< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
ཏདཱ ཏཏྶམཱིཔཾ བཧཝོ ལོཀཱ ཨཱཡཱཏཱ ཨཏསྟེཥཱཾ བྷོཛྱདྲཝྱཱབྷཱཝཱད྄ ཡཱིཤུཿ ཤིཥྱཱནཱཧཱུཡ ཛགཱད, །
2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
ལོཀནིཝཧེ མམ ཀྲྀཔཱ ཛཱཡཏེ ཏེ དིནཏྲཡཾ མཡཱ སཱརྡྡྷཾ སནྟི ཏེཥཱཾ བྷོཛྱཾ ཀིམཔི ནཱསྟི།
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
ཏེཥཱཾ མདྷྱེ྅ནེཀེ དཱུརཱད྄ ཨཱགཏཱཿ, ཨབྷུཀྟེཥུ ཏེཥུ མཡཱ སྭགྲྀཧམབྷིཔྲཧིཏེཥུ ཏེ པཐི ཀླམིཥྱནྟི།
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
ཤིཥྱཱ ཨཝཱདིཥུཿ, ཨེཏཱཝཏོ ལོཀཱན྄ ཏརྤཡིཏུམ྄ ཨཏྲ པྲནྟརེ པཱུཔཱན྄ པྲཱཔྟུཾ ཀེན ཤཀྱཏེ?
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
ཏཏཿ ས ཏཱན྄ པཔྲཙྪ ཡུཥྨཱཀཾ ཀཏི པཱུཔཱཿ སནྟི? ཏེ྅ཀཐཡན྄ སཔྟ།
6 Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
ཏཏཿ ས ཏཱལློཀཱན྄ བྷུཝི སམུཔཝེཥྚུམ྄ ཨཱདིཤྱ ཏཱན྄ སཔྟ པཱུཔཱན྄ དྷྲྀཏྭཱ ཨཱིཤྭརགུཎཱན྄ ཨནུཀཱིརྟྟཡཱམཱས, བྷཾཀྟྭཱ པརིཝེཥཡིཏུཾ ཤིཥྱཱན྄ པྲཏི དདཽ, ཏཏསྟེ ལོཀེབྷྱཿ པརིཝེཥཡཱམཱསུཿ།
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
ཏཐཱ ཏེཥཱཾ སམཱིཔེ ཡེ ཀྵུདྲམཏྶྱཱ ཨཱསན྄ ཏཱནཔྱཱདཱཡ ཨཱིཤྭརགུཎཱན྄ སཾཀཱིརྟྱ པརིཝེཥཡིཏུམ྄ ཨཱདིཥྚཝཱན྄།
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
ཏཏོ ལོཀཱ བྷུཀྟྭཱ ཏྲྀཔྟིཾ གཏཱ ཨཝཤིཥྚཁཱདྱཻཿ པཱུརྞཱཿ སཔྟཌལླཀཱ གྲྀཧཱིཏཱཤྩ།
9 Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
ཨེཏེ བྷོཀྟཱརཿ པྲཱཡཤྩཏུཿ སཧསྲཔུརུཥཱ ཨཱསན྄ ཏཏཿ ས ཏཱན྄ ཝིསསརྫ།
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
ཨཐ ས ཤིཥྱཿ སཧ ནཱཝམཱརུཧྱ དལྨཱནཱུཐཱསཱིམཱམཱགཏཿ།
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
ཏཏཿ པརཾ ཕིརཱུཤིན ཨཱགཏྱ ཏེན སཧ ཝིཝདམཱནཱསྟསྱ པརཱིཀྵཱརྠམ྄ ཨཱཀཱཤཱིཡཙིཧྣཾ དྲཥྚུཾ ཡཱཙིཏཝནྟཿ།
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
ཏདཱ སོ྅ནྟརྡཱིརྒྷཾ ནིཤྭསྱཱཀཐཡཏ྄, ཨེཏེ ཝིདྱམཱནནརཱཿ ཀུཏཤྩིནྷཾ མྲྀགཡནྟེ? ཡུཥྨཱནཧཾ ཡཐཱརྠཾ བྲཝཱིམི ལོཀཱནེཏཱན྄ ཀིམཔི ཙིཧྣཾ ན དརྴཡིཥྱཏེ།
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
ཨཐ ཏཱན྄ ཧིཏྭཱ པུན རྣཱཝམ྄ ཨཱརུཧྱ པཱརམགཱཏ྄།
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
ཨེཏརྷི ཤིཥྱཻཿ པཱུཔེཥུ ཝིསྨྲྀཏེཥུ ནཱཝི ཏེཥཱཾ སནྣིདྷཽ པཱུཔ ཨེཀཨེཝ སྠིཏཿ།
15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
ཏདཱནཱིཾ ཡཱིཤུསྟཱན྄ ཨཱདིཥྚཝཱན྄ ཕིརཱུཤིནཱཾ ཧེརོདཤྩ ཀིཎྭཾ པྲཏི སཏརྐཱཿ སཱཝདྷཱནཱཤྩ བྷཝཏ།
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
ཏཏསྟེ྅ནྱོནྱཾ ཝིཝེཙནཾ ཀརྟུམ྄ ཨཱརེབྷིརེ, ཨསྨཱཀཾ སནྣིདྷཽ པཱུཔོ ནཱསྟཱིཏི ཧེཏོརིདཾ ཀཐཡཏི།
17 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
ཏད྄ བུདྭྭཱ ཡཱིཤུསྟེབྷྱོ྅ཀཐཡཏ྄ ཡུཥྨཱཀཾ སྠཱནེ པཱུཔཱབྷཱཝཱཏ྄ ཀུཏ ཨིཏྠཾ ཝིཏརྐཡཐ? ཡཱུཡཾ ཀིམདྱཱཔི ཀིམཔི ན ཛཱནཱིཐ? བོདྡྷུཉྩ ན ཤཀྣུཐ? ཡཱཝདདྱ ཀིཾ ཡུཥྨཱཀཾ མནཱཾསི ཀཋིནཱནི སནྟི?
