< Marko 3 >
1 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
And he entered again into a synagogue; and there was a man there having a withered hand;
2 Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
and they watched him, whether he would heal him on the sabbath, that they might accuse him.
3 Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
And he saith to the man having the withered hand, Stand up in the midst.
4 Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
And he saith to them, Is it lawful to do good on the sabbath, or to do evil? to save life, or to kill? But they were silent.
5 Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
And looking round on them with anger, being grieved for the hardness of their hearts, he saith to the man, Stretch forth thy hand. And he stretched it forth; and his hand was restored.
6 Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
And the Pharisees went forth, and immediately had a consultation with the Herodians against him, how they might destroy him.
7 Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
And Jesus withdrew with his disciples to the lake; and a great multitude from Galilee, and from Judaea followed;
8 Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
and from Jerusalem, and from Idumaea, and from beyond the Jordan, and the people about Tyre and Sidon, a great multitude, when they heard what great things he was doing, came to him.
9 Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
And he gave direction to his disciples, that a boat should be in readiness for him because of the multitude, that they might not throng him.
10 Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
For he had healed many, so that as many as had plagues pressed upon him to touch him.
11 Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
And the unclean spirits, when they saw him, fell down before him, and cried out, saying, Thou art the Son of God.
12 Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
And he strictly charged them that they should not make him known.
13 Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
And he goeth up into the mountain, and calleth to him whom he would; and they came to him.
14 Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
And he appointed twelve to be with him, and whom he might send forth to preach,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
and to have authority to cast out demons. And he appointed the twelve,
16 Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
and Simon he surnamed Peter;
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
and James the son of Zebedee, and John the brother of James; and he surnamed them Boanerges, that is, Sons of thunder;
18 Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James the son of Alphaeus, and Thaddaeus, and Simon of Cana,
19 na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
and Judas Iscariot, who betrayed him. And he cometh into the house.
20 Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
And again a multitude cometh together, so that they could not so much as eat bread.
21 Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
And his relations hearing of it went out to lay hold of him; for they said, He is beside himself.
22 Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
And the scribes who came down from Jerusalem said, He hath Beelzebul; and, He casteth out the demons through the prince of the demons.
23 Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
And calling them to him, he said to them in parables: How can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
And if a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand;
25 Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
and if a house be divided against itself, that house will not be able to stand;
26 Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
and if Satan rise up against himself, he is divided, and cannot stand, but hath an end.
27 Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
Moreover, no one can enter into a strong man's house, and plunder his goods, unless he first bind the strong man; and then he will plunder his house.
28 Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
Truly do I say to you, All sins will be forgiven the sons of men, and the blasphemies wherewith they shall blaspheme;
29 Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn , aiōnios )
but he that shall blaspheme against the Holy Spirit hath no forgiveness forever, but is exposed to everlasting sin.— (aiōn , aiōnios )
30 Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
Because they said, He hath an unclean spirit.
31 Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
And his mother and his brothers came; and, standing without, sent to him, to call him.
32 Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
And a multitude was sitting about him; and they say to him, Lo! thy mother and thy brothers and thy sisters are without, seeking for thee.
33 Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
And he answering saith to them, Who is my mother, and my brothers?
34 Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
And looking round on those who sat about him, he saith, Behold my mother and my brothers.
35 Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
Whoever shall do the will of God, he is my brother, and sister, and mother.