< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, umati mkubwa wa watu ulikusanyika tena. Kwa kuwa walikuwa hawana chakula, Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
In those days the multitude being very great, and not having what they may eat, Jesus having called near His disciples, says to them,
2 “Ninauhurumia huu umati wa watu, kwa sababu sasa wamekuwa nami kwa muda wa siku tatu na hawana chakula.
“I have compassion on the multitude, because now three days they continue with Me, and they have not what they may eat;
3 Nikiwaaga waende nyumbani bila kula, watazimia njiani kwa sababu baadhi yao wametoka mbali.”
and if I will let them away fasting to their home, they will faint in the way, for certain of them are come from far.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Lakini hapa nyikani tutapata wapi mikate ya kutosha kuwalisha?”
And His disciples answered Him, “From where will anyone be able to feed these here in a wilderness with bread?”
5 Yesu akawauliza, “Mna mikate mingapi?” Wakajibu, “Tuna mikate saba.”
And He was questioning them, “How many loaves do you have?” And they said, “Seven.”
6 Akawaambia watu waketi chini. Akiisha kuichukua mikate saba na kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi wake ili wawagawie watu. Wanafunzi wake wakafanya hivyo.
And He commanded the multitude to sit down on the ground, and having taken the seven loaves, having given thanks, He broke, and was giving to His disciples that they may set before [them]; and they set before the multitude.
7 Walikuwa pia na visamaki vichache, Yesu akavibariki, akawaamuru wanafunzi wake wawagawie watu.
And they had a few small fishes, and having blessed, He said to set them also before [them];
8 Wale watu walikula na kutosheka. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
and they ate and were filled, and they took up that which was over of broken pieces—seven baskets;
9 Watu waliokula walikuwa wapata 4,000. Akiisha kuwaaga,
and those eating were about four thousand. And He let them away,
10 aliingia kwenye mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda sehemu za Dalmanutha.
and immediately having entered into the boat with His disciples, He came to the parts of Dalmanutha,
11 Mafarisayo wakaja, wakaanza kumhoji Yesu. Ili kumtega, wakamwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.
and the Pharisees came forth, and began to dispute with Him, seeking from Him a sign from Heaven, tempting Him;
12 Akahuzunika moyoni, akawaambia, “Kwa nini kizazi hiki kinataka ishara? Amin nawaambieni, hakitapewa ishara yoyote.”
and having sighed deeply in His spirit, He says, “Why does this generation seek after a sign? Truly I say to you, no sign will be given to this generation.”
13 Kisha akawaacha, akarudi kwenye mashua, akavuka hadi ngʼambo.
And having left them, having entered again into the boat, He went away to the other side;
14 Wanafunzi walikuwa wamesahau kuchukua mikate ya kutosha. Walikuwa na mkate mmoja tu kwenye mashua.
and they forgot to take loaves, and except one loaf they had nothing with them in the boat,
15 Yesu akawaonya: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo na ya Herode.”
and He was charging them, saying, “Take heed, beware of the leaven of the Pharisees, and of the leaven of Herod,”
16 Wakajadiliana wao kwa wao, na kusema, “Anasema hivi kwa sababu hatukuleta mikate.”
and they were reasoning with one another, saying, “Because we have no loaves.”
17 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akawauliza: “Mbona mnajadiliana kuhusu kutokuwa na mikate? Je, bado hamtambui wala hamwelewi? Je, mbona mioyo yenu ni migumu kiasi hicho?
And Jesus having known, says to them, “Why do you reason, because you have no loaves? Do you not yet perceive, nor understand, yet have you hardened your heart?
18 Je, mna macho lakini mnashindwa kuona, na mna masikio lakini mnashindwa kusikia? Je, hamkumbuki?
Having eyes, do you not see? And having ears, do you not hear? And do you not remember?
19 Nilipoimega ile mikate mitano kuwalisha watu 5,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Kumi na viwili.”
When I broke the five loaves to the five thousand, how many hand-baskets full of broken pieces did you take up?” They say to Him, “Twelve.”
