< Marko 4 >

1 Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
Again he began to teach beside the sea, and a large crowd gathered around him. He stepped into a boat that was on the sea, and he sat down in it. The whole crowd was on the shore beside the sea.
2 Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
He taught them many things in parables, and in his teaching, this is what he said to them.
3 “Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
“Listen, the farmer went out to sow his seed.
4 Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
As he sowed, some seed fell on the road, and the birds came and devoured it.
5 Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
Other seed fell on the rocky ground, where it did not have much soil. Immediately it sprang up, because it did not have deep soil.
6 Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
But when the sun rose, the plants were scorched, and because they had no root, they dried up.
7 Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
Other seed fell among the thorn plants. The thorn plants grew up and choked it, and it did not produce a crop.
8 Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
Other seed fell into good soil and it produced a crop growing up and increasing thirty, sixty, and even a hundred times.”
9 Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
Then he said, “Whoever has ears to hear, let him hear!”
10 Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
When Jesus was alone, those who were close to him and with the twelve asked him about the parables.
11 Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
He said to them, “To you is given the mystery of the kingdom of God. But to those outside everything is in parables,
12 ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
so that when they look, yes they look, but do not see, and so that when they hear, yes they hear, but do not understand, or else they would turn and God would forgive them.”
13 Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
Then he said to them, “Do you not understand this parable? How then will you understand all the other parables?
14 Yule mpanzi hupanda neno.
The farmer who sows his seed is the one who sows the word.
15 Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
These are the ones that fall beside the road, where the word was sown, but when they hear it, Satan immediately comes and takes away the word that was sown in them.
16 Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
These are the ones that are sown on rocky ground, who, when they hear the word, immediately receive it with joy.
17 Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
They have no root in themselves, but endure for a short time. Then tribulation or persecution comes because of the word, and immediately they stumble.
18 Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
The others are the ones that were sown among the thorns. They hear the word,
19 lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
but the cares of the world, the deceitfulness of riches, and the desires of other things enter in and choke the word, and it does not produce a crop. (aiōn g165)
20 Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
Then those that were sown in the good soil are the ones who hear the word and receive it, and they produce crops—thirty, sixty, or a hundred times what was sown.”
21 Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
Jesus said to them, “Do you bring a lamp inside the house to put it under a basket, or under the bed? You bring it in and you put it on a lampstand.
22 Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
For nothing is hidden that will not be known, and nothing is secret that will not come out into the open.
23 Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
If anyone has ears to hear, let him hear!”
24 Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
He said to them, “Pay attention to what you hear, for the measure you use will be measured to you, and more will be added to you.
25 Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
Because whoever has, to him will be given more, and whoever does not have, even what he has will be taken.”
26 Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
He also said, “The kingdom of God is like a man who sows his seed on the ground.
27 Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
He sleeps at night and gets up by day, and the seed sprouts and grows, though he does not know how.
28 Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
The earth bears grain by itself: First the blade, then the ear, then the mature grain in the ear.
29 Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
When the crop is ripe, he immediately sends in the sickle because the harvest has come.”
30 Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
Again he said, “To what can we compare the kingdom of God, or what parable can we use to explain it?
31 Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
It is like a mustard seed which, when it is sown, is the smallest of all the seeds on earth.
32 Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
Yet, when it is sown, it grows and becomes greater than all the garden plants, and it forms large branches, so that the birds of heaven can make their nests in its shade.”
33 Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
With many parables like this he spoke the word to them, as much as they were able to understand,
34 Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
and he did not speak to them without a parable. But when he was alone, he explained everything to his own disciples.
35 Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
On that day, when evening had come, he said to them, “Let us go over to the other side.”
36 Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
So they left the crowd, taking Jesus with them, just as he was, in the boat. There were other boats going along with him.
37 Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
Just then a violent windstorm arose and the waves were breaking into the boat so that the boat was almost full of water.
38 Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
But Jesus himself was in the stern, asleep on a cushion. They woke him up, saying, “Teacher, do you not care that we are about to die?”
39 Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
He got up, rebuked the wind, and said to the sea, “Peace! Be still!” Then the wind ceased, and there was a great calm.
40 Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
Then he said to them, “Why are you afraid? Do you still not have faith?”
41 Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”
They were filled with great fear and said to one another, “Who then is this, because even the wind and the sea obey him?”

< Marko 4 >