< Marko 5 >

1 Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi.
Vakafika umwamboijinge ija lisumbe, mulikaja lya Gerasi
2 Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye.
Nakalingi u Yesu ye ihuma mu ngalama, akisa kwa mwene umuunhu jumonga unyalipepo lilamafu akahumile ku mbiipa.
3 Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo.
U muumhu uu akikalagha ku mbiipa. Nakwalyale uwakunkola nabe kukundindila, nambe kukunkunga ni minyololo.
4 Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia.
kekinga akapinywagha ni pingu na manyololo. akadumulagha amanyololo ni pingu akadenyagha. Nakwaliyale unyangufu ghwa kumulefia.
5 Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.
Pakilo na pamwisi akikalagha ku mbiipa na kufidunda, akakolagha na kukutemateme namavue amajodofu.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake.
Ye am'bwene u Yesu pavutaali, akankimbilila na kufughama pa mwene.
7 Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”
Akakola ni lisio ilivaha, “Lunoghile nivombe kiki, Yesu, Mwana ghwa Nguluve juno alikukyanya fijo? Nikukusuma mulitavua lya Nguluve, uleke pikumumusia.”
8 Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”
Ulwakuva yumbulile, “Ghwe lipepo lichafu uve, huma mwa muunhu uju.”
9 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tuko wengi.”
Gwoope akamposia akati, “Ilitavua lyako veeve veeni?” Ghwope akamwamula, “Ilitavua lyango nene Ligioni, ul. wakuva tuliviinga.”
10 Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
Akampelepesia kange leka pikughadaga mu iisi jila.
11 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima.
Ilipugha ilivaha ilya ngube lilyale pakyana pakidunda silyale sidimua,
12 Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.”
ghoope ghokampelepesia, sikati, “Utusung'e mu ngube, mwetwingile munkate mu sene.”
13 Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.
Akaghatavula; amapepo amalamafu ghakahuma mwa muunhu na pikwingila mu ngube, sope sikakimbilila pasi pa kidunda na pikwingila mulisumbe, neke ilipugha lya ngube imbilima ivili sikadwivila mulisumbe
14 Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia.
Navadima ngube vakakimbila vakaluta mulikaja na mufikaja kuhumia imhola kusino sihumile na pivombeka mu likaja na mukisina. Pepano avaanhu vinga vakahuma kuta kulola kino kikahumile.
15 Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa.
Pepano vakisa kwa Yesu pe vakamwagha umuunhun juno ahasiling'ine na mapepo alyale nu nsikali ikalile pasi, afwasivue, ali nuluhala lunofu, voope va koghopa.
16 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia.
Vala vano vakasivwene sino sivombike kwa muunhu juno alyahassiling'ine na mapepo vakakimbila kino kikahumile kwa mwene kange vwimila ingube.
17 Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.
Voope vakampelepesia kuuti avuuke mu iisi jave.
18 Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja.
U Yesu ye ikwingila mu ngalava, umuunhu juno alyahasiling'ine na mapepo akampelepesiaa kuuti alutaghe palikimo nu mwene.
19 Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.”
U Yesu akankana, akati, “Lutagha kukaja na kuva nyalukolo vako, uvavule akuvombile u Mtwa, nulusungu luno akupelile.”
20 Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.
Pepano akavuka na kuluta kupulisia imbaha sino am'bombili u Yesu mu Dekapoli, imhola isio sikava kidegho ku vooni
21 Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari.
Pano u Yesu alyalovwike kange imwambo ijinge, mu ngalava, ilipugha ilivaha lika kong'ana kukunsungutila, pano alyale mulubale mulisumbe.
22 Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake,
Umbaha jumo ughwa va sinagogi, akatambuluagha Yairo, akisa, ye amwaghile, akaghua pa maghulu gha mwene.
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.”
Akampelepesia fijo kange fijo, akati, “Mwalivango n'debe ghukova pifua. Nikusuma ghwise uvike uluvoko lwako pakyanya pa mwne ulwakuuti usoke akupele uvwumi ughendelele pikukala.”
24 Hivyo Yesu akaenda pamoja naye. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga.
Apunakavuka palikimo nu mwene, nalilipugha ilivaha lika m'bingililaa vaka mpitagha kukunsungutila.
25 Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili.
Pwe alyale umumama jumonga juno alyale ihuma idanda inaaaamu ijio jilya mpumwisia amaka kijigho na gha viili.
26 Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya.
Alya pumuike yongo kuva ghanga vinga alya vombiile ikyuma kyoni kino alyale nakyo. Neke nalyasokile nambe padebe, looli inamu jikava jifikwongelela.
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake,
Akapulika imola isa Yesu. Pe akatengula kukwisa kughenda mumbele muno mwa mwene pano alyale ighenda pakate palipugha. ghwope akagusa umwenda ghwa mwene.
28 kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.”
wakuva akajovile, Nane ninga guse ghamenda ghake ni soka, niva mwumi.”
29 Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.
Ye agusile, idanda jikabuhilapihuma, akivoona mumbili ghwake asokile kuhuma munamu jila.
30 Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”
Unsiki ghughuo u Yesu akivona mu m'bili ghwake sihumile ingufu. Akyasyetuka imbale soni mulipugha pe akaposia, “Ghwe veeni juno abasisie u mwenda ghwango?”
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’”
Avavulanisivua vaake vaka mwamula, “Ulivwene ilipugha ilili likikupita lisyungutile, najuve ghuti, ghweveeni juno ikukwabasia?
32 Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa.
Looli u Yesu akava ifilolesia ulwakuuti ankagule juno amwabasisie.
33 Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote.
Umukijuuva, akakagula lunoluhumile kwa mwene, akoghopa na pihilila. Akalukagula pe akaghua pasi pamwene akolelela sooni sino sivombike.
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
Akajova kwa mwene, “Mwalivango usokile vwimila ulwitiko lwako. Ulutaghe nulutangano inamu jako jisoke lwoni
35 Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
Pano alyale ijova, valisile avaanhu vamo kuhuma kwa ngoyo wa Sinagogi, vakaati, “Umwalivo afuile. Kiki ghuku n'gasia um'bulanisi?”
36 Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
Looli u Yesu ye akipulike kino valyajovile, akambula um'baha ghwa sinagogi, “Uloghopagha. Itikagha.”
37 Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo.
Akavakana vooni kulutania naghwope, looli akantoola u Petro, Yakobo, nu Yohana navanyalukolo va Yakobo.
38 Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.
Vakisilepakaja pa m'baha ghwa va sinagogi ghwope akalivona ili batu, kukola na kulila.
39 Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.”
Ye ingile mu nyuma, akavaposia akati, “Kiki musukunile kange kiki mulila? Umwana nahwile looli ighona.”
40 Wale watu wakamcheka kwa dharau. Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto.
Vakanseka, looli umwene akavahumia vooni kunji, akavatola ava pafi nava vulanisivua vala, kingila munkaate muno mwealyale u mwana.
41 Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”)
Akankola uluvoko lwa mwana akati, “Talitha koum,” kwekuuti, “Ggwe minja uve nikukuvula, simuka.”
42 Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana.
Unsiki ghughuo umwana jula akasimuka na na pighenda (ulwakuva alyale na maka kijigho na ghaviili). nakalinga vakakoluo ni nganighani na nuludegho luvaha.
43 Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.
Akavakana ku ngufu kuuti nalunoghile umuunhu ghweni akagule imbombo jino jivombika apa. Akavavuula kuuti vampele uminja jula ikyakulia.

< Marko 5 >