akazunguka Galilaya kote, akihubiri katika masinagogi yao na kutoa pepo wachafu.
And He was preaching in their synagogues in all Galilee, and casting out the demons.
40 Mtu mmoja mwenye ukoma alimjia Yesu, akamwomba akipiga magoti, akamwambia, “Ukitaka, waweza kunitakasa.”
And a leper comes to Him, entreating Him, and bowing the knee to Him, and saying to Him, That if thou mayest be willing, thou art able to cleanse me.
41 Yesu, akiwa amejawa na huruma, akanyoosha mkono wake akamgusa, akamwambia, “Nataka. Takasika!”
And Jesus being moved with compassion, reaching forth His hand, touched him, and says to him, I will; be thou cleansed.
42 Mara ukoma ukamtoka, naye akatakasika.
And He speaking, immediately the leprosy departed from him, and he was cleansed.
43 Baada ya Yesu kumwonya vikali, akamruhusu aende zake
And charging him, He immediately sent him away,
44 akimwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote habari hizi, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
and says to him, See that you may speak nothing to any one: but go, show thyself unto the priest, and offer for thy cleansing those things which Moses commanded, for a testimony unto them.
45 Lakini yule mtu akaenda akaanza kutangaza habari za kuponywa kwake waziwazi. Kwa hiyo, Yesu hakuweza tena kuingia katika miji waziwazi lakini alikaa sehemu zisizo na watu. Hata hivyo watu wakamfuata huko kutoka kila upande.
And he having gone out, began to proclaim many things, and to publish abroad the word, so that He was no longer able openly to come into the city, but was out in desert places: and they continued to come to Him from all directions.

< Marko 1 >