< Marko 7 >
1 Mafarisayo na baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu wakakusanyika mbele ya Yesu.
YA mandaña guiya güiya y Fariseo sija, yan palo gui escriba sija ni manmato guine Jerusalem,
2 Wakawaona baadhi ya wanafunzi wake wakila chakula kwa mikono iliyo najisi, yaani, bila kunawa kama ilivyotakiwa na sheria ya dini ya Wayahudi.
Ya malie palo gui disipuluña na mañochocho pan yan áplacha na canae, ni comequeilegña na pot ti jafagase.
3 (Kwa kuwa Mafarisayo na Wayahudi wote hawali chakula pasipo kunawa kwa kufuata desturi za wazee wao.
Sa y Fariseo sija, yan toda y Judio sija, jaadadaje y tradision manamco sija, yaguin megae nae ti jafagase y canaeñija, ti ufañocho.
4 Wanapotoka sokoni hawawezi kula pasipo kunawa. Pia kuna desturi nyingine nyingi wanazofuata kama vile jinsi ya kuosha vikombe, vyungu na vyombo vya shaba.)
Ya anae manmato guine y metcado, yaguin ti jafagase sija, ti ufañocho; yan megae sija na güinaja rinesibeñija para ujaadaje, parejoja yan mafagase y copa sija, yan y jara sija, yan y bason coble sija.
5 Kwa hiyo wale Mafarisayo na walimu wa sheria wakamuuliza Yesu, “Mbona wanafunzi wako hawafuati desturi za wazee, na badala yake wanakula kwa mikono najisi?”
Ya mafaesen ni Fariseo sija yan y escriba sija: Jafa y disipulumo sija na ti manmamómocat taemano y tradision manamco sija; mañochochoja pan yan aplacha y canaeñija?
6 Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki. Kama ilivyoandikwa: “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
Ya ilegña nu sija: Hipocrita jamyo; mauleg sinanganña si Isaias, ni y esta matugue: Este sija na taotao y labiosñija nae maonrayo, lao y corasonñija chago guiya guajo.
7 Huniabudu bure, nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’
Lao taebale jaadorayo, manmamananagüe ni finanagüe ni tinago taotao sija.
8 Ninyi mmeziacha amri za Mungu na kushika desturi za watu.”
Sa inpelo jamyo y tinago Yuus, ya mantietiene fitme y tradision taotao sija: (ni y mafagase y jara sija, yan y copa sija, yan infatinas megae sija na güinaja parejo yan este.)
9 Naye akawaambia, “Ninyi mnayo njia nzuri ya kukataa amri za Mungu ili mpate kuyashika mapokeo yenu!
Ya ilegña nu sija: Magajet jamyo yumute y tinago Yuus para inadaje y tradisionmiyo.
10 Kwa mfano, Mose alisema, ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na, ‘Yeyote amtukanaye baba yake au mama yake, na auawe.’
Sa si Moises ilegña: Onra si tatamo yan si nanamo; ya y mumatdise y tata pat y nana, seguro na umatae.
11 Lakini ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho ningeweza kukusaidia ni Korbani’ (yaani kimewekwa wakfu kwa Mungu),
Lao jamyo ilegmiyo: Yaguin y taotao ilegña ni tataña pat nanaña: Y Cotban (cumequeilegña y ninae) na jago umaprobecha pot guajo, güiya sumaga libre.
12 basi hawajibiki tena kumsaidia baba yake au mama yake.
Ya inpelo güe na ufatinas taya para si tataña pat si nanaña;
13 Kwa njia hiyo ninyi mnabatilisha neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyojiwekea. Nanyi mnafanya mambo mengi ya aina hiyo.”
Inrechasa y sinangan Yuus ni ninaenmiyo na tradision; yan megae sija na güinaja finatinasmiyo parejo yan este.
14 Yesu akaita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni, kila mmoja wenu na mwelewe jambo hili.
Ya jaagang talo guiya güiya todo y linajyan taotao ya ilegña: Ecungog jamyo todos, ya intingo.
15 Hakuna kitu kinachomwingia mtu kimtiacho unajisi, lakini kile kimtokacho ndicho kimtiacho unajisi. [
Taya gui sumanjiyong gui taotao ni y janajalom, siña numataelaye, lao y janajujuyong gui jinalomña, ayo sija munatataelaye y taotao
16 Kama mtu yeyote ana masikio ya kusikia na asikie.]”
(Yaguin guaja gaetalanga para ufanjungog, uecungog)
17 Akiisha kuuacha ule umati wa watu na kuingia ndani, wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano ule.
Ya anae jumalom gui guima, jadingo y linajyan taotao, y disipuluña sija mafaesen güe ni acomparasion.
18 Akawajibu, “Je, hata nanyi hamwelewi? Je, hamfahamu kwamba kitu kimwingiacho mtu hakimtii unajisi?
Ya ilegña nu sija: Taegüenaja jamyo locue manaetiningo? Ti intingo na todo y guine jiyong ni jumajalom y taotao ti siña ninataelaye?
