< Marko 3 >

1 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
Again he went into a synagogue where there was a man with his hand withered.
2 Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
And they kept watching Jesus to see whether he would cure him on the Sabbath; so as to have some charge to bring against him.
3 Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
"Stand up," Jesus said to the man with the withered hand, "and come forward."
4 Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
Then he asked them. "Is it lawful to do good on the Sabbath Day, or to do harm? to save a life, or to destroy it?"
5 Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
They were silent. Then looking around upon them with anger, and deeply grieved by the hardening of their hearts, he said to the man, "Stretch out your hand!" He stretched it out, and the hand was at once completely restored.
6 Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
As soon as they came out, the Pharisees plotted against him with the Herodians, in order to destroy him.
7 Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
Then Jesus withdrew to the sea with his disciples; and a great crowd of people from Galilee followed.
8 Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
From Judea, too, and Jerusalem, and Idumea, and from beyond Jordan, and from the district of Tyre and Sidon, they came to him a vast multitude, because they heard what he was doing.
9 Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
So he directed his disciples to keep a little boat in readiness for him, because of the crowd, to prevent their crushing him.
10 Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
For he had healed so many that all the people who had ailments pressed upon him so as to touch him.
11 Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
And whenever the unclean spirits beheld him, they threw themselves down at his feet, screaming out, "You are the Son of God."
12 Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
But over and over, he strictly forbade them to make him known.
13 Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
Then he went up the hillside and called to him those whom he chose, and they came to him.
14 Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
Twelve of them whom he also called "Apostles," he appointed to be with him, and also that he might send them out to preach,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
and to have authority to cast out demons.
16 Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
There was Simon, whom he surnamed Peter,
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
and James(them he surnamed Boanerges, that is, Sons of Thunder),
18 Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and Jamesthe son of Alphaeus, and Thaddeus, and Simon the Zealot,
19 na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
and Judas Iscariot who betrayed him.
20 Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
Then he went into a house, but again such a multitude assembled that they could not get their food.
21 Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
When his relatives heard of it, they came to take possession of him, for they said, "He is out of his mind."
22 Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
The Scribes also who had come down from Jerusalem, said, "He is Beelzebub," and, "He casts out demons by the power of the Prince of the demons."
23 Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
So when he had called them to him he spoke to them in parables. "How," said he, "can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
If a kingdom be divided against itself, that kingdom cannot stand;
25 Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
if a household be divided against itself, that household cannot stand;
26 Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
and if Satan has revolted against himself, and is divided, he cannot stand. Nay, he meets his end!
27 Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
"Indeed, no one can enter the strong man’s house and carry off his property without first binding the strong man; then he can plunder his house.
28 Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
In solemn truth I tell you that the sons of men shall be forgiven all their sins and all the blasphemies they may utter,
29 Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
but he who blasphemes against the Holy Spirit is never forgiven. Nay, he is in the grasp of an eternal sin." (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
Because they kept saying, "He has an unclean spirit."
31 Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
Then his mother and his brothers came up, and standing outside, they sent a messenger to him to call him.
32 Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
Now a crowd was sitting round him and they told him, "See! your mother and your brothers and sisters are outside, wanting to see you."
33 Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
"Who are my mother and my brothers?" he replied.
34 Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
Then, with a glance at those who were in the circle sitting around him, he added.
35 Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
"Here are my mother and my brothers! Whoever does the will of God, that one is my brother and sister and mother."

< Marko 3 >