< Marko 5 >
1 Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi.
Et ils arrivèrent à l’autre rive de la mer, dans le pays des Gadaréniens.
2 Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye.
Et aussitôt, comme il sortait du bateau, un homme possédé d’un esprit immonde,
3 Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo.
[et] qui avait sa demeure dans les sépulcres, sortant des sépulcres, le rencontra; et personne ne pouvait le lier, pas même avec des chaînes;
4 Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia.
car souvent, quand il avait été lié de fers aux pieds et de chaînes, il avait rompu les chaînes et mis les fers en pièces, et personne ne pouvait le dompter.
5 Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.
Et il était continuellement, de nuit et de jour, dans les sépulcres et dans les montagnes, criant et se meurtrissant avec des pierres.
6 Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake.
Et voyant Jésus de loin, il courut et se prosterna devant lui;
7 Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”
et, criant avec une voix forte, il dit: Qu’y a-t-il entre moi et toi, Jésus, Fils du Dieu Très-haut? Je t’adjure par Dieu, ne me tourmente pas.
8 Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”
Car il lui disait: Sors de cet homme, esprit immonde!
9 Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tuko wengi.”
Et il lui demanda: Quel est ton nom? Et il lui dit: J’ai nom Légion, car nous sommes plusieurs.
10 Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
Et il le priait instamment pour qu’il ne les envoie pas hors du pays.
11 Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima.
Et il y avait là, vers la montagne, un grand troupeau de pourceaux qui paissait.
12 Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.”
Et ils le prièrent, disant: Envoie-nous dans les pourceaux, afin que nous entrions en eux.
13 Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.
Et aussitôt Jésus le leur permit. Et les esprits immondes, sortant, entrèrent dans les pourceaux, et le troupeau se rua du haut de la côte dans la mer; [or ils étaient] environ 2 000; et ils furent étouffés dans la mer.
14 Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia.
Et ceux qui les paissaient s’enfuirent, et portèrent la nouvelle dans la ville et dans les campagnes. Et ils sortirent pour voir ce qui était arrivé;
15 Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa.
et ils viennent vers Jésus, et voient le démoniaque, assis, vêtu, et dans son bon sens, celui qui avait Légion; et ils eurent peur.
16 Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia.
Et ceux qui avaient vu [ce qui s’était passé], leur racontèrent ce qui était arrivé au démoniaque et ce qui concernait les pourceaux;
17 Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.
et ils se mirent à le prier de s’en aller de leur territoire.
18 Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja.
Et comme il montait dans le bateau, celui qui avait été démoniaque le pria [de permettre] qu’il soit avec lui.
19 Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.”
Et il ne le lui permit pas, mais lui dit: Va dans ta maison, vers les tiens, et raconte-leur tout ce que le Seigneur t’a fait, et [comment] il a usé de miséricorde envers toi.
20 Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.
Et il s’en alla, et se mit à publier en Décapolis tout ce que Jésus lui avait fait; et tous s’en étonnaient.
21 Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari.
Et Jésus, ayant encore repassé à l’autre rive, dans le bateau, une grande foule se rassembla auprès de lui; et il était au bord de la mer.
22 Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake,
Et un des chefs de synagogue, nommé Jaïrus, vient; et le voyant, il se jette à ses pieds;
23 akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.”
et il le suppliait instamment, disant: Ma fille est à l’extrémité; [je te prie] de venir et de lui imposer les mains, afin qu’elle soit sauvée, et qu’elle vive.
24 Hivyo Yesu akaenda pamoja naye. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga.
Et il s’en alla avec lui; et une grande foule le suivit, et elle le pressait.
25 Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili.
Et une femme qui avait une perte de sang depuis douze ans,
26 Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya.
et qui avait beaucoup souffert d’un grand nombre de médecins, et avait dépensé tout son bien, et n’en avait retiré aucun profit, mais plutôt allait en empirant,
27 Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake,
ayant entendu parler de Jésus, vint dans la foule par-derrière, et toucha son vêtement;
28 kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.”
car elle disait: Si je touche, ne serait-ce que ses vêtements, je serai guérie.
29 Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.
Et aussitôt son flux de sang tarit; et elle connut en son corps qu’elle était guérie du fléau.
30 Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”
Et aussitôt Jésus, connaissant en lui-même la puissance qui était sortie de lui, se retournant dans la foule, dit: Qui a touché mes vêtements?
31 Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’”
Et ses disciples lui dirent: Tu vois la foule qui te presse, et tu dis: Qui m’a touché?
32 Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa.
Et il regardait tout à l’entour pour voir celle qui avait fait cela.
33 Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote.
Et la femme, effrayée et tremblante, sachant ce qui lui était arrivé, vint et se jeta devant lui, et lui déclara toute la vérité.
34 Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
Et il lui dit: [Ma] fille, ta foi t’a guérie; va en paix, et sois guérie de ton fléau.
35 Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
Comme il parlait encore, il vient des gens de chez le chef de synagogue, disant: Ta fille est morte; pourquoi tourmentes-tu encore le maître?
36 Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
Et Jésus, ayant entendu la parole qui avait été dite, dit aussitôt au chef de synagogue: Ne crains pas, crois seulement.
37 Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo.
Et il ne permit à personne de le suivre, sinon à Pierre et à Jacques et à Jean le frère de Jacques.
38 Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.
Et il vient à la maison du chef de synagogue; et il voit le tumulte, et ceux qui pleuraient et jetaient de grands cris.
39 Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.”
Et étant entré, il leur dit: Pourquoi faites-vous ce tumulte, et pourquoi pleurez-vous? L’enfant n’est pas morte, mais elle dort.
40 Wale watu wakamcheka kwa dharau. Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto.
Et ils se riaient de lui. Mais les ayant tous mis dehors, il prend le père de l’enfant et la mère, et ceux qui étaient avec lui, et entre là où l’enfant était couchée.
41 Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”)
Et ayant pris la main de l’enfant, il lui dit: Talitha coumi; ce qui, interprété, est: Jeune fille, je te dis, lève-toi.
42 Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana.
Et aussitôt la jeune fille se leva et marcha, car elle avait douze ans; et ils furent transportés d’une grande admiration.
43 Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.
Et il leur enjoignit fort que personne ne le sache; et il dit qu’on lui donne à manger.