< Marko 3 >

1 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono.
耶稣回到会堂,那里有个男人的一只手已经残疾。有人问耶稣:“在安息日可以治病吗?”
2 Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki.
众人观察他会不会在安息日医治那个人,好去控告他。
3 Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”
耶稣对那残手之人说:“起来,站在大家面前!”
4 Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.
然后又对他们说:“在安息日能做哪件事,好事还是坏事?救命还是害命?”众人不发一声。
5 Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa!
耶稣怒目环视他们,为他们的铁石心肠感到难过。于是就对那人说:“伸出手来!”那人把手一伸,手就复原了。
6 Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.
法利赛人离开后,立刻与希律党人一起商量如何对付耶稣和除掉他。
7 Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata.
耶稣和门徒回到海边,一大群人跟着他。
8 Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni.
还有许多人听说了他所做的一切,纷纷从犹太、耶路撒冷、以土迈、约旦河外和推罗、西顿等地方前来跟随他。
9 Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga.
因为人太多,耶稣就吩咐门徒为他准备一条小船,免得众人拥挤他。
10 Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa.
他医好了许多人,所有病患都挤过来希望触摸他。
11 Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.”
恶灵每次看到他,就仆倒在他面前,大声喊叫说:“你是上帝之子!”
12 Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.
但耶稣严厉要求他们,不要把他的身份张扬出去。
13 Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia.
耶稣继续去往丘陵乡村,召唤那些他需要的人,那些人于是纷纷聚来。
14 Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
他选择了十二个人,称他们为师徒。他们与耶稣在一起,接受耶稣的派遣,宣传福音,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
耶稣还赋予他们驱魔的力量。
16 Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
他选择的十二个人是:西门(耶稣给他起名叫彼得),
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
西庇太的大儿子雅各和他弟弟约翰(耶稣给约翰起名叫半尼其,即“雷之子”),
18 Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
安得烈、腓力、巴多罗迈、马太、多马、亚勒腓的儿子雅各、达太、激进派西门
19 na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
以及后来出卖耶稣的加略人犹大。
20 Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula.
耶稣走进屋子,民众又聚过来,他们甚至没有时间吃饭。
21 Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”
耶稣的家人听闻这一切,就跑过来想把他带走,说:“他疯了。”
22 Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli! Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”
但来自耶路撒冷的宗教老师说:“别西卜附在他身上!”又说:“他靠魔鬼之王的力量驱除魔鬼。”
23 Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani?
但耶稣把他们叫过来,讲了一个比喻:“撒旦怎能赶逐撒旦呢?
24 Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
一个国家若自相残杀,这个国家就无以为续,
25 Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
一个家庭若内部纷争,这个家庭就会垮掉。
26 Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia.
如果撒旦分裂,哥和拿就不会持久,很快就会灭亡。
27 Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake.
很显然,一个人闯入壮汉的家想要抢东西,但必须先把壮汉捆绑起来,才可以如愿以偿。
28 Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa.
告诉你们实话,世人的一切罪行和亵渎之话,都可以得到赦免。
29 Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
但亵渎圣灵者,永世不得赦免,因为他们犯下永世罪过。” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”
(耶稣这样说是因为他们说他“有恶灵附体。”
31 Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita.
耶稣的母亲和弟弟来了,站在外面向他传了个口信,叫他出来。
32 Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”
人群围坐在耶稣身边,对他说:“你母亲和兄弟在外面找你。”
33 Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”
耶稣回答:“谁是我的母亲?谁是我的兄弟?”
34 Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
他环顾身边围坐之人,说:“这就是我的母亲!我的兄弟!
35 Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
凡遵行上帝旨意之人,就是我的母亲和兄弟姐妹。”

< Marko 3 >