< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
During those days, a large crowd of people gathered again. [After they had been there a couple days], they had no food to eat. So Jesus summoned the disciples [to come closer] and then he said to them,
2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
“This is the third day that these people have been with me, and they have nothing [left] to eat, so now I feel very sorry for them.
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
Furthermore, if I send them home [while they are still] hungry, [some of] them will faint on the way home, because some of them have come from far away.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
[Knowing that he was suggesting that they give the people something to eat, one of] his disciples replied, “(We cannot possibly find food to satisfy this crowd, here in this place where no people live!/How can we find food to satisfy this crowd, here in this place where no people live?)” [RHQ]
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
Jesus asked them, “How many loaves of bread do you have?” They replied, “[We have] seven [flat loaves].”
6 Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
Jesus commanded the crowd, “Sit down on the ground!” [After they sat down], he took the seven loaves, he thanked [God for them], he broke them [into pieces] and started giving them to his disciples in order that they might distribute them [to the people].
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
[They found that] they [also] had a few small [dried] fish. So after he thanked God for these, he told the disciples, “Distribute these also.” [After they distributed the bread and fish to the crowd],
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
the people ate this food and they had plenty [to] satisfy [them]. [The disciples] collected the pieces of food that were left over. [They filled] seven large baskets full of those pieces.
9 Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
[They estimated that] there were about 4,000 people [who ate on that day].
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
Then Jesus dismissed the crowd. Immediately after that, he got into the boat along with his disciples, and they went [around Lake Galilee] to Dalmanutha district.
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
[In those days some] Pharisees came to Jesus. They asked him [to perform] a miracle [that would show that] God [had sent him]. They wanted to [find a way by which they could] convince the people to reject him. [So] they started to argue with him.
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
Jesus sighed quietly to himself, and then he said, “I am disgusted that [RHQ], [even though] you people have seen how I [have healed people], you keep asking me to perform miracles! Note this: Such a miracle will certainly not be shown {I will certainly not show such a miracle} [just] for you people!”
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
Then he left them. He got into the boat again, along [with his disciples], and they went further around [Lake Galilee].
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
The disciples had forgotten to bring along [enough] food. Specifically, they had only one flat loaf of bread with them in the boat.
15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
[As they were going], Jesus warned them against [the attitudes the Pharisees and Herod Antipas had, attitudes that were having a bad effect on other people. He did this by telling them a parable]. He said, “Be careful! Beware of the yeast of the Pharisees and the yeast of Herod!”
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
[The disciples misunderstood him]. So they said to one another, “[He must have said that] because we have no bread.”
17 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
Jesus knew [what they were discussing among themselves]. So he said to them, “([I am disappointed that you are] discussing about your not having enough bread!/Why are you discussing about your not having enough bread?) [RHQ] (You should understand by now [that I can provide miraculously for you if you need food!/Why do you not yet perceive or understand that I can provide miraculously for you if you need food]?) [RHQ] (You are not thinking!/Why are you not thinking?) [RHQ]
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
(I am also disappointed that, although you have eyes, you do not [understand what you] see!/Why is it that, although you have eyes, you do not [understand what you] see?) [RHQ] You have ears, but you do not understand [what I say] [RHQ]!” [Then he asked], “Do you not remember [what happened]
19 Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
when I broke [only] five loaves [and fed] the 5.000 people [RHQ]? [Not only was everyone satisfied, but there was food left over] How many baskets full of pieces of bread [that were left over] did you collect?” They replied, “We collected twelve baskets full.”
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
Then he asked, “When I broke the seven loaves in order to [feed] the 4,000 people, [again when everyone had plenty to eat], how many large baskets [of pieces of bread that were left over] did you collect?” They replied, “[We collected] seven [large baskets full].”
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
Then he kept saying to them, “([I am disappointed that] you do not understand yet [that you should never worry that you do not have enough food]!/Why do you not understand yet [that you should never worry that you do not have enough food]?)” [RHQ]
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
They arrived [in the boat] at Bethsaida [town]. People brought to Jesus a blind man and earnestly requested that Jesus touch him [in order to heal him].
23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
Jesus took the hand of the blind man, led him outside the town, he put his saliva on the man’s eyes, he put his hands on the man, and then he asked him, “Do you see anything?”
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
The man looked up and then he said, “[Yes], I see people! They are walking around, but I cannot see them [clearly]. They look like trees!”
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
Then Jesus again touched the eyes of the blind man. The man looked intently and at that moment he was completely healed! He could see everything clearly.
26 Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
Jesus said to him, “Do not go into the town! [First go straight home and tell the people there about what I did]!” Then he sent the man to his home.
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
Jesus and the disciples [left Bethsaida town and went to the villages near Caesarea Philippi town]. On the way he questioned them, “Who do people say that I [really] am?”
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
They replied, “[Some people say] that you are John the Baptizer, [who has come back to life again]. Others say [that you are the prophet] Elijah [who has returned from heaven as God promised]. And others say that you are one of the [other former] prophets [who has come back to life again].”
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
He asked them, “What about you? Who do you say that I am?” Peter replied to him, “[We believe that] you are the Messiah!”
30 Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
Then Jesus warned them strongly that they should not tell anyone [yet that he was the Messiah].
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
Then Jesus began to teach them, “[Even though] I am the one who came from heaven, it is necessary that I suffer very much. It is also necessary that I be rejected by the elders, the chief priests, and the men who teach the [Jewish] laws {that the elders, the chief priests, and the men who teach the [Jewish] laws reject me}, and that I be killed {they kill me}. But on the third day [after I am killed I] will become alive again.”
32 Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
He said this to them clearly. But Peter took Jesus aside and then, [because he assumed that the Messiah would never die], he started to rebuke Jesus [for talking about dying].
33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
Jesus turned around and looked at his disciples. Then he rebuked Peter, saying, “Stop thinking like that! Satan [is causing you to talk like that! Instead] of wanting what God wants [me to do, you are wanting] me to do [only] what [most] people [would want me to do].”
34 Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
Then he summoned the crowd along with his disciples [so that they might listen to him]. He told them, “If any one [of you] wants to be my disciple, you must not do [only] what you yourself want to do. Specifically, you must [be willing to allow people to hurt you and to disgrace you. That is what they do to criminals] who are forced to carry crosses [MET] [to the places where they will be crucified]. That is what anyone who wants to be my disciple must do.
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
[You must do that], because those who try to save their lives [by denying that they belong to me when people want to kill them for believing in me] will not live [eternally], but those who are killed because of being my [disciples] and [because of telling others my] good message will live [forever with me].
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
People might get everything [they want] in this world, but (they are really gaining nothing if they do not get eternal life [because they do not become my disciples!]/what will they gain if they do not get eternal life [because they do not become my disciples]?) [RHQ]
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
([Think carefully about the fact that] there is absolutely nothing that people can give [to God] that would enable them to gain eternal life!/Is there anything that a person can give [to God] in order to gain eternal life?) [RHQ]
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
And think about this: Those who refuse [to say that they belong to] me and who reject what I say in these days when many people have turned away [from God] and are very sinful, I, the one who came from heaven, will also refuse [to say that they belong to me] when I come back with the holy angels and have the glorious brightness that my Father has!”

< Marko 8 >