< Marko 2 >

1 Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani.
tadanantaraM yIzai katipayadinAni vilambya punaH kapharnAhUmnagaraM praviSTE sa gRha Asta iti kiMvadantyA tatkSaNaM tatsamIpaM bahavO lOkA Agatya samupatasthuH,
2 Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno.
tasmAd gRhamadhyE sarvvESAM kRtE sthAnaM nAbhavad dvArasya caturdikSvapi nAbhavat, tatkAlE sa tAn prati kathAM pracArayAnjcakrE|
3 Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne.
tataH paraM lOkAzcaturbhi rmAnavairEkaM pakSAghAtinaM vAhayitvA tatsamIpam AninyuH|
4 Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
kintu janAnAM bahutvAt taM yIzOH sammukhamAnEtuM na zaknuvantO yasmin sthAnE sa AstE taduparigRhapRSThaM khanitvA chidraM kRtvA tEna mArgENa sazayyaM pakSAghAtinam avarOhayAmAsuH|
5 Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
tatO yIzustESAM vizvAsaM dRSTvA taM pakSAghAtinaM babhASE hE vatsa tava pApAnAM mArjanaM bhavatu|
6 Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao,
tadA kiyantO'dhyApakAstatrOpavizantO manObhi rvitarkayAnjcakruH, ESa manuSya EtAdRzImIzvaranindAM kathAM kutaH kathayati?
7 “Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
IzvaraM vinA pApAni mArSTuM kasya sAmarthyam AstE?
8 Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
itthaM tE vitarkayanti yIzustatkSaNaM manasA tad budvvA tAnavadad yUyamantaHkaraNaiH kuta EtAni vitarkayatha?
9 Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’?
tadanantaraM yIzustatsthAnAt punaH samudrataTaM yayau; lOkanivahE tatsamIpamAgatE sa tAn samupadidEza|
10 Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza,
kintu pRthivyAM pApAni mArSTuM manuSyaputrasya sAmarthyamasti, Etad yuSmAn jnjApayituM (sa tasmai pakSAghAtinE kathayAmAsa)
11 “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
uttiSTha tava zayyAM gRhItvA svagRhaM yAhi, ahaM tvAmidam AjnjApayAmi|
12 Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
tataH sa tatkSaNam utthAya zayyAM gRhItvA sarvvESAM sAkSAt jagAma; sarvvE vismitA EtAdRzaM karmma vayam kadApi nApazyAma, imAM kathAM kathayitvEzvaraM dhanyamabruvan|
13 Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha.
tadanantaraM yIzustatsthAnAt punaH samudrataTaM yayau; lOkanivahE tatsamIpamAgatE sa tAn samupadidEza|
14 Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.
atha gacchan karasanjcayagRha upaviSTam AlphIyaputraM lEviM dRSTvA tamAhUya kathitavAn matpazcAt tvAmAmaccha tataH sa utthAya tatpazcAd yayau|
15 Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata.
anantaraM yIzau tasya gRhE bhOktum upaviSTE bahavaH karamanjcAyinaH pApinazca tEna tacchiSyaizca sahOpavivizuH, yatO bahavastatpazcAdAjagmuH|
16 Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
tadA sa karamanjcAyibhiH pApibhizca saha khAdati, tad dRSTvAdhyApakAH phirUzinazca tasya ziSyAnUcuH karamanjcAyibhiH pApibhizca sahAyaM kutO bhuMktE pivati ca?
17 Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
tadvAkyaM zrutvA yIzuH pratyuvAca, arOgilOkAnAM cikitsakEna prayOjanaM nAsti, kintu rOgiNAmEva; ahaM dhArmmikAnAhvAtuM nAgataH kintu manO vyAvarttayituM pApina Eva|
18 Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”
tataH paraM yOhanaH phirUzinAnjcOpavAsAcAriziSyA yIzOH samIpam Agatya kathayAmAsuH, yOhanaH phirUzinAnjca ziSyA upavasanti kintu bhavataH ziSyA nOpavasanti kiM kAraNamasya?
19 Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga.
tadA yIzustAn babhASE yAvat kAlaM sakhibhiH saha kanyAyA varastiSThati tAvatkAlaM tE kimupavastuM zaknuvanti? yAvatkAlaM varastaiH saha tiSThati tAvatkAlaM ta upavastuM na zaknuvanti|
20 Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
yasmin kAlE tEbhyaH sakAzAd varO nESyatE sa kAla Agacchati, tasmin kAlE tE janA upavatsyanti|
21 “Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi.
kOpi janaH purAtanavastrE nUtanavastraM na sIvyati, yatO nUtanavastrENa saha sEvanE kRtE jIrNaM vastraM chidyatE tasmAt puna rmahat chidraM jAyatE|
22 Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
kOpi janaH purAtanakutUSu nUtanaM drAkSArasaM na sthApayati, yatO nUtanadrAkSArasasya tEjasA tAH kutvO vidIryyantE tatO drAkSArasazca patati kutvazca nazyanti, ataEva nUtanadrAkSArasO nUtanakutUSu sthApanIyaH|
23 Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke.
tadanantaraM yIzu ryadA vizrAmavArE zasyakSEtrENa gacchati tadA tasya ziSyA gacchantaH zasyamanjjarIzchEttuM pravRttAH|
24 Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”
ataH phirUzinO yIzavE kathayAmAsuH pazyatu vizrAmavAsarE yat karmma na karttavyaM tad imE kutaH kurvvanti?
25 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?
tadA sa tEbhyO'kathayat dAyUd tatsaMgginazca bhakSyAbhAvAt kSudhitAH santO yat karmma kRtavantastat kiM yuSmAbhi rna paThitam?
26 Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
abiyAtharnAmakE mahAyAjakatAM kurvvati sa kathamIzvarasyAvAsaM pravizya yE darzanIyapUpA yAjakAn vinAnyasya kasyApi na bhakSyAstAnEva bubhujE saggilOkEbhyO'pi dadau|
27 Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
sO'paramapi jagAda, vizrAmavArO manuSyArthamEva nirUpitO'sti kintu manuSyO vizrAmavArArthaM naiva|
28 Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
manuSyaputrO vizrAmavArasyApi prabhurAstE|

< Marko 2 >