20 “Je, nilipoimega ile mikate saba kuwalisha watu 4,000, mlikusanya vikapu vingapi vilivyojaa vya masazo?” Wakamjibu, “Saba.”
“And when the seven to the four thousand, how many hand-baskets full of broken pieces did you take up?” And they said, “Seven.”
21 Ndipo akawauliza, “Je, bado hamwelewi?”
And He said to them, “How do you not understand?”
22 Wakafika Bethsaida na baadhi ya watu wakamleta mtu mmoja kipofu wakamsihi Yesu amguse.
And He comes to Bethsaida, and they bring to Him one blind, and call on Him that He may touch him,
23 Yesu akamshika mkono huyo kipofu akampeleka nje ya kijiji. Baada ya kuyatemea mate macho ya yule kipofu na kumwekea mikono, Yesu akamuuliza, “Unaona chochote?”
and having taken the hand of the blind man, He led him forth outside the village, and having spit on his eyes, having put [His] hands on him, He was questioning him if he beholds anything:
24 Yule kipofu akaangalia, akasema, “Ninaona watu, wanaonekana kama miti inayotembea.”
and he, having looked up, said, “I behold men, as I see trees, walking.”
25 Yesu akamwekea tena mikono machoni. Kisha macho yake yakafunguka, kuona kwake kukarejea naye akaona kila kitu dhahiri.
Afterward again He put [His] hands on his eyes, and made him look up, and he was restored, and discerned all things clearly,
26 Yesu akamuaga aende nyumbani kwake, akimwambia, “Hata kijijini usiingie.”
and He sent him away to his house, saying, “Neither may you go into the village, nor tell [it] to any in the village.”
27 Yesu na wanafunzi wake wakaondoka kwenda katika vijiji vya Kaisaria-Filipi. Walipokuwa njiani, Yesu akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
And Jesus went forth, and His disciples, into the villages of Caesarea Philippi, and in the way He was questioning His disciples, saying to them, “Who do men say I am?”
28 Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema wewe ni mmojawapo wa manabii.”
And they answered, “John the Immerser, and others Elijah, but others one of the prophets.”
29 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo.”
And He says to them, “And you—who do you say I am?” And Peter answering says to him, “You are the Christ.”
30 Yesu akawaonya wasimwambie mtu yeyote habari zake.
And He strictly charged them that they may tell no one about it,
31 Ndipo akaanza kuwafundisha wanafunzi wake kuwa Mwana wa Adamu lazima atapata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini baada ya siku tatu afufuke.
and began to teach them that it is necessary for the Son of Man to suffer many things, and to be rejected by the elders, and chief priests, and scribes, and to be killed, and to rise again after three days;
32 Aliyasema haya waziwazi, ndipo Petro akamchukua kando na akaanza kumkemea.
and openly He was speaking the word. And Peter having taken Him aside, began to rebuke Him,
33 Lakini Yesu alipogeuka na kuwaangalia wanafunzi wake, akamkemea Petro. Akasema, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.”
and He, having turned, and having looked on His disciples, rebuked Peter, saying, “Get behind Me, Satan, because you do not mind the things of God, but the things of men.”
34 Ndipo akauita ule umati wa watu pamoja na wanafunzi wake, akasema, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate.
And having called near the multitude, with His disciples, He said to them, “Whoever wills to come after Me—let him disown himself, and take up his cross, and follow Me;
35 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili atayaokoa.
for whoever may will to save his life will lose it; and whoever may lose his life for My sake and for the good news’ sake, he will save it;
36 Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?
for what will it profit a man, if he may gain the whole world, and forfeit his life?
37 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
Or what will a man give as an exchange for his life?
38 Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu wakati atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.”
For whoever may be ashamed of Me, and of My words, in this adulterous and sinful generation, the Son of Man will also be ashamed of him when He may come in the glory of His Father with the holy messengers.”

< Marko 8 >