19 Mtu akila kitu hakiingii moyoni mwake bali tumboni, na baadaye hutolewa nje ya mwili wake.” (Kwa kusema hivi, Yesu alivihalalisha vyakula vyote kuwa ni “safi.”)
Sa ti jumajalom gui corasonña na y tiyanña ya malolofan gui secreto; taegüenao janagasgas todo y nengcano.
20 Akaendelea kusema, “Kile kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.
Yan ilegña: Y jumujuyong gui taotao, ayo munatataelaye y taotao.
21 Kwa maana kutoka ndani ya moyo wa mtu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi,
Sa y gui jinalomña gui corason y taotao sija nae, manjujuyong y manaelaye na jinaso sija, y manadulterio, y manábale yan y manpegno,
22 tamaa mbaya, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, matukano, kiburi na upumbavu.
Y mañaque sija, y manlatga, y manaelaye, y dinague, y inábale, y taelaye na atadog, y chinatfino contra si Yuus, y sobetbio, y bababa:
23 Maovu haya yote hutoka ndani ya mtu, nayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi.”
Todo este sija na tinaelaye, manguine jalom ya janatataelaye y taotao.
24 Ndipo Yesu akaondoka hapo akaenda sehemu za Tiro. Akaingia katika nyumba moja, naye hakutaka mtu yeyote ajue kwamba yuko humo. Lakini hakuweza kujificha.
Ya cajulo güije, mapos para y oriyan Tiro yan Sidon; ya jumalom gui guima, malagoña na taya utiningo; lao ti siña unatog.
25 Mara mwanamke mmoja, ambaye binti yake mdogo alikuwa na pepo mchafu, akaja na kumpigia magoti miguuni pake.
Sa jajungog masasangan güe un palaoan na y diquique na jagaña, guaja un áplacha na espiritu, mato ya jatomba güe gui adengña:
26 Basi huyo mwanamke alikuwa Myunani, aliyezaliwa Foinike ya Siria. Akamsihi Yesu amtoe binti yake huyo pepo mchafu.
Ya y palaoan Griega, gui tano Sirofenisa, y tinayuyut güe na uyute juyong gui jagaña y anite.
27 Yesu akamwambia, “Waache watoto washibe kwanza, kwa maana si vyema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”
Lao ilegña nu guiya: Polo finena ya ufanjaspog y famaguon sija; sa ti mauleg machule y pan y famaguon, ya ufanmayotte y galago sija.
28 Lakini yule mwanamke akamjibu, “Bwana, hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya chakula cha watoto.”
Ya manope y palaoan, ilegña: Junggan, Señot; lao y galago sija, gui papa lamasa, jacacanoja y andesmoronan y famaguon sija.
29 Ndipo Yesu akamjibu, “Kwa sababu ya jibu lako, nenda zako nyumbani; yule pepo mchafu amemtoka binti yako.”
Ayo nae ilegña ni palaoan: Pot este na sinangan, janao y anite jumanao gui jagamo.
30 Akaenda zake nyumbani akamkuta binti yake amelala kitandani, yule pepo mchafu akiwa amemtoka.
Ya anae jumanao para iyasija, jasoda na y jagaña umaason gui jilo cama, ya y anite esta jumanao.
31 Kisha Yesu akaondoka sehemu za Tiro, akapita katikati ya Sidoni, hadi Bahari ya Galilaya na kuingia eneo la Dekapoli.
Ya tumalo jumanao gui oriyan Tiro yan malofan guiya Sidon, ya mato gui tasen Galilea; ya malofan gui entalo y oriyan Decapolis.
32 Huko, watu wakamletea Yesu mtu mmoja kiziwi, ambaye pia alikuwa na kigugumizi, wakamwomba aweke mkono wake juu ya huyo mtu na amponye.
Ya maconie güe un tanga ya udo, ya matayuyut güe na upolo y canaeña gui jiloña.
33 Baadaye Yesu akampeleka yule kiziwi kando mbali na watu, Yesu akatia vidole vyake masikioni mwa yule mtu. Kisha akatema mate na kuugusa ulimi wa yule mtu.
Ya janasajnge güe gui linajyan taotao, ya japolo y calolotña gui talangan y tanga, ya tumola ya japacha y jilaña;
34 Ndipo Yesu akatazama mbinguni, akavuta hewa ndani kwa nguvu akamwambia, “Efatha!” (yaani, “Funguka!”)
Ya jaatan julo y langet sumospiros, ya ilegña: Efatha, cumequeilegña, mababa!
35 Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukaachiliwa, akaanza kuongea sawasawa.
Ya mababa y talangaña; ya mapula y gumogode y jilaña, ya cumuentos mauleg.
36 Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hizi. Lakini kadiri alivyowazuia, ndivyo walivyozidi kutangaza kwa bidii.
Ya jaencatga sija, na chañija sumangangane ni jaye; lao mientras mas jaencatga, mas manamamto;
37 Walistaajabu mno. Wakasema, “Amefanya mambo yote vizuri mno! Amewawezesha viziwi wasikie na bubu waseme!”
Ya ninafangosmanman, ilegñija: Mauleg finatinasña todo: janafanmanjungog y mananga, ya y manudo janafanguentos.