< Marko 5 >
1 Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi.
Eles vieram para o outro lado do mar, para o país dos gadarenos.
2 Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye.
Quando ele saiu do barco, imediatamente um homem com um espírito impuro o encontrou fora dos túmulos.
3 Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo.
Ele vivia nos túmulos. Ninguém mais podia amarrá-lo, nem mesmo com correntes,
4 Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia.
porque ele havia sido frequentemente amarrado com grilhões e correntes, e as correntes haviam sido rasgadas por ele, e os grilhões quebrados em pedaços. Ninguém tinha a força para domá-lo.
5 Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.
Sempre, noite e dia, nos túmulos e nas montanhas, ele gritava, e se cortava com pedras.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake.
Quando viu Jesus de longe, ele correu e se curvou diante dele,
7 Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”
e gritando com voz alta, disse: “O que tenho a ver com você, Jesus, seu Filho do Deus Altíssimo? Eu te conjuro por Deus, não me atormentes”.
8 Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”
Pois ele lhe disse: “Saia do homem, seu espírito impuro!”
9 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tuko wengi.”
Ele lhe perguntou: “Qual é o seu nome?” Ele lhe disse: “Meu nome é Legião, pois somos muitos”.
10 Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
Ele lhe implorou muito que não os mandasse para fora do país.
11 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima.
Agora na encosta da montanha havia um grande rebanho de porcos alimentando-se.
12 Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.”
Todos os demônios lhe imploraram, dizendo: “Mande-nos para os porcos, para que possamos entrar neles”.
13 Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.
Imediatamente Jesus lhes deu permissão. Os espíritos impuros saíram e entraram nos porcos. O rebanho de cerca de dois mil pessoas apressou-se a descer a margem íngreme para o mar, e eles foram afogados no mar.
14 Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia.
Aqueles que alimentaram os porcos fugiram e o contaram na cidade e no campo. As pessoas vieram para ver o que tinha acontecido.
15 Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa.
Eles vieram a Jesus, e viram aquele que tinha sido possuído por demônios sentados, vestidos e em seu juízo perfeito, até mesmo aquele que tinha a legião; e ficaram com medo.
16 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia.
Aqueles que o viram declararam-lhes o que aconteceu com ele que estava possuído por demônios, e sobre os porcos.
17 Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.
Eles começaram a implorar para que ele saísse de sua região.
18 Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja.
Ao entrar no barco, aquele que tinha sido possuído por demônios implorou-lhe que pudesse estar com ele.
19 Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.”
Ele não o permitiu, mas lhe disse: “Vá a sua casa, a seus amigos, e diga-lhes que grandes coisas o Senhor fez por você e como ele teve misericórdia de você”.
20 Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.
Ele seguiu seu caminho, e começou a proclamar na Decápolis como Jesus havia feito grandes coisas por ele, e todos se maravilharam.
21 Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari.
Quando Jesus atravessou de volta no barco para o outro lado, uma grande multidão foi reunida a ele; e ele estava junto ao mar.
22 Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake,
Eis que veio um dos chefes da sinagoga, Jairo pelo nome; e vendo-o, caiu a seus pés
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.”
e implorou-lhe muito, dizendo: “Minha filhinha está a ponto de morrer”. Por favor, venha e ponha suas mãos sobre ela, para que ela se torne saudável, e viva”.
24 Hivyo Yesu akaenda pamoja naye. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga.
Ele foi com ele, e uma grande multidão o seguiu, e eles o pressionaram de todos os lados.
25 Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili.
Uma certa mulher que teve uma descarga de sangue durante doze anos,
26 Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya.
e que tinha sofrido muitas coisas por muitos médicos, e tinha gasto tudo o que tinha, e não era melhor, mas sim piorou,
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake,
having ouviu as coisas relativas a Jesus, veio atrás dele na multidão e tocou suas roupas.
28 kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.”
Pois ela disse: “Se eu apenas tocar suas roupas, eu ficarei bem”.
29 Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.
Imediatamente o fluxo de seu sangue secou, e ela sentiu em seu corpo que estava curada de sua aflição.
30 Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”
Imediatamente Jesus, percebendo em si mesmo que o poder havia saído dele, virou-se na multidão e perguntou: “Quem tocou minhas roupas?
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’”
Seus discípulos lhe disseram: “Você vê a multidão pressionando contra você, e você diz: 'Quem me tocou?
32 Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa.
Ele olhou à sua volta para ver quem tinha feito isto.
33 Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote.
Mas a mulher, temendo e tremendo, sabendo o que havia sido feito com ela, veio e caiu diante dele, e lhe disse toda a verdade.
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
Ele disse a ela: “Filha, sua fé a fez bem. Vá em paz, e seja curada de sua doença”.
35 Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
Enquanto ele ainda falava, as pessoas vinham da casa do dirigente da sinagoga, dizendo: “Sua filha está morta”. Por que incomodar mais o Professor”?
36 Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
Mas Jesus, ao ouvir a mensagem, disse imediatamente ao dirigente da sinagoga: “Não tenha medo, apenas acredite”.
37 Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo.
Ele não permitiu que ninguém o seguisse, exceto Pedro, Tiago e João, o irmão de Tiago.
38 Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.
Ele veio à casa do regente da sinagoga, e viu um alvoroço, choroço e grande pranto.
39 Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.”
Quando ele entrou, disse-lhes: “Por que vocês fazem um alvoroço e choram? A criança não está morta, mas está dormindo”.
40 Wale watu wakamcheka kwa dharau. Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto.
Eles o ridicularizaram. Mas ele, depois de expulsá-los a todos, levou o pai da criança, sua mãe e aqueles que estavam com ele, e entrou onde a criança estava deitada.
41 Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”)
Tomando a criança pela mão, ele lhe disse: “Talitha cumi!” que significa, sendo interpretado: “Menina, eu lhe digo, levante-se!”
42 Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana.
Imediatamente a menina se levantou e caminhou, pois tinha doze anos de idade. Eles ficaram maravilhados com grande espanto.
43 Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.
Ele lhes ordenou estritamente que ninguém soubesse disso e ordenou que algo fosse dado a ela para comer.