< Marko 3 >

1 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
耶穌又進了會堂,在那裏有一個人枯乾了一隻手。
2 Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
眾人窺探耶穌,在安息日醫治不醫治,意思是要控告耶穌。
3 Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
耶穌對那枯乾一隻手的人說:「起來,站在當中。」
4 Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
又問眾人說:「在安息日行善行惡,救命害命,哪樣是可以的呢?」他們都不作聲。
5 Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
耶穌怒目周圍看他們,憂愁他們的心剛硬,就對那人說:「伸出手來!」他把手一伸,手就復了原。
6 Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
法利賽人出去,同希律一黨的人商議怎樣可以除滅耶穌。
7 Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
耶穌和門徒退到海邊去,有許多人從加利利跟隨他。
8 Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
還有許多人聽見他所做的大事,就從猶太、耶路撒冷、以土買、約旦河外,並泰爾、西頓的四方來到他那裏。
9 Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
他因為人多,就吩咐門徒叫一隻小船伺候着,免得眾人擁擠他。
10 Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
他治好了許多人,所以凡有災病的,都擠進來要摸他。
11 Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
污鬼無論何時看見他,就俯伏在他面前,喊着說:「你是上帝的兒子。」
12 Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
耶穌再三地囑咐他們,不要把他顯露出來。
13 Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
耶穌上了山,隨自己的意思叫人來;他們便來到他那裏。
14 Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
他就設立十二個人,要他們常和自己同在,也要差他們去傳道,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
並給他們權柄趕鬼。
16 Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
這十二個人有西門(耶穌又給他起名叫彼得),
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
還有西庇太的兒子雅各和雅各的兄弟約翰(又給這兩個人起名叫半尼其,就是雷子的意思),
18 Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
又有安得烈、腓力、巴多羅買、馬太、多馬、亞勒腓的兒子雅各,和達太,並奮銳黨的西門,
19 na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
還有賣耶穌的加略人猶大。
20 Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
耶穌進了一個屋子,眾人又聚集,甚至他連飯也顧不得吃。
21 Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
耶穌的親屬聽見,就出來要拉住他,因為他們說他癲狂了。
22 Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
從耶路撒冷下來的文士說:「他是被別西卜附着」;又說:「他是靠着鬼王趕鬼。」
23 Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
耶穌叫他們來,用比喻對他們說:「撒但怎能趕出撒但呢?
24 Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
若一國自相紛爭,那國就站立不住;
25 Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
若一家自相紛爭,那家就站立不住。
26 Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
若撒但自相攻打紛爭,他就站立不住,必要滅亡。
27 Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
沒有人能進壯士家裏,搶奪他的家具;必先捆住那壯士,才可以搶奪他的家。
28 Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
我實在告訴你們,世人一切的罪和一切褻瀆的話都可得赦免;
29 Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
凡褻瀆聖靈的,卻永不得赦免,乃要擔當永遠的罪。」 (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
這話是因為他們說:「他是被污鬼附着的。」
31 Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
當下,耶穌的母親和弟兄來,站在外邊,打發人去叫他。
32 Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
有許多人在耶穌周圍坐着,他們就告訴他說:「看哪,你母親和你弟兄在外邊找你。」
33 Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
耶穌回答說:「誰是我的母親?誰是我的弟兄?」
34 Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
就四面觀看那周圍坐着的人,說:「看哪,我的母親,我的弟兄。
35 Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
凡遵行上帝旨意的人就是我的弟兄姊妹和母親了。」

< Marko 3 >