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
སཏྶུ ནེཏྲེཥུ ཀིཾ ན པཤྱཐ? སཏྶུ ཀརྞེཥུ ཀིཾ ན ཤྲྀཎུཐ? ན སྨརཐ ཙ?
19 Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
ཡདཱཧཾ པཉྩཔཱུཔཱན྄ པཉྩསཧསྲཱཎཱཾ པུརུཥཱཎཱཾ མདྷྱེ བྷཾཀྟྭཱ དཏྟཝཱན྄ ཏདཱནཱིཾ ཡཱུཡམ྄ ཨཝཤིཥྚཔཱུཔཻཿ པཱུརྞཱན྄ ཀཏི ཌལླཀཱན྄ གྲྀཧཱིཏཝནྟཿ? ཏེ྅ཀཐཡན྄ དྭཱདཤཌལླཀཱན྄།
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
ཨཔརཉྩ ཡདཱ ཙཏུཿསཧསྲཱཎཱཾ པུརུཥཱཎཱཾ མདྷྱེ པཱུཔཱན྄ བྷཾཀྟྭཱདདཱཾ ཏདཱ ཡཱུཡམ྄ ཨཏིརིཀྟཔཱུཔཱནཱཾ ཀཏི ཌལླཀཱན྄ གྲྀཧཱིཏཝནྟཿ? ཏེ ཀཐཡཱམཱསུཿ སཔྟཌལླཀཱན྄།
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
ཏདཱ ས ཀཐིཏཝཱན྄ ཏརྷི ཡཱུཡམ྄ ཨདྷུནཱཔི ཀུཏོ བོདྭྭུཾ ན ཤཀྣུཐ?
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
ཨནནྟརཾ ཏསྨིན྄ བཻཏྶཻདཱནགརེ པྲཱཔྟེ ལོཀཱ ཨནྡྷམེཀཾ ནརཾ ཏཏྶམཱིཔམཱནཱིཡ ཏཾ སྤྲཥྚུཾ ཏཾ པྲཱརྠཡཱཉྩཀྲིརེ།
23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
ཏདཱ ཏསྱཱནྡྷསྱ ཀརཽ གྲྀཧཱིཏྭཱ ནགརཱད྄ བཧིརྡེཤཾ ཏཾ ནཱིཏཝཱན྄; ཏནྣེཏྲེ ནིཥྛཱིཝཾ དཏྟྭཱ ཏདྒཱཏྲེ ཧསྟཱཝརྤཡིཏྭཱ ཏཾ པཔྲཙྪ, ཀིམཔི པཤྱསི?
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
ས ནེཏྲེ ཨུནྨཱིལྱ ཛགཱད, ཝྲྀཀྵཝཏ྄ མནུཛཱན྄ གཙྪཏོ ནིརཱིཀྵེ།
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
ཏཏོ ཡཱིཤུཿ པུནསྟསྱ ནཡནཡོ རྷསྟཱཝརྤཡིཏྭཱ ཏསྱ ནེཏྲེ ཨུནྨཱིལཡཱམཱས; ཏསྨཱཏ྄ ས སྭསྠོ བྷཱུཏྭཱ སྤཥྚརཱུཔཾ སཪྻྭལོཀཱན྄ དདརྴ།
26 Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
ཏཏཿ པརཾ ཏྭཾ གྲཱམཾ མཱ གཙྪ གྲཱམསྠཾ ཀམཔི ཙ ཀིམཔྱནུཀྟྭཱ ནིཛགྲྀཧཾ ཡཱཧཱིཏྱཱདིཤྱ ཡཱིཤུསྟཾ ནིཛགྲྀཧཾ པྲཧིཏཝཱན྄།
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
ཨནནྟརཾ ཤིཥྱཻཿ སཧིཏོ ཡཱིཤུཿ ཀཻསརཱིཡཱཕིལིཔིཔུརཾ ཛགཱམ, པཐི གཙྪན྄ ཏཱནཔྲྀཙྪཏ྄ ཀོ྅ཧམ྄ ཨཏྲ ལོཀཱཿ ཀིཾ ཝདནྟི?
