< Marko 8 >
1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
tadA tatsamIpaM bahavo lokA AyAtA atasteShAM bhojyadravyAbhAvAd yIshuH shiShyAnAhUya jagAda, |
2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
lokanivahe mama kR^ipA jAyate te dinatrayaM mayA sArddhaM santi teShAM bhojyaM kimapi nAsti|
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
teShAM madhye. aneke dUrAd AgatAH, abhukteShu teShu mayA svagR^ihamabhiprahiteShu te pathi klamiShyanti|
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
shiShyA avAdiShuH, etAvato lokAn tarpayitum atra prantare pUpAn prAptuM kena shakyate?
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
tataH sa tAn paprachCha yuShmAkaM kati pUpAH santi? te. akathayan sapta|
6 Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
tataH sa tAllokAn bhuvi samupaveShTum Adishya tAn sapta pUpAn dhR^itvA IshvaraguNAn anukIrttayAmAsa, bhaMktvA pariveShayituM shiShyAn prati dadau, tataste lokebhyaH pariveShayAmAsuH|
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
tathA teShAM samIpe ye kShudramatsyA Asan tAnapyAdAya IshvaraguNAn saMkIrtya pariveShayitum AdiShTavAn|
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
tato lokA bhuktvA tR^iptiM gatA avashiShTakhAdyaiH pUrNAH saptaDallakA gR^ihItAshcha|
9 Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
ete bhoktAraH prAyashchatuH sahasrapuruShA Asan tataH sa tAn visasarja|
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
atha sa shiShyaH saha nAvamAruhya dalmAnUthAsImAmAgataH|
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
tataH paraM phirUshina Agatya tena saha vivadamAnAstasya parIkShArtham AkAshIyachihnaM draShTuM yAchitavantaH|
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
tadA so. antardIrghaM nishvasyAkathayat, ete vidyamAnanarAH kutashchinhaM mR^igayante? yuShmAnahaM yathArthaM bravImi lokAnetAn kimapi chihnaM na darshayiShyate|
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
atha tAn hitvA puna rnAvam Aruhya pAramagAt|
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
etarhi shiShyaiH pUpeShu vismR^iteShu nAvi teShAM sannidhau pUpa ekaeva sthitaH|
15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
tadAnIM yIshustAn AdiShTavAn phirUshinAM herodashcha kiNvaM prati satarkAH sAvadhAnAshcha bhavata|
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
tataste. anyonyaM vivechanaM kartum Arebhire, asmAkaM sannidhau pUpo nAstIti hetoridaM kathayati|
17 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
tad budvvA yIshustebhyo. akathayat yuShmAkaM sthAne pUpAbhAvAt kuta itthaM vitarkayatha? yUyaM kimadyApi kimapi na jAnItha? boddhu ncha na shaknutha? yAvadadya kiM yuShmAkaM manAMsi kaThinAni santi?
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
satsu netreShu kiM na pashyatha? satsu karNeShu kiM na shR^iNutha? na smaratha cha?
19 Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
yadAhaM pa nchapUpAn pa nchasahasrANAM puruShANAM madhye bhaMktvA dattavAn tadAnIM yUyam avashiShTapUpaiH pUrNAn kati DallakAn gR^ihItavantaH? te. akathayan dvAdashaDallakAn|
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
apara ncha yadA chatuHsahasrANAM puruShANAM madhye pUpAn bhaMktvAdadAM tadA yUyam atiriktapUpAnAM kati DallakAn gR^ihItavantaH? te kathayAmAsuH saptaDallakAn|
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
tadA sa kathitavAn tarhi yUyam adhunApi kuto bodvvuM na shaknutha?
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
anantaraM tasmin baitsaidAnagare prApte lokA andhamekaM naraM tatsamIpamAnIya taM spraShTuM taM prArthayA nchakrire|
23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
tadA tasyAndhasya karau gR^ihItvA nagarAd bahirdeshaM taM nItavAn; tannetre niShThIvaM dattvA tadgAtre hastAvarpayitvA taM paprachCha, kimapi pashyasi?
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
sa netre unmIlya jagAda, vR^ikShavat manujAn gachChato nirIkShe|
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
tato yIshuH punastasya nayanayo rhastAvarpayitvA tasya netre unmIlayAmAsa; tasmAt sa svastho bhUtvA spaShTarUpaM sarvvalokAn dadarsha|
26 Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
tataH paraM tvaM grAmaM mA gachCha grAmasthaM kamapi cha kimapyanuktvA nijagR^ihaM yAhItyAdishya yIshustaM nijagR^ihaM prahitavAn|
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
anantaraM shiShyaiH sahito yIshuH kaisarIyAphilipipuraM jagAma, pathi gachChan tAnapR^ichChat ko. aham atra lokAH kiM vadanti?
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
te pratyUchuH tvAM yohanaM majjakaM vadanti kintu kepi kepi eliyaM vadanti; apare kepi kepi bhaviShyadvAdinAm eko jana iti vadanti|
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
atha sa tAnapR^ichChat kintu koham? ityatra yUyaM kiM vadatha? tadA pitaraH pratyavadat bhavAn abhiShiktastrAtA|
30 Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
tataH sa tAn gADhamAdishad yUyaM mama kathA kasmaichidapi mA kathayata|
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
manuShyaputreNAvashyaM bahavo yAtanA bhoktavyAH prAchInalokaiH pradhAnayAjakairadhyApakaishcha sa ninditaH san ghAtayiShyate tR^itIyadine utthAsyati cha, yIshuH shiShyAnupadeShTumArabhya kathAmimAM spaShTamAchaShTa|
32 Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
tasmAt pitarastasya hastau dhR^itvA taM tarjjitavAn|
33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
kintu sa mukhaM parAvartya shiShyagaNaM nirIkShya pitaraM tarjayitvAvAdId dUrIbhava vighnakArin IshvarIyakAryyAdapi manuShyakAryyaM tubhyaM rochatatarAM|
34 Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
atha sa lokAn shiShyAMshchAhUya jagAda yaH kashchin mAmanugantum ichChati sa AtmAnaM dAmyatu, svakrushaM gR^ihItvA matpashchAd AyAtu|
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
yato yaH kashchit svaprANaM rakShitumichChati sa taM hArayiShyati, kintu yaH kashchin madarthaM susaMvAdArtha ncha prANaM hArayati sa taM rakShiShyati|
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
apara ncha manujaH sarvvaM jagat prApya yadi svaprANaM hArayati tarhi tasya ko lAbhaH?
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
naraH svaprANavinimayena kiM dAtuM shaknoti?
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
eteShAM vyabhichAriNAM pApinA ncha lokAnAM sAkShAd yadi kopi mAM matkathA ncha lajjAspadaM jAnAti tarhi manujaputro yadA dharmmadUtaiH saha pituH prabhAveNAgamiShyati tadA sopi taM lajjAspadaM j nAsyati|