< Marko 8 >
1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those days, when there was a large crowd, and they had nothing to eat, he called the talmidim to himself, and said to them,
2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
"I have compassion on the crowd, because they have stayed with me now three days, and have nothing to eat.
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
If I send them away fasting to their home, they will faint on the way, and some of them have come a long way."
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
His talmidim answered him, "From where could one satisfy these people with bread here in a deserted place?"
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
He asked them, "How many loaves do you have?" They said, "Seven."
6 Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
He commanded the crowd to sit down on the ground, and he took the seven loaves. Having given thanks, he broke them, and gave them to his talmidim to serve, and they served the crowd.
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
They had a few small fish. Having blessed them, he said to serve these also.
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
They ate, and were filled. They took up seven baskets of broken pieces that were left over.
9 Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
Now they were about four thousand. Then he sent them away.
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
Immediately he entered into the boat with his talmidim, and came into the region of Dalmanutha.
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
The Pharisees came out and began to question him, seeking from him a sign from heaven, and testing him.
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
He sighed deeply in his spirit, and said, "Why does this generation seek a sign? Truly I tell you, no sign will be given to this generation."
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
And he left them, and got into the boat again, and went to the other side.
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
Now they forgot to take bread; and they did not have more than one loaf in the boat with them.
15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
He warned them, saying, "Watch out; guard yourselves against the hametz of the Pharisees and the hametz of Herod."
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
And they began discussing among themselves that they had no bread.
17 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
He, perceiving it, said to them, "Why do you reason that it's because you have no bread? Do you not perceive yet, neither understand? Are your hearts hardened?
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
Having eyes, do you not see? Having ears, do you not hear? Do you not remember?
19 Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
When I broke the five loaves among the five thousand, how many baskets full of broken pieces did you take up?" They told him, "Twelve."
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
"When the seven loaves fed the four thousand, how many baskets full of broken pieces did you take up?" And they said, "Seven."
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
He asked them, "Do you not yet understand?"
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
He came to Beit Tzaidah. They brought a blind man to him, and begged Yeshua to touch him.
23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
He took hold of the blind man by the hand, and brought him out of the village. When he had spit on his eyes, and laid his hands on him, he asked him if he saw anything.
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
He looked up, and said, "I see people; they look like trees walking."
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
Then again he laid his hands on his eyes. He made him look up, and was restored, and saw everything clearly.
26 Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
He sent him away to his house, saying, "Do not enter into the village."
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
Yeshua went out, with his talmidim, into the villages of Caesarea Philippi. On the way he asked his talmidim, "Who do people say that I am?"
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
And they said to him, saying, "John the Immerser, and others say Elijah, but others: one of the prophets."
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
He said to them, "But who do you say that I am?" Peter answered and said to him, "You are the Messiah."
30 Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
He commanded them that they should tell no one about him.
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
He began to teach them that the Son of Man must suffer many things, and be rejected by the elders, the chief cohanim, and the scribes, and be killed, and after three days rise again.
32 Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
He spoke to them openly. Peter took him, and began to rebuke him.
33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
But he, turning around, and seeing his talmidim, rebuked Peter, and said, "Get behind me, Satan. For you have in mind not the things of God, but the things of humans."
34 Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
He called the crowd to himself with his talmidim, and said to them, "If anyone wants to come after me, let him deny himself, and take up his cross, and follow me.
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
For whoever wants to save his life will lose it; and whoever will lose his life for my sake and the sake of the Good News will save it.
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
For what does it profit a person to gain the whole world, and forfeit his soul?
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
Or what will a person give in exchange for his soul?
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
For whoever will be ashamed of me and of my words in this adulterous and sinful generation, the Son of Man also will be ashamed of him, when he comes in the glory of his Father with the holy angels."