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
ཏེ པྲཏྱཱུཙུཿ ཏྭཱཾ ཡོཧནཾ མཛྫཀཾ ཝདནྟི ཀིནྟུ ཀེཔི ཀེཔི ཨེལིཡཾ ཝདནྟི; ཨཔརེ ཀེཔི ཀེཔི བྷཝིཥྱདྭཱདིནཱམ྄ ཨེཀོ ཛན ཨིཏི ཝདནྟི།
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
ཨཐ ས ཏཱནཔྲྀཙྪཏ྄ ཀིནྟུ ཀོཧམ྄? ཨིཏྱཏྲ ཡཱུཡཾ ཀིཾ ཝདཐ? ཏདཱ པིཏརཿ པྲཏྱཝདཏ྄ བྷཝཱན྄ ཨབྷིཥིཀྟསྟྲཱཏཱ།
30 Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
ཏཏཿ ས ཏཱན྄ གཱཌྷམཱདིཤད྄ ཡཱུཡཾ མམ ཀཐཱ ཀསྨཻཙིདཔི མཱ ཀཐཡཏ།
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
མནུཥྱཔུཏྲེཎཱཝཤྱཾ བཧཝོ ཡཱཏནཱ བྷོཀྟཝྱཱཿ པྲཱཙཱིནལོཀཻཿ པྲདྷཱནཡཱཛཀཻརདྷྱཱཔཀཻཤྩ ས ནིནྡིཏཿ སན྄ གྷཱཏཡིཥྱཏེ ཏྲྀཏཱིཡདིནེ ཨུཏྠཱསྱཏི ཙ, ཡཱིཤུཿ ཤིཥྱཱནུཔདེཥྚུམཱརབྷྱ ཀཐཱམིམཱཾ སྤཥྚམཱཙཥྚ།
32 Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
ཏསྨཱཏ྄ པིཏརསྟསྱ ཧསྟཽ དྷྲྀཏྭཱ ཏཾ ཏརྫྫིཏཝཱན྄།
33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
ཀིནྟུ ས མུཁཾ པརཱཝརྟྱ ཤིཥྱགཎཾ ནིརཱིཀྵྱ པིཏརཾ ཏརྫཡིཏྭཱཝཱདཱིད྄ དཱུརཱིབྷཝ ཝིགྷྣཀཱརིན྄ ཨཱིཤྭརཱིཡཀཱཪྻྱཱདཔི མནུཥྱཀཱཪྻྱཾ ཏུབྷྱཾ རོཙཏཏརཱཾ།
34 Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
ཨཐ ས ལོཀཱན྄ ཤིཥྱཱཾཤྩཱཧཱུཡ ཛགཱད ཡཿ ཀཤྩིན྄ མཱམནུགནྟུམ྄ ཨིཙྪཏི ས ཨཱཏྨཱནཾ དཱམྱཏུ, སྭཀྲུཤཾ གྲྀཧཱིཏྭཱ མཏྤཤྩཱད྄ ཨཱཡཱཏུ།
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
ཡཏོ ཡཿ ཀཤྩིཏ྄ སྭཔྲཱཎཾ རཀྵིཏུམིཙྪཏི ས ཏཾ ཧཱརཡིཥྱཏི, ཀིནྟུ ཡཿ ཀཤྩིན྄ མདརྠཾ སུསཾཝཱདཱརྠཉྩ པྲཱཎཾ ཧཱརཡཏི ས ཏཾ རཀྵིཥྱཏི།
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
ཨཔརཉྩ མནུཛཿ སཪྻྭཾ ཛགཏ྄ པྲཱཔྱ ཡདི སྭཔྲཱཎཾ ཧཱརཡཏི ཏརྷི ཏསྱ ཀོ ལཱབྷཿ?
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
ནརཿ སྭཔྲཱཎཝིནིམཡེན ཀིཾ དཱཏུཾ ཤཀྣོཏི?
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
ཨེཏེཥཱཾ ཝྱབྷིཙཱརིཎཱཾ པཱཔིནཱཉྩ ལོཀཱནཱཾ སཱཀྵཱད྄ ཡདི ཀོཔི མཱཾ མཏྐཐཱཉྩ ལཛྫཱསྤདཾ ཛཱནཱཏི ཏརྷི མནུཛཔུཏྲོ ཡདཱ དྷརྨྨདཱུཏཻཿ སཧ པིཏུཿ པྲབྷཱཝེཎཱགམིཥྱཏི ཏདཱ སོཔི ཏཾ ལཛྫཱསྤདཾ ཛྙཱསྱཏི།

< Marko